• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC MWASSA AWATAKA VIONGOZI KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Posted on: September 14th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Fatma Mwassa, amewaagiza Viongozi wa Halmashauri kufanya ziara za kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi badala ya kusubiri viongozi wa Serikali ya mkoa ndio wazitatue changamoto za wananchi.

Ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara wa kusikiliza na kutatua kero za Wananchi Kata ya Kihonda, uliofanyika Septemba 13/2022 katika eneo la Ofisi ya Kata ya Kihonda .



RC Mwassa, amesema Serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo lakini wananchi hawajui kinachoendelea kwasababu viongozi ambao wanapaswa kuwaeleza hawafanyi hivyo.

"Ni muhimu mno kufanya mikutano ya wananchi kusikiliza kero zao, wahamasisheni Madiwani, makatibu tarafa wafanye ziara, mkoa wetu umekuwa ukipata fedha nyingi za miradi ya maendeleo ni wajibu wetu kama viongozi kuzisimamia ili zilete tija katika maendeleo," Amesema RC Mwassa.

Aidha, amesema kuwa kusikiliza ni moja ya uwajibikaji bora kwa wananchi, hivyo kutofanya mikutano ya hadhara kwa wananchi kuna sababisha kuibuka kwa kero nyingi ambazo kama ziara zingekuwa zinafanyika hali hiyo isingejitokeza.

Katika hatua nyingine, amepiga marufuku Watendaji wa Kata na Mitaa na wenyeviti wa Serikali za Mitaa kutojihusisha na uuzaji wa ardhi, kwani kufanya hivyo kuna pelekea kuwa na mlundikano wa migogoro ya ardhi kila uchwao.


 Hata hivyo, RC Mwassa, amewaagiza Viongozi wa Wilaya na Halmashauri kwa kushirikiana na wataalam wa ardhi kufuatilia migogoro yote ya ardhi na kuipatia ufumbuzi na kuiweka kwenye 'data base'.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa, amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa yote aliyoyaagiza atayafanyia kazi kwa kushirikiana na Watendaji wa Halmashauri za Mkoa.

RAS Mussa, amewataka Watumishi wa Umma kuhakikisha kila mtumishi awe na sheria ya Serikali za Mitaa ambayo sheria hiyo ndio inayoonesha majukumu yao kwa ujumla katika kuwatumikia wananchi.

"Mkasome sheria za Serikali za Mitaa, lakini kila mtumishi awe na Ilani ya CCM inayoelekeza mambo ya kufanya , pia tuangalie maelekezo ya mkoa yanataka nini , tujenge utamaduni wa kuwajibishana ili mifumo ifanye kazi , kwa kufanya haya tunaamini kabisa tutaweza kufikia viwango vya juu vya utendaji " Amesema RAS Mussa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa