• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC MALIMA AZINDUA WIKI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Posted on: November 24th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mheshimiwa Adam Malima, amewahimiza wananchi wa mkoa huo na wa mikoa jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye shughuli zote zinazoendelea kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Morogoro, ikiwemo kupata huduma za upimaji wa afya na kupata elimu ya VVU na UKIMWI itakayokuwa ikitolewa kila siku na wadau mbalimbali, katika kipindi chote cha wiki ya maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani.

Mhehsimiwa Malima ameyasema hayo katika hotuba yake ya uzinduzi wa Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani, uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Morogoro leo tarehe 24.11.2023, ambapo pia alisema kwamba baada ya maadhimisho hayo, kama Mkoa wa Morogoro na Tanzania kwa ujumla tutafikia malengo ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI (UNAIDS), ya kuwa na sifuri tatu ambazo ni sifuri ya maambukizi mapya ya VVU, sifuri ya vifo vitokanavyo na maambukizi ya VVU na UKIMWI na sifuri ya unyanyapaa.

Vilevile, katika hotuba yake hiyo, mheshimiwa Malima amesema, Mkoa wa Morogoro mpaka sasa umefanya juhudi kubwa sana katika kupambana na maambukizi ya VVU na UKIMWI, kwani katika vituo 629 vya kutolea huduma za afya vilivyopo ndani ya mkoa, vituo 516 vina uwezo wa kutoa huduma za VVU na UKIMWI, vituo 359 vinatoa huduma ya kupima VVU, vituo 112 vinatoa huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU, na vituo 368 vinatoa huduma za kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama mwenye VVU kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito, kujifungua na wakati wa unyonyeshaji.

Kwa upande mwingine, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI nchini (NACOPHA), ndugu Emmanuel Msinga ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI nchini kuendelea kupata bure dawa za kufubaza virusi (ARV’s), na kutoa mikopo kwa vikundi wezeshi vya watu hao ili kuwasaidia kuondokana na umaskini ambao wakati mwingine unasababishwa na unyanyapaa katika jamii zinazowazunguka.

Naye mwakilishi wa Wizara ya Afya, ndugu Zeye Nkomela, amesema Wizara ya Afya inaendelea kuimarisha huduma za VVU kwa watu wanaoishi na maambukizi na kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu isemayo “Jamii Iongoze Kutokomeza UKIMWI”, Wizara inaamini kwamba kufikia mwaka 2030 Serikali itakuwa imefanikiwa kufikia malengo ya kutokomeza maambukizi ya VVU nchini.  

Aidha, Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani inaenda sambamba na Kampeni ya Siku 16 ya Kupinga Ukatili wa Kijinsia yenye kaulimbiu isemayo “Wekeza Kuzuia Ukatili wa Kijinsia, ambayo pia imezinduliwa rasmi leo na kilele chake kitakuwa tarehe 10.12.2023, ikiwa na lengo la kusisitiza jamii kuwekeza zaidi katika kuzuia vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na wasichana kwa kuwa ndilo kundi linalosadikiwa kupitia changamoto zaidi za vitendo vya ukatili.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa