• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

UNUNUZI WA VYEO SEKTA YA ELIMU,TABIA HIYO HAIKUBARIKI..WAZIRI KAIRUKI.

Posted on: January 11th, 2023

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI), Angellah Kairuki amewaonya watumishi katika sekta ya elimu wanaodaiwa kutumia madaraka yao kwa kutoa vyeo kwa misingi ya Rushwa kuacha mara moja kabla hawajabainika na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Waziri Kairuki alisema hayo Januari 9, 2023 mjini Morogoro wakati akifungua kikao kazi cha mapitio ya tathimini ya utekelezaji wa shughuli za uboreshaji na usimamizi wa elimu kwa mwaka 2022 na mpango mwaka 2023.

Waziri amesema wapo baadhi ya watumishi wa sekta ya elimu wanaodaiwa kutoa rushwa ili kupata madaraka ya Ofisa elimu wa wilaya na ngazi nyingine jambo ambalo ni kinyume na taratibu za kiutumishi na ni kosa kisheria.

Kairuki amesema hategemei endapo mkuu wa shule amepata cheo hicho kwa kutoa rushwa kwani hataweza kufanya kazi kwa uadilifu, kwa maana lazima atafanya kila njia ili aweze kurejesha kile alichotoa.

" Nasema kama mambo haya yapo yakome mara moja, Serikali ipo makini, hatutawafumbia macho wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivi na kwamba wakibainika watachukuliwa hatua kali za kisheria "amesema Waziri Kairuki

Waziri amesema kwa upande wa viongozi kuna nyakati wamepewa madaraka ya kukathimisha uongozi na kupendekeza wanaostahili kushika nafasi mbalimbali za uongozi na kuwataka kuwa macho.

“ Tumetoa mwongozo wa teuzi mbalimbali katika sekta yetu ya elimu katika mamlaka za Serikali za mitaa , ni vema tukafuata miongozo hiyo” amesema Waziri

Waziri amesema zipo tuhuma au yako maneno ya kwamba wengine wameingia kama maofisa elimu kwa kutoa rushwa , wapo wengine wamepata ukuu wa shule kwa kutoa fedha.

“Tutaendelea kuyangalia kwa umakini mkubwa,tunataka mtu anayepata nafasi ya uongozi awe ni yule kweli ni mahili yule anayekidhi vigezo vyote vilivyowekwa” amesema Kairuki

Pia amesema yako maneno ya kwamba wako baadhi ya maofisa elimu ili aweze kuteua baadhi ya wakuu wa shule ukipewa nafasi lazima watoe fedha na kila mwezi wanapekelewa fedha .

“ Kama yapo hayo kwa maofisa elimu yakome , kwa wakuu wa shule yakome na ikitokea wewe mkuu wa shule unashinikizo la kutoa fedha kwa yoyote …nitaancha namba zangu hapa tafadhari usisite kuweza kutoa taarifa na tutawalinda’ amesema Waziri

Waziri amesema Ofisi yake ipo macho na kwamba mabadiliko mengi yataendelea kufanyika na pia hatua zitachukuliwa za kisheria na hata za kijinai zitachukuliwa dhidi ya hao na kutoa rai kama wapo mambo hayo yakome.

Waziri pia amewatahadharisha watumishi wa umma wanaokiuka taratibu na kanuni za kiutumishi kwa kutoa lugha chafu kwa wananchi wanashungulikiwa kulingana na sheria za kinidhamu na kwamba itawekwa mitego kila sehemu zinapotolewa huduma za kijamii kwa watawatega kwa maswali ili mjibu lugha chafu tuwabaini wenye tabia za kutoa lugha chafu ili tuwachukulia hatua.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa