• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

Mkaguzi wa Ndani


Ukaguzi wa Ndani

Utangulizi

Ukaguzi wa ndani ni kitengo huru, kinachofanya kazi za kushauri, kupendekeza, kuelekeza, kutadharisha, kuainisha viashilia hatarishi, kusaidia kuongeza thamani na kuboresha uendeshaji  ili taasisi itimize malengo yake. Kitengo kinatoa taarifa za ukaguzi kwa mkurugenzi kila robo ya mwaka (Quarterly audit report)

Malengo/ Madhumuni
Kipengele Na. 28 cha Kanuni za Fedha za Umma (2004) na Mwongozo wa Ukaguzi wa Ndani kipengele cha 2.3 wa Mwaka 2013 inamtaka Afisa Masuuli kuanzisha Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani. Madhumuni ya kitengo hiki ni kutoa ushauri kwa Afisa Masuuli juu ya utumiaji mzuri wa rasilimali. Watu, fedha na mali. Majukumu hayo ni kama ifuatavyo:-

Mamlaka ya ukaguzi.

 Ukaguzi wa ndani unafanyika kwa mamlaka aliyopewa Mkaguzi wa Ndani na Sheria ya Fedha za Mamlaka za Serikali za Mitaa Na. 9 ya mwaka 1982 Sehemu ya 45 (1) (iliyorekebishwa mwaka 2000), Memoranda ya Fedha za Serikali za Mitaa ya mwaka 2009 Agizo Namba 13(1)& 14(10), Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2001, Sheria ya Manunuzi ya Umma Na. 7 ya mwaka 2011 “International Professional Practice Framework” (IPPF) na Sheria ya Fedha za Umma Namba 6 ya mwaka 2001 (iliyorekebishwa mwaka 2010).

Huduma za ukaguzi zitolewazo na kitengo cha ukaguzi wandani.

  • Ukaguzi wa usimamizi taratibu (Compliance/ Governance Audit); unatumika kutathmini iwapo Halmashauri inafuata sheria, kanuni, sera na taratibu zilizowekwa.
  • Ukaguzi wa Mazingira (Environmental Audit); unaainisha athati za shughuli za Halmashauri kwa mazingira na iwapo Halmashauri inafuata na kutekeleza sheria na kanuni za mazingira.
  • Ukaguzi wa teknolojia ya habari (Information Technology); kutathmini mfumo wa usimamizi wa habari na kazi data za tarakilishi (Computer database) kuhakikisha usiri wa taarifa za mteja na kuhakikisha taarifa zote za siri kuwa salama. Ukaguzi wa teknolojia ya habari utahakikisha kuwa watumiaji wa mfumo waliohalalishwa ndio wanaweza kutumia taarifa za mfumo na kuhakikisha kuwa taarifa hizo zipo sahihi.
  • Ukaguzi wa Utendaji (Performance Audit); kuona kama Halmashauri inafikia shabaha na malengo yaliyowekwa. Kama haifikii malengo yaliyowekwa Mkaguzi wa ndani atainisha mapungufu ya mfumo na kupendekeza namna ya kurekebisha.
  • Ukaguzi wa Uendeshaji (Operational Audit); kutathmini ufanisi na umadhubuti wa taratibu za Halmashauri. Kuona jinsi gani Halmashauri inagawanya raslimali zake katika uendeshaji. Iwapo raslimali hazitumiki kwa ufanisi Mkaguzi wa Ndani atatoa taarifa pamoja na mapendekezo ni jinsi gani kupunguza upotevu wa rasilimali.
  • Ukaguzi wa miradi (Project Audit). Kutathimini thamani ya fedha za miradi iliyoelekezwa ktk huko na kushauri namna bora ya matumizi, manunuzi kwa kufuata taratibu ya fedha na manunuzi ya umma
  • Ukaguzi wa viashiria (Risk control Audit). Kutathmini na kuifatilia mifumo ya uthibiti wa ndani kama inafanyakazi vizuri na kwa ufanisi (internal control system)

 

Majukumu ya kitengo cha ukaguzi wa ndani ni:

1. Kukagua, kuthibiti na kutoa taarifa kama kuna udhibiti wa kutosha kwenye makusanyo, utunzaji na matumizi ya rasilimali fedha za ofisi.

2. Kukagua na kutoa taarifa kama mifumo ya utendaji iliyoainishwa kwenye sheria , kanuni na maelekezo mbalimbali kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali yanafuatwa ili kuhakikisha kuwa kuna udhibiti wa kutosha kwenye matumizi fedha katika ofisi.

3. Kukagua na kutoa taarifa ya mipangilio na mgawanyo katika akaunti za mapato (revenue) na matumizi ni sahihi.

4. Kukagua na kutoa taarifa juu ya usahihi wa hesabu na taarifa mbalimbali zinazoandaliwa na ofisi.

5. Kukagua na kutoa taarifa juu ya mifumo iliyopo na inayotumika kutunza mali za serikali, pamoja na kufanya uhakiki wa mali hizo.

6. Kupitia na kutoa taarifa juu ya shughuli au mipango ya ofisi ili kuona kama inaendana na malengo na madhumuni ya uanzishwaji wa ofisi.

7. Kupitia na kutoa taarifa juu ya hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Menejimenti katika kujibu hoja za Mkaguzi wa Ndani; na kusaidia Menejimenti juu ya utekelezaji wa mapendekezo ya hoja hizo; na pale inapofaa kusaidia namna ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

8. Kukagua mifumo ya TEKAMA iliyopo katika ofisi na kutoa taarifa kama kuna umadhubuti wa udhibiti uliopo.

9. Kuandaa Mpango kazi na Mpango mkakati wa ukaguzi.

10. Kuandaa na kusimamia mipango ya ukaguzi.

11. Kufanya ukaguzi wa thamani kwenye Miradi ya kimaendeleo na ukaguzi wa thamani mbalimbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa