• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

SEKTA YA AFYA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO KUENDELEA KUBORESHWA,SENGO AREJESHWA TENA NAIBU MEYA

Posted on: July 19th, 2019

Idadi ya wanawake wajawazito wanaojifungulia katika Vituo vya huduma Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imeongezeka kutoka asilimia 97 kwa mwaka 2017/ 2018 hadi kufikia asilimia 99 mwaka 2018/2019.

Licha ya ongezeko hilo , vituo vya Afya vinavyotoa huduma ya kupima wingi wa damu kwa akina mama wajawazito vimeongezeka kutoka vituo vitatu mwaka 2017/2018 na kufikia 19 kwa mwaka 2018/2019.

Meya wa Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga alisema hayo katika mkutano wa kawaida wa mwaka wa Baraza la Madiwani ambao ulioambatana na uchangzi wa nafasi ya Naibu Meya pamoja na wenyeviti wa kamati ya Mipangomiji na Mazingira, Kamati ya Maadili ya Madiwani na Kamati ya huduma za jamii.

Kihanga alisema ,Halmashauri  kwa kushirikiana na Madiwani , Watendaji na wananchi imefanikisha kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo kwenye sekta za uchumi na uwekezaji ,miundombinu , ardhi, elimu ya msingi na sekondari, mazingira ,maji , kilimo, utawala bora , afya na nyinginezo.

Kwa upande wa sekta ya afya alisema,kumekuwepo na kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kutoka kituo kimoja hadi kufikia viwili mwaka 2018/2019.

Alisema ,Halmashauri pia imeweza kununua mashine mbili za Ultrasound na kuziweka katika vituo vya Afya Mafiga na Kingolwira pamoja na ukarabati wa Kituo cha Afya Kingolwira unaoendelea sambamba na ujenzi wa wodi ya wazazi kwenye Kituo cha Afya Saba Saba.

Kuhusu mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF III) Meya alisema ,Halmashauri ina jumla ya walengwa 2,850 hadi kufikia Juni , 2019 wanaishi katika mitaa 164 kutoka kwenye kata zote 29 ambao wamenufaika kwa jumla ya Sh milioni 378.5 kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019.

Hata hivyo alisema , jumla ya kaya 874 za wa TASAF III wameweza kujiwekea akiba kwa ajili ya kuhudumia matibabu ya familia zao kwa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) iliyoboreshwa baada ya kuhamasishaji.

Wakati huo huo , Baraza la Madiwani lilimchagua kwa mara nyingine tena Diwani wa Kata ya Kiwanja cha Ndege , Isihaka Sengo (CCM) kuwa Naibu Meya baada ya kupata kura 34 na kumshinda Diwani wa Viti Maalumu, Scolastika Mkude ( Chadema ) aliyepata kura tano ambazo ni za madiwani wa Chama hicho.

Mkurugenzi wa Manispaa John Mgalula pia aliwatangaza wenyeviti wa kamati za baraza waliochanguliwa na madiwani wenzao wote kutoka CCM ni Spear Komanya mwenyekiti wa kamati ya huduma ya jamii , Ally Kalungwana mwenyekiti wa kamati ya Mipangomiji na Mazingira , na Madaraka Byanguze mwenyekiti wa kamati ya maadili ya Madiwani wakati Naibu Meya akiingia moja kwa moja kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ukimwi.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa