• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WANAUME BADO WANA ‘UKAKASI ‘ KUPIMA MAAMBUKIZI YA VVU

Posted on: October 7th, 2018

Wakazi wa Mkoa wa Morogoro wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma za Afya ili kutambua Afya zao ikiwemo kupima virusi vya Ukimwi wakiwemo wanaume badala ya wao kusubiri majibu kutoka kwa wenza wao pindi wanapokwenda kupima Afya zao.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Dk Kebwe Stephen Kebwe oktoba 6 mwaka huu wakati akizindua kampeni ya FURAHA YANGU iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kiwanja cha ndege iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro .

Kampeni hiyo imelenga kuhamasisha Jamii kutambua Afya zao ikiwa ni pamoja na kupima virusi vya Ukimwi.

Mkuu wa mkoa alitoa wito huo kufuatia taarifa ya upimaji katika kipindi Januari mwaka 2017 hadi Juni 2018 huku ambacho jumla ya wakazi 341,992 pekee Mkoani humo ndio waliojitokeza kupima virusi vya Ukimwi huku idadi ya wanaume 160,219 na wanawake 181,673.

“Ushahidi wa Kisayansi unathibitisha kuwa mmoja kati ya wanandoa au wapenzi anaweza kuwa na virusi vya Ukimwi na mwingine asiwe navyo, kwa hiyo ndugu zangu wanaume tujitokeze kupima virusi vya Ukimwi tusisubiri majibu ya wake zetu” alisema Kebwe.

Katika kuhakikisha kampeni hiyo inaenea Mkoa mzima wa Morogoro alitoa siku 28 kwa Wakuu wote wa Wilaya za Mkoa huo kuhakikisha wanazindua kampeni hiyo katika Wilaya zao na kutoa taarifa ya utekelezaji wake.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Frank Jacob akimkaribisha Mgeni Rasmi amesema licha ya changamoto zilizopo wanashirikiana na wadau mbalimbali kuhamasisha jamii kujitokeza kupima Afya zao.

Awali akisoma risala ya uzinduzi wa kampeni hiyo mbele ya mgeni rasmi, Mratibu wa huduma za Ukimwi ngazi ya jamii Mkoa wa Morogoro , Dk Emmanuel Mihayo alisema , miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo ni pamoja na muitikio mdogo wa wakazi wa Mkoa huo hasa wanaume kujitokeza kupima Afya zao

Pia uchache wa vituo vya kutolea huduma na matunzo kwa wenye virusi vya Ukimwi (CTC) ambapo kwa sasa Mkoa una jumla ya vituo 66 pekee.

Uzinduzi wa kampeni ya FURAHA YANGU Mkoani Morogoro inafanyika ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya kupima virusi vya UKIMWI iliyozinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Mkoani Dodoma iliyofanyika Juni 19 mwaka huu ikiwa na lengo la kuwafikia wanaume , vijana na akina mama wajawazito ambapo kauli mbiu yake ni PIMA,JITAMBUE, ISHI.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa