• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

VYAMA VYA USHIRIKA VYATAKIWA KUTUMIA TEHAMA KATIKA UTENDAJI KAZI WAKE.

Posted on: May 19th, 2023

VYAMA vya ushirika hapa nchini vimeshauriwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika uendeshaji wa shughuli zake za kila siku ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia na kurahisisha kuongeza ufanisi wa kazi katika utendaji wa vyama hivyo.

Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa Mei 17 mwaka huu wakati akifungua mafunzo ya ya usimamizi kwa Maafisa wa vyama vya ushirika wa kanda ya mashariki inayojumuisha Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro yaliyofanyika katika hoteli ya Savoy Mkoani Morogoro.

Dkt. Mussa amebainisha kuwa ili vyama vya ushirika viweze kujiendesha kibiashara ni wazi suala la TEHAMA kwao halikwepeki na linatakiwa kuwekewa mkazo wa hali ya juu lengo likiwa ni kuondoa dosari ndogo ndogo zinazojitokeza mara kwa mara katika vyama vya Ushirika, hivyo kutojiendesha kibiashsara.

“...tuhakikishe tunatumia ipasavyo tehama, dunia inaendelea na teknolojia inakua kwa kasi, na kwa hakika ikituacha nyuma hakuna kitu kitakachoendelea... kwa hiyo kuna haja ya kuhakikisha kuwa Tume ya maendeleo ya ushirika na vyama vya ushirika vinakuwa na matumizi ya kiwango kikubwa cha Tehama...” amesema Dkt. Mussa.

Akibainisha Changamoto za Vyama hivyo amesema kuna ukosefu wa maadili na uadilifu miongoni mwa viongozi wa vyama hivyo na kushindwa kufikia ndoto waliyo nayo wakulima waliojiunga na vyama vya ushirika.

Katika Hatua nyingine Katibu Tawala huyo ameiagiza Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC)kuhakikisha Tume hiyo inafanya kazi kwa karibu na Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuondoa migogoro ya mara kwa mara inayojitokeza kwenye vyama vya Ushirika na kuboresha maisha ya wananchi wa chini ambao ndio walengwa namba moja wa vyama hivyo.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro Ndg. Solomon Kasaba amesema wanatarajia kuona mabadiliko ya uendeshaji wa vyama vya Ushirika na kwamba haitaleta maana kama pamoja na kupata mafunzo hayo bado ushirika utajiendesha kizamani.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Hussein Mohamed amesema ili kufikia Malengo ya Serikali kupitia sekta ya kilimo katika kuchangia fedha za kigeni Bilioni Tano na ajira Bil. Tatu kwa wananchi hasa vijana ifikapo mwaka 2030 ni lazima kuboresha vyama vya ushirika viwe Bora zaidi.

Akielezea faida za vyama vya ushirika Mrajisi na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika TCDC Dkt. Benson Ndiege amesema, mfumo wa kuuza mazao ya kimkakati kupitia vyama vya ushirika una manufaa makubwa tofauti na kuuza mazao hayo kwa mkulima mmoja mmoja.

Akibainisha hayo Dkt. Benson amesema kwa mfano msimu wa kilimo 2021/2022 na 2022/2023 zaidi ya tani trilioni 1.009. za mazao ya kimkakati ikiwemo tumbaku, kahawa, korosho pamba na mkonge ziliuzwa kupitia vyama vya ushirika ambapo zaidi ya Tsh. trilioni 2.9 zilipatikana, kati ya fedha hizo shilingi bilioni 15.144 zilikusanywa kama ushuru kupitia mamlaka za Serikali za mitaa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa