• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

Huduma za Afya

Manispaa ya Morogoro ni moja kati ya Halmashauri 9 za Mkoa wa Morogoro. Ina Tarafa 1, kata 29 na mitaa 294. Halmashauri hii ina wakazi wapatao 471,409 ambapo wanaume ni 226,817 na 244,592 ni wanawake kwa mujibu wa maoteo yanayotokana na sensa ya mwaka 2022.

 IDADI YA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA

Halmashauri ina jumla ya Vituo 92 vya kutolea huduma katika mgawanyo ufuatao:- Hospitali  5 (2- Serikali, 2- Taasisi za uma 1, binafsi ), Vituo vya Afya 15 (7 vya serikali,3 vya mashirika ya Dini (FBO)  na 5 vya wau binafsi)  kliniki 14, Zahanati 57 ( 25 Serikali,mashirika ya dini - 5, Binafsi 27 na  Martenity home 1.

UTAWALA NA UONGOZI 

Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe ina vitengo vitatu ikiwemo Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na timu ya uendeshaji wa huduma za Afya (CHMT’S). katika kuendesha shughuli zake.

Halmashauri ya Manispaa inayo Bodi ya Afya Pamoja na kamati za vituo zilizo hai  katika kila kituo cha kutolea huduma za Afya  ambazo zinafanya kazi kwa mujibu wa mwongozo. Kamati hizi zinasaidia kutatua changamoto nyingi toka kwenye jamii hali iliyopelekea kupunguza malalamiko ya wateja na kuimarika kwa utoaji wa huduma kwa ujumla.

Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe inafanya usimamizi shirikishi katika vituo vya kutolea huduma ambapo jumla ya vituo 56 kati ya 92 vilitembelewa sawa na 61% kwa mwaka.

 

MFUMO WA GOTHOMIS

Ili kudhibiti upotevu wa mapato katika vituo Halmashauri inaendelea na ufungaji wa mfumo wa GOTHOMIS katika vituo vya kutolea huduma ya afya ambapo hadi sasa vituo vyenye mfumo huo ni 11 kati ya vituo 30 vinavyomilikiwa na serikali hii ni sawa na aslilima 34.5 Aidha Vituo 5 viko katika Hatua ya kufunga mfumo wa Got Homis ifikapo Juni 30, 2024 na Halmashauri imetenga kiasi cha Tsh milioni 37,800,000 katika mwaka wa fedha 2024/25 kukamilisha vituo vilivyobakia .

WATUMISHI 

Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe ina Jumla ya watumishi 659 ambapo watumishi 3 wako kitengo cha Lishe, 19 ni Kitengo cha Ustawi wa Jamii na 628 wapo kitengo cha Huduma za Afya (Tiba na Kinga)

 Aidha kuna upungufu wa kada mahsusi kama wataalamu wa dawa za usingizi (3), wataalamu wa kutengeneza meno bandia (8), wataalamu wa mionzi (8), data clerk (38), wataalamu wa macho.

Kwa mwaka 2022/2023 na 2023/2024 Halmashauri imepokea jumla watumishi wapya 55 ambao wamepangwa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma. 

FEDHA ZA MFUKO WA PAMOJA (BASKET FUND ZILIZOPOKELEWA KWA MWAKA 2023/2024.

NGAZI (COST CENTRE)
BAKAA 2022/2023
FEDHA ZILIZOPOKELEWA
FEDHA ZILIZOTUMIKA
FEDHA ZINAZOENDELEA NA MATUMIZI 
CHMT
0

71,407,425.00

38,980,000.76

32,427,424.24

HOSPITALI
59,818,000. 75

119,022,375

122,819,576.82

56,020,798.18

VITUO VYA AFYA
27,392,829.88

156,626,346

133,032,179.20

50,986,996.68

ZAHANATI
53,650,378.31

135,460,682

127,449,884.75

61,661,175.56

TOTAL
140,861,207.00

482,516,828

  422,281,641.53

 

201,096,394.66

 

 

MIRADI YA MAENDELEO

Halmashauri inaendeleza ujenzi wa miradi mbalimbali kama inavyoonesha kwenye Majedwali 2A na 2B hapo chini.

Jedwali Na. 2A: Mchango wa mapato ya ndani katika uendelezaji wa miundombinu ya Sekta ya Afya 2022 - 2024 yenye thamani ya Tsh.1,395,000,000.00

Na
JINA LA MRADI
ENEO ULIOPO (KATA)
FEDHA ZILIZO
POKELEWA
HATUA ILIOFIKIWA
1.
 KITUO CHA AFYA TUNGI
TUNGI
770,000,000
Hatua ya umaliziaji, OPD,RCH  na walkway vimekamilika
2.
ZAHANATI YA KAUZENI
KAUZENI
140,000,000.00
Jengo la OPD Limekamilika na kuanza kutumika.
3.
 ZAHANATI UWANJA WA TAIFA
UWANJA WA TAIFA
70,000,000.00
Jengo limekamilika na huduma za OPD zimeanza kutolewa
4.
 ZAHANATI YA MLAPAKOLO (OPD NA MAABARA)
MJI MKUU
140,000,000.00
OPD na Maabara  imekamilika na huduma zimeanza kutolewa.
5
ZAHANATI YA MAZIMBU
MAZIMBU
135,000,000.00
Jengo limekamilika huduma za awali zimeanza kutolewa.
6.
KIEGEA “B” (Ujenzi wa nyumba Mtumishi.
KIEGEA
100,000,000.00
Ujenzi hatua ya ukamilishaji nyumba ya mtumishi
7.
Ujenzi wa Maabara zahanati ya Kilakala
KILAKALA
40,000,000.00
Ujenzi iumekamilika

 

 

Jedwali Na. 2B. Fedha kutoka Serikali kuu yenye thamani ya Tsh 2,600,000,000/=

Na
JINA LA MRADI
 KATA
FEDHA PO
KELEWA
HATUA ILIOFIKIWA
3
HOSPITALI YA WILAYA(OPD,MAABARA WODI YA WAZAZI,MIONZI,DAWA,JENGO LA KUFULIA,WODI YA WANAUME,WODI YA WANAWAKE NA WODI YA WATOTO)
KIHONDA

2,000,000,000.00

OPD(100%) maternity,theatre(100%) na maabara(100%), bohari ya dawa(100%), mionzi(100%) na jengo la kufulia(100%).,Ujenzi wa wodi ya watoto,wanaume na wanawake ipo katika katika hatua za upauaji  Hata Hivyohuduma kwa baadhi ya majengo zimeanza kutolewa.
4
KITUO CHA AFYA LUKOBE
LUKOBE

500,000,000.00

OPD, Maabara  kichomea taka kimekamika 100%
Jengo la wazazi asilimia 84%
laundry 99%.huduma za OPD zimeanza kutolewa.
5
 JENGO LA WAZAZI ZAHANATI YA KONGA
MZINGA

100,000,000.00

Hatua ya upakaji rangi

   

UTAYARI WA KUPAMBANA NA MAGONJWA YA MLIPUKO

Kipindupindu ni ugonjwa wa kuharisha na kutapika, unaosababisha mwili kupoteza maji mengi na kuishiwa nguvu hivyo unaweza kupelekea kifo. Ugonjwa huu unasababishwa na bakteria aina ya Vibrio.

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ilianza kufanya maadalizi ya milipuko ya magonjwa (Emergency Preparedness plan), hii ilikuja baada ya mvua nyingi namilipuko ya kipindupindu kutoka maeneo menggi ya nchi.

 

HALI YA MLIPUKO

Tarehe 29.01.2024 halmashauri ya Manispaa Ya Morogoro iliripoti mgonjwa wa ugonjwa wa kipindupindu kutoka kata ya boma mtaa wa OLD DSM ROAD. aMpaka sasa tuna jumla ya wagonjwa/wahisiwa 57 na kifo kimoja vilivyothibitishwa.Aidha ufuatiliaji wa wahisiwa na waliokuwa karibu na wagonjwa wamefuatiliwa.

KAZI ZINAZOFANYIKA KUKABILIANA NA KIPINDUPINDU.

Kutoa elimu kwa jamii kupitia maafisa afya, watendaji na wahudumu wa afya ngazi ya jamii.

Kufanya Vikao vya kuimarisha timu za maafisa afya kutoa elimu ya afya na usimamizi wa usafi wa mazingira.

Kufanya ukaguzi wa afya na mazingira katika kata zenye maeneo Hatarishi zikiwemo Mafisa, Tungi, Mwembesongo Na Chamwino maeneo hatarishi ikiwemo stendi ya mafiga,soko la mawenzi.

Kutembelea, kukagua na kutoa elimu kwenye taasisi mbalimbali zikiwemo shule, makanisa/misikiti.

Ukaguzi wa maeneo yote ya huduma ya chakula (migahawa,mama/baba lishe,hotel).

Kuzuia uuzaji holela wa vyakula,matunda ya kumenya, uuzaji wa ice cream, maji ya kandoro, mahindi ya kuchoma, na kupikwa, juisi ya matunda ya miwa na matunda bila utaratibu maalumu

kutoa elimu kinga na udhibiti kupitia gari la matangazo na radio.

Kugawa vidonge vya chlorine kwa wakazi wa mwembesongo,mafisa  na kichangani pamoja na kata hatarishi.

MAGONJWA 10 YALIYOONGOZA KITENGO CHA WAGONJWA WA NJE (OPD) KWA KIPINDI CHA JANUARI 2023 HADI FEBRUARI 2024

         Watoto chini ya miaka 
Na
          Watu wazima
Na
OPD Diagnoses
Number of Diagnoses
%

OPD Diagnoses
Number of Diagnoses
%
1.
Upper Respiratory Infections
26,463
36.13
1.
Upper Respiratory Infections
34,631
14.17
2.
Urinary Tract Infections
8,535
10.55
2.
Urinary Tract Infection
32,341
13.23
3.
Diarrhea with no Dehydration
7,120
8.80
3.
Ill Defined Symptoms (No Diagnosis)
19,599
8.02
4.
Pneumonia-Severe & Non-severe
5,198
6.42
4.
Hypertension
19,378
7.93
5.
Skin Infection, Non-Funga
4,601
5.69
5.
Peptic Ulcers
11,431
4.68
6.
Ill Defined Symptoms (No Diagnosis
3,912
4.83
6.
Anemia-Mild & Severe
9,944
4.07
7.
Intestinal Worms
3,135
3.87
7.
Diabetes Mellitus
8,285
3.39
8.

Other Non-Infectious GIT Diseases
3,052
3.77
8.
Rheumatoid and Joint Diseases
7,502
3.07
9.
Skin Infection - Fungal
2,517
3.11
9.
Skin Infection-Fungal
5,687
2.33
10.
Anaemia, Severe & Mild/Moderate
2,129
2.63
10.
Intestinal Worms
5,359
2.19

 

HUDUMA ZA MAMA NA MTOTO

Halmashauri ya manispaa ya morogoro ina jumla ya vituo 58 vinavyotoa huduma za afya ya uzazi,24 (40%) kati ya hivi vinatoa huduma ya kujifungua na vituo 5 vinavyotoa huduma jumuishi za kujifungua na dharura za uzazi.Katika kipindi cha mwaka 2023

  • Jumla ya waliohudhuria kliniki ni 62675
  • jumla ya waliohudhuria kliniki kwa mara ya kwanza ni 17308
  • mahudhurio chini ya wiki 12 ni 3734(22%).
  • Waliojifungua15383 kati yao 11785 walijifungua kawaida upasuaji ni 3553(24%)
  • Rufaa kwenda hospitali ya mkoa ni 2036(14.4%)
  • Vifo vya wajawazito 43(20 kutoka manispaa)
  • Vifo vya watoto wachanga 209 kati ya vizazi hai 15303
  • Sababu zilizoongoza kwa vifo vya uzazi ni kifafa cha mimba,kuvuja damu wakati wa ujauzito,kuvuja damu wakati wa kujifungua,kuharibika mamba na maambukizi.

N.B Halmashauri imeweka lengo la kushusha vifo kwa asilimia 50% kwa kipindi cha miezi 6.

HUDUMA ZA CHANJO

Huduma za chanjo zimeendelea kutolewa kwa walengwa ambao ni watoto walio katika umri wa kupata chanjo, wasichana wenye umri wa miaka 14, wanawake walio katika umri wa kujifungua na walengwa wengine kwa makundi yao kulingana na aina ya chanjo wanazostahili.

Kampeni mbalimbali zimetolewa ikiwa ni Pamoja na utoaji jumishi wa chanjo ya Mlango wa kizazi na chanjo za nyongeza kama jedwali linavyojionesha hapa chini.

 IDADI YA WATU WALIOCHANJWA:

NA
AINA YA CHANJO
MALENGO
WALIOCHANJWA
KIWANGO CHA UCHANJAJI

1

CHANJO DHIDI YA KIFUA KIKUU

12,713

23,402

184%

2

POLIO

12,713

20,262

159%

3

POLIO YA SINDANO

11,522

14,578

127%

4

CHANJO DHIDI YA PNEUMONIA

11,522

14,596

127%

5

CHANJO DHIDI YA KUHARA

11,522

14,637

127%

6

SURUA

11,522

15,001

130%

7

DONDAKOO, PEPOPUNDA NA KIFADURO (DTP)

11,522

14,807

129%

8

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI (HPV)

4,855

6,001

124%

9

PEPOPUNDA NA DONDAKOO KWA WAJAWAZITO

12,713

13,293

105%

AFP 5 (133%) FRI 15(120%)

 

DAWA NA VIFAA TIBA

Hali ya upatikanaji wa dawa, Vifaa Tiba na Vitendanishi kwa Halmashauri kwa mwaka 2023 ilikuwa kwa wastani wa asilimia 95.2%  kulinganisha na 94% mwaka 2022  kwa mujibu wa mfumo wa eLMIS.

Dawa na vifaa tiba vilizokosekana katika baadhi ya vituo ni Pamoja na diclofenac inj , liginocaine inj , gauze ,Urine Pregnant test, unalysisi strips,gauze, examination gloves mzani wa watoto na microscope  uhaba huo ni kutokana na kukosekana MSD

Tatizo ambalo lilitatuliwa kwa kuomba dawa na vifaa tiba hivyo toka kwa washitiri wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi nakupandisha upatikanaji wa dawa na vitendanishi kufikia wastani wa asilimia 98%

 UAGIZAJI WA DAWA, VIFAA TIBA NA VITENDANISHI MSD NA KWA MZABUNI TEULE 

Bidhaa zenye thamani ya Tsh. 758,194,978.68 zimepokelewa  katika Halmashauri kwa  kwa kipindi cha julai 2023 mpaka machi 2024 kwa mchanganuo ufuatao, mwaka 2023 Tsh. 765,585,547.00 zilipokelewa kwa ajili ya  Dawa na vitendanishi toka MSD na  Tsh. 117,287,149.88 ni mfumo jazia toka kwa Wazabuni teule, ilikujazia dawa na vitendanishi vilivyokosekana bohari ya dawa (MSD)

 

KIPINDI
THAMANI MAPOKEZI MSD
THAMANI MAPOKEZI WASHITIRI 
JULAI-SEPTEMBA
192,372,256.39
60,899,099.19
OCTOBA-DESEMBA
296,792,176.80
31,165,555.00
JAN-MARCH 2024
151,743,395.61
 25,222,495.69
JUMLA YA FEDHA
640,907,828.80
117,287,149.88

Aidha baadhi ya vifaa tiba vilipokelewa katika vituo vya  kutolea huduma ambavyo ni

X-ray machine, hospital bed, wheelchair, bed sheet, oxygen concentrator, examination bed, delivery beds

Ultrasound machine, Dental chair zenye dental X-ray, mayo table, mahine ya usingizi na vifaa vya upasuaji, infant radiant warmer, blood warmer, patient monitor , delivery set

TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA ZA RUZUKU TSH. 600,000,000 KWA AJILI YA UNUNUZI WA VIFAA TIBA.

Kiasi tajwa hapo juu kilipokelewa  kwa ajili ya ununuzi wa wa Vifaa Tiba. Mgawanyiko wa manunuzi ya vifaa umefanyika katika vituo nane vipya ambavyo ujenzi wake umekamilika na vifaa venye thamani ya Tsh. 200,000,000.00 (kwa mwaka 2022/2023) viliagizwa na fedha zake zililipwa katika akaunti za bohari kuu ya dawa (MSD) za vituo na Tayari Vifaa vyenye thamani ya Tsh. 161,505,949.29 toka Bohari vimepokelewa hii ikiwa ni asilimia 80.8 ya mapokezi

Aidha Halmashauri ilipokea fedha za Vifaa Tiba (2023/2024) toka serikali kuu kiasi cha Tsh 400,000,000.00 ambapo manunuzi ya vifaa yamefanyika na kupokea baadhi ya vifaa Tiba vyenye thamani ya Tsh 196,039,949.72 ambayo ni asilimia 49 ya vifaa vilivyopokelewa na malipo yake yamekamilika.

MAOTEO

Halmashauri ilifanya maoteo ya bidhaa za Afya mnamo Mwezi Agosti 2023 yenye thamani ya Tsh 1,955,857,518.00 kwa vituo 38: ikiwa ni Hospitali tatu (3) , Vituo vya Afya sita (6) na zahanati ishirini na tisa (29)

IDADI YA VITUO
JINA LA KITUO
THAMANI YA MAOTEO
3
HOSPITALS
                       621,061,736.00
6
HEALTH FACILITIES
                       507,550,134.00
29
DISPENSARIES
                       827,245,648.00
TOTAL   FACILITIES   38
TOTAL AMOUNT
                   1,955,857,518.00 

  

HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII 

Huduma za Ustawi wa Jamii hutolewa kwa kufuata Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali.Maeneo yanayosimamiwa na kitengo cha ustawi wa jamii ni pamoja na:

Huduma ya Ustawi wa Jamii wa Familia na Watoto

Huduma ya Marekebisho ya Tabia na Haki za Mtoto Kisheria

Huduma  kwa Wazee na Watu Wenye Ulemavu

 

IDADI YA VITUO VYA KULELEA WATOTO WADOGO MCHANA (DCC) NA MAKAO YA WATOTO YATIMA

AINA YA KITUO

IDADI

YALIYOSAJILIWA

VISIVYOSAJILIWA

VITUO (DCC)
103
42
61
MAKAO
12
11
1
NYUMBA SALAMA
3
0
3

Mkakati

Ni kuendelea kuvifanyia ukaguzi vituo vile ambavyo vina hali nzuri visajiliwe na vile vinaonekana hali yake ni mbaya haviwezi kusajiliwa kulingana na mwongozo uliopo ni kuvifunga.

HALI YA UKATILI WA KIJINSIA NA UKATILI DHIDI YA WATOTO 

Aina ya Ukatili
Watu wazima
Jumla

Watoto

Me

Ke

Me

Ke

Jumla
Ukatili wa Kimwili (vipigo)

02

15

17

11

22

33

Kingono (kubakwa/Kulawitiwa)

0

10

10

25

67

92

Ukatili wa Kihisia

03

14

17

27

93

120

Wahanga walioripoti ndani ya masaa 72 baada ya tukio

0

0

0

7

9

16

Wahanga waliopata matibabu ya Kinga(PEP)

0

0

0

7

9

16

JUMLA KUU

5

39

44

77

200

277

 

UTEKELEZAJI WA KUPUNGUZA MATUKIO YA UKATILI

  • Kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya kujikinga na kutoa taarifa za ukatili wa kijinsia
  • Kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara yatokanayo na ukatili wa kiinsia
  • Kuendelea kutoa elimu kwa wazazi juu malezi bora kwa watoto.
  • Kutumia  Kamati za MTAKUWWA na SMAUJATA katika kushughulikia masuala ya Ukatili.
  • Kamati ya wazee imeundwa kutoa elimu ya maadili.

UUNDWAJI WA MABARAZA YA WAZEE, KAMATI ZA WATU WENYE ULEMAVU NA KAMATI ZA KUZUIA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

 

ENEO

MABARAZA YALIYOUNDWA NGAZI YA HALMASHAURI

IDADI YA KATA ZILIZOPO

KATA ZILIZOUNDA

MITAA ILIYOPO

MITAA ILIYOUNDA

MABARAZA YA WAZEE

1

29

29

294
294
KAMATI ZA WATU WENYE ULEMAVU

1

-

-

294

294

KAMATI ZA MTAKUWWA

1

29

29

294

294

VYETI VYA KUZALIWA KWA WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO

Idadi ya watoto chini ya miaka mitano walioandikishwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa ni watoto 8890 amabapo watoto wa kiume ni 3,720 na watoto wa  kike 5,170. Vyeti vilivyoingizwa kwenye mfumo ni vyeti 5,678 sawa na asilimia 63.8%, hii ni kutokana na changamoto ya ubovu wa simu za kusajilia vyeti vya kuzaliwa.

MIKAKATI KWA AJILI YA USAJILI 

  • Rejista kutoka kwenye vituo vya usajili  zimekusanywa na kuletwa  kwa ajili ya kuingiza  kwenye mfumo na vijana 5 ambao wamefundishwa namna ya kuingiza taarifa za vyeti vya kuzaliwa.
  • Fedha kuendelea kutengwa kwa ajili ya usimamizi shirikishi ngazi ya vituo na kata.

 

HUDUMA ZA LISHE.

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imeendelea kuboresha utekelezaji wa Afua za lishe kwa kuzingatia ubora wa huduma katika vituo vya kutolea huduma na ueimamizi wa mkatbata wa viashiria vya lishe

 HALI YA LISHE


IDADI
ASILIMIA
UDUMAVU
208/6940
3%
UZITO PUNGUFU(NEWBORN)
1467/1944
7.5%
UPUNGUFUWA DAMU(WANAWAKE WAJAWAZITO
343/17143
2%
UZITO ULIOZIDI(WATOTO)
110/7434
1.5%

 

Utekelezwaji wa Afua za lishe umeendelea kuzingatiwa  kwenye usimamizi  wa viashiria vya Mkataba wa lishe Pamoja na  huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya. Halmashauri ina jumla ya watoto  49,575 waliochini ya miaka mitano

Katika kipindi cha mwaka 2023/24 halmashauri imezingatia muongozo wa utengaji wa fedha za lishe na kutenge sh 1334 kwa kila mtoto  na kufanya jumla sh (66,133,050mapato ya ndani)  kwa ajili ya matumizi ya  utekelzaji Afua  za lishe .

Pia shilingi 7,642,000/=zimetengwa kutoka mfuko wa pamoja yaan(busket fund)ambazo zimetengwa na kutumika kwenye vituo vya kutolea huduma pamoja na sh 3,170,000/=kutoka vyanzo vingine yaan(userfee,nhif, na ichf)

Na kufanya jumla ya fedha zote za utekelezaji wa Afua za lishe kuwa sh                                                                                    

76,945,050/=

MCHANGANUO WA UTENGAJI FEDHA ZA LISHE

NO
CHANZO
KIASI CHA FEDHA
1
MAPATO YA NDANI
66,133,050
2
BUSKET FUND
7,642,000
3
USERFEE
1,520,000
4
NHIF
800,000
5
Ichf
850,000

JUMLA
76,945,050/=

Jedwali likionyesha mchanganuo wa utengaji  fedha za lishe kwa mwaka wa fedha 2023/24

Pia halmashauri imefanikiwa kuwajengea uwezo watendaji wa mitaa 147, na wahudumu ngazi ya jamii 167.Lengo ni kuendelea na kuimarisha utekelezaji wa Afua  za lishe ngazi ya mitaa na kaya kwa ujumla.

Sambamba na hilo Halmashauri imefanikiwa kununua length board 29 kutumia mapato ya ndani na pia kuzigawa kwenye vituo vya kutolea huduma

 huduma za lishe zimeendelea kutolewa katika vituo vya kutolea huduma na watoa huduma   63 wamejengewa uwezo juu ya utambuzi wa hali ya lishe kwa watoto chini ya miaka mitano kwa kutumia vibao (lengh board) Pamoja na  maswala mengine ya usimamizi wa viashiria vya lishe ngazi za vituo.

                                                                                                                                                                                                                                                                                    BIMA YA AFYA YA JAMII ILIYOBORESHWA (iCHF)

Kiwango cha uandikishaji wa wateja wa ichf kuanzia mwezi julai 2023 hadi kufikia machi 2024 ni kaya 1313  zenye wanufaika 6801.Aidha vituo viliweza kupokea marejesho  kwa kipindi tajwa ya jumla ya kiasi cha Tsh 19,441,964.92.

CHANGAMOTO KUBWA ZA JUMLA

  • Ukosefu wa Usafiri katika divisheni ya afya unaopelekea kusuasaua kwa ufuatiliaji wa huduma za afya ,ustawi na lishe pamoja na huduma za magari ya wagonjwa.
  • Upungufu wa vituo vya huduma za afya vya serikali vya kimkakati na vinavyoendana na hadhi ya manispaa pamoja na nyumba za watumishi karibu na vituo vya huduma.
  • Uwepo wa matukio mengi yanayohusiana na ukatili wa kijinsia/kingono
  • Vifo  vitokanavyo na uzazi

MIKAKATI  NA UTATUZI

  • Halmashauri ya manispaa kushirikisha wadau ikiwemo Wizara ili kuongeza idadi ya magari kwa ajili  ya  usimamizi wa huduma pamoja na gari la kubeba wagonjwa.
  • Halmashauri ya manispaa kukamilisha ujenzi wa hospitali na vituo vya huduma vya kimkakati.
  • Halmashauri kupitia kitengo cha Ustawi wa Jamii kuendelea na afua za kupunguza matukio ya ukatili.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa