• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA MOROGORO KWA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA SOKO KUU.

Posted on: November 19th, 2019

JUMUIYA ya  Tawala za Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT), imeipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa usimamizi mzuri wa Soko kuu la kisasa.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Novemba 19,2019,  Makamu  Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Ndg. Stephen Mhapa, amesema kasi ya mradi huo imewafurahisha hivyo ameitaka Manispaa kuhakikisha sehemu iliyobakia ya ujenzi inakamilika kwa wakati uliopangwa.

Amesema kuwa, Manispaa ya Morogoro inahitaji kupongezwa sana kwani kabla ya pesa za ruzuku ya Serikali katika Miradi Mikakati tayari Halmashauri ya Manispaa ilishaanza kutafuta pesa kwaajili ya ujenzi , hizi ni juhudi kubwa sana , hatua iliyofikia ya mradi  imeonesha thamani ya pesa iliyotumika.

Amemshauri Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha inaweka vipaumbele vya miradi katika vikao vyao wanavyo kaa ili kuweza kupata mradi mmoja wenye tija kwa Wananchi kuliko kuwa na miradi mingi ambayo haitekelezeki.

Amesema ni vyema kuwa na mradi katika eneo moja na kuchagua kata moja ambayo watajenga mradi mkubwa na utakaowafanya wananchi kufika kwa urahisi ili kupatiwa huduma.

"'Niwapongeze viongozi wa Manispaa kazi inaonekana fedha kidogo kazi kubwa , kwakweli mradi huu tutautangaza kwa Mhe. Rais Dkt . John Magufuli kuonesha jinsi gani mlivyokuwa makini katika matumizi ya fedha, pia niwaombe najua kila Diwani wa Kata angetamani kuwa na mradi ndani ya kata yake lakini ni vyema mkawa na kipaumbele cha kuweka mradi katika kata moja tu ambayo mtaona wananchi wanaweza kufika kwa urahisi kuliko kuwa na miradi mingi isiyotekelezeka," Amesema Mhapa.

Hata hivyo, amemtaka Mkurugenzi wa   Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, kuhakikisha mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Soko kuu la kisasa waweke uongozi mzuri ambao wataamua katika Baraza lao  na  utakaokuwa unauwezo wa kukusanya fedha ili Manispaa  iweze kuendesha miradi mingine.

Amesema siku zote rasilimali pesa inakuwa ndogo kuliko idadi ya watu, hivyo wajifunze katika miradi ya wenzao kuona wanaendesha soko vizuri, isje tena mkawa mmeleta mradi harafu mradi huo ukaleta migogoro na kutokuwa na tija kitu ambacho hakitawasaidia katika kufikia malengo yao ya kukusanya kodi.

Katika hatua nyengine, ameutaka Uongozi wa Halmashauri kuhakikisha wanaweka viwango vya bei rafiki na nafuu kwa Wafanyabiashara ili waweze kufanya biashara katika kupata vipato vyao na Halmashauri kuingiza mapato.

Katika hatua nyengine, ameipongeza Manispaa kwa kupata hati safi kwa kipindi cha miaka 6 mfululizo, hivyo amewaambia kupata hati safi sio jambo jepesi hii inaonesha ni jinsi gani Mkurugenzi, Meya pammoja na waatalamu wake walivyo na ushirikiano katika kuijenga Manispaa hiyo.

Amesema Mhe. Rais Dkt John Magufuli hanaga utani katika fedha anazozitoa katika miradi , hivyo anataka kuona pesa anazozitoa zinatumika kwa miradi iliyokusudiwa na kuleta tija kwa Wananchi na kuona watu wa chini wananufaika na miradi hiyo.

Kwa upande wa Katibu Mkuu wa ALAT,  Elirehema Kaaya, ameitaka Halmashauri kuhakikisha Soko hilo linatumika vizuri ili wale waliokusudiwa kuingia katika Soko  wawe wakwanza kuingia.

"" Nikuombe Mkurugenzi pamoja na Mstahiki Meya nategemea Soko likiisha kuwepo na amani nawaamini sana  , asipatikane mtu yeyote akajipatia kipato kupitia mgongo wa nyuma, nataka kila anayeingia katika soko hili awe mfanyabiashara, mnajua tunavyoumia sasa endeleeni kusimamia jengo liishe salama na muwakee wamamchinga pamoja na Mama lishe maeneo yao ya biashara hawa ni marafiki wa Mhe.  Rais John Pombe Magufuli, Mhe.  hataki kuona watu wanakula kupitia jasho la mtu fanyeni kazi ili tupate pesa za kuendesha miradi mingine kwani mradi huu ni chanzo kikubwa cha pesa za ndani " Amesema Kaaya.

Pia amefurahishwa zaidi kuona Watu wenye uhitaji maalumu wametengewa maeneo yao maalumu, jambo ambalo linalenga kuleta usawa kwa wote na kuendeleza adhima ya Mhe. Rais ya kuwaendeleza Walemavu , Wakina Mama pamoja na Vijana.

Hata hivyo, amempongeza Mkandarasi pamoja na Mhandisi  wa Manispaa kwa kazi nzuri na kuwataka wote kwa pamoja waongeze umakini zaidi ili mradi huo ukamilike kwa wakati na uwanufaishe wananchi.

Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, ameupongeza Uongozi wa ALAT Taifa kwa kutembelea mradi wa Soko kuu la kisasa na kujua  maendeleo yake.Amesema Manispaa imekuwa ikitembelea mradi huo mara kwa mara katika kuona mradi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa.

Aidha amesema atahakikisha mara baada ya kukamilika kwa mradi huo, wafanyabiashara waliosaini mikataba ya awali kabla ya ujenzi kuanza ambao walikuwa katika Soko la zamani wanapewa kipaumbele  kufanya biashara katika soko hilo.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, ameishukuru ALAT na kusema wamefanya jambo zuri kutembelea mradi huo kwani wameanzia Mkoa wa Iringa na sasa wapo Mkoani Morogoro hii inaonesha mabadiliko  makubwa kwa upande wa ALAT.

Amesema, kitendo cha ALAT kutembelea miradi mbali mbali kinasaidia kuzimulika Manispaa na kuonesha jinsi utekelezaji wa miradi inavyotekelezwa.

.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa