• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAZIRI JAFFO AIPONGEZA MANISPAA MORO KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA BARABARA NA HOSPITALI YA WILAYA.

Posted on: October 30th, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Suleiman Jafo amekagua mradi wa barabara yenye urefu wa Km.4.6 iliyopo Manispaa ya Morogoro uliogharimu shilingi Bil. 12.6 ikiwa ni utekelezaji wa uboreshaji miji (ULGSP).

Akikagua Mradi huo Waziri Jaffo alisema kuwa lengo la kukagua mradi wa barabara ya Tubuyu,Nanenane na Maelewano ni kujiridhisha na kuona kama fedha za serikali zimetumika kikamilifu kama ilivyoelekezwa na serikali katika kuwaletea wananchi wake maendeleo kupitia miradi mbalimbali inatokelezwa na serikali ya awamu ya tano.

Waziri Jaffo alisema kuwa baada ya ukaguzi wa mradi wa barabara hizo ameipongeza serikali ya Mkoa wa Morogoro kwa kusimimamia kikamilifu hadi kukamilika kwa mradi huo .

Alitoa wito kwa viongozi na wananchi kwa ujumla kuhakikisha barabara hiyo inatunzwa miundombinu yake ikiwemo kulinda taa za nishati ya jua zilizowekwa barabarani ili kuweza kuifanya kuwa endelevu kwani kumekuwepo na baadhi ya maeneo barababara zinapowekwa miundombinu yake inaharibiwa na baaadhi ya watu wasio waadilifu na hivyo kuisabababishia serikali hasara.

‘’Ni lazima muhakikishe miundombinu ya barabara ,taa,na mitaro iliyojengwa inalindwa isiharibike ‘’alisema Waziri Jaffo.

Awali akisoma taarifa ya Mradi ,Mratibu wa Mradi huo Injinia Godwin Mpinzile alisema kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Halmashauri 18 zinazotekeleza mradi wa uboreshaji miji(ULGSP) kwa kutumia fedha za mkopo toka benki ya dunia.

Injinia Mpinzile alisema kuwa mradi huo ulioanza rasmi mwaka 2017ambao umegharimu kiasi cha shil Bil 12.6 kazi mbalimbali zimeweza kufanyika ikiwemeo kujenga njia za chini ya ardhi,kujenga makalvati,kuweka taa za barabarani .

‘’Pia kazi nyingine iliyofanyika ni pamoja na kuweka vivuko vya kuvusha magari ,kujenga vivuko vya waenda kwa miguu na pia kufanya ukamilishaji wa kazi ikiwemo kuweka alama ,matuta na kuchora mistari.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Steven Kebwe alisema kuwa uongozi wa mkoa umekuwa ukifuatilia kwa ukaribu ujenzi wa mradi huo ili kuhakikisha fedha za serikali hazipotei na zinaendena na thamani halisi ya mradi.

Hata hivyo katika ukaguzi wa mradi huo wa barabara pia Waziri Jafo aliweza pia kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya uliopo katika Kata Kihonda Manispaa ya Morogoro ambapo aliahidi kuzifuatilia kiasi cha sh Mil 400 zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya mradi huo ambapo hadi hivi sasa hazijafika.

‘’Nimekuja kukagua kuona fedha zilizotumwa na serikali kama zimetekeleza vipi huu mradi lakini mmesema hamjaingiziwa hivyo nitafanya ufutailiaji ili fedha hizo niweze kujua zimekwama wapi , ili muweze kuzipata ili kukamilisha rasmi mradi huu’’alisema Waziri Jaffo.

Hata hivyo Mganga Mkuu wa Manispaa Baraka Jonas alisema kuwa lengo la mradi ni kujenga hospitali ya wilaya ya Manispaa itakayosaidia kuweka mfumo mzuri wa rufaa kuanzia zahanati kwenda kituo cha afya na hivyo kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa