• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

AFISA UTUMISHI MANISPAA YA MOROGORO AKUTANA NA MAAFISA AFYA NA WATENDAJI KATA KUFANYA TATHIMINI NA HATUA ZILIZOCHUKULIWA KATIKA KATA DHIDI YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA CORONA COVID-19 .

Posted on: March 26th, 2020

Afisa Utumishi Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Waziri Kombo , amekutana na Watendaji wa Kata zote 29 pamoja na Watendaji wa Mitaa, Maafisa Afya kwa ajili ya kuwasilisha taarifa za jinsi gani walivyochukua hatua katika maeneo yao dhidi ya kujikinga na ugonjwa wa CORONA.


Mkutano huo wa kuwasilisha taarifa na kujadiliana juu ya kujikinga na Ugonjwa wa CORONA umefanyikika leo Machi 26 , 2020 katika Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Morogoro.


Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, amesema lengo la mkutano huo ni kufanya tathimini juu ya hatua zilizochukuliwa na Maafisa Afya wa Kata pamoja na Watendaji dhidi ya kujikinga na Ugonjwa wa CORONA.


Amesema tangia Serikali itangaze taratibu za Kujikinga , kwa upande wa Manispaa hali ya utoaji wa elimu imefanyika kwa kiasi kikubwa sana na mapokeo ni mazuri licha ya kuwepo kwa maeneo machache ambayo yamekuwa chini sana katika mapokeo ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huo.


Aidha, amewataka Maafisa Afya pamoja na Watendaji kushirikiana kikamilifu na kuunda timu ndogo ambayo ikatakuwa inafanya ufuatiliaji kuanzia ngazi zote na maeneeo yote ambayo yana mkusanyiko, kwenye maduka, Hoteli, Nyumba za Ibada pamoja na Stendi za Mabasi ili kuoana hali ya utekelezaji ikoje katika maeneo hayo.


“Kiujumla katika Manispaa yetu ya Morogoro tumejitahidi sana kuelimisha Wananchi , tumekuwa tukitumia njia mbalimbali kama vile matangazo ya vipeperushe, Magari mitaani, Vyombo vya habari, lakini sasa tumekwenda mbali zaidi kwa kugawana majukumu na kuunda timu tatu ambazo zitakuwa zikifanya kazi za ufuatiliaji ikiwemo timu itakayopitia Hotelini, Vitu vya Mabasi na Bodaboda na ile itakayopitia katika Maduka ya Dawa na kawaida ili kuona kama Vitakasa mikono vinazingatia bei elekezi ya Serikali” Amesema Kombo.

Hata hivyo ametoa agizo kwa Maafisa Afya wote na Watendaji katika ngazi za Kata na Mitaa kuhakikisha kila mwezi wanatoa taarifa jinsi gani wameshughulikia suala hilo kikamilifu katika maeneo yao na taarifa hizo ziwasilishwe kwa Afisa Afya wa Manispaa ambaye atatoa fomu maalumu za kujaza.



Naye Kaimu Afisa Afya Mkoa, Prisca Gallet, ameipongeza timu ya Waatalamu pamoja na Maafisa Afya wa Kata na Watendaji kwa jitihada walizochukua za kutoa elimu ya kujikinga na Ugonjwa wa CORONA licha ya kuwepo na changamoto za baadhi ya maeneo kutofuata taratibu hizo.

Amesema mipango iliyopo ni kuhakikisha maeneo yote yaliyopo Manispaa ya Morogoro yanatenga Maji tiririkia na sabuni pamoja na Vitakasa Mikono na kwa wale watakao kaidi watachukuliwa hatua kali za kisheria.

‘Tumeanza kuona matokeo mazuri, hata katika pita pita yangu nimeona tunajitahidi hongereni sana wataalamu , lakini tusibweteke Ugonjwa huu kama mnavyojua ni mgeni katika Nchi yetu , sasa tuanakila sababu za kufuata maelekezo ya Viongozi wetu wa Ngazi za Juu pamoja na Wataalamu wetu wa Afya, tukifanya hivyo na kila mtu akifanya kwa nafasi yake tutakuwa salama katika kujikinga na Ugonjwa huu, kikubwa Maafisa Afya na Watendaji mshirikiane kikamilifu na kila Kata ichukue tahadhari kubwa ya kuwaelimisha Wananchi wake”Amesema Gallet.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa