• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

BALOZI BATILDA AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MASHARIKI.

Posted on: August 2nd, 2024

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mhe.Balozi Dkt. Batilda Buriani leo Agosti 2, 2024 amezindua Sherehe za Maonesho ya Wakulima – Nane Nane Kanda ya Mashariki inayojumuisha mikoa ya Dar Es Salaam, Pwani, Tanga na Morogoro na kutembelea mabanda mbalimbali ya maenesho katika katika Viwanja vya Kambarage Nyerere Nanenane Mkoani Morogoro.

Akifungua maonesho hayo, Balozi Batilda, amewashauri wakulima,wavuvi na wafugaji kutumia vyema fursa ya maonesho ya wakulima ya Nanenane, kujifunza teknolojia mpya na ya kisasa ambayo itawasaidia kupata tija katika shughuli zao za kilimo, mifugo na uvuvi.

Balozi Dkt. Batilda,amesema asilimia 65 ya Watanzania wamejiajiri kupitia sekta ya kilimo, ambacho inachangia asilimia 28 ya pato la taifa, hivyo kuwataka kuongeza juhudi katika kujifunza teknolojia mbalimbali za kisasa ili sekta hiyo iweze kuchangia pato la taifa kwa asilimia 30 ifikapo mwaka 2030.

“Tunategemea baada ya uzinduzi huu kuona wananchi wengi kutoka kwenye kanda zetu wanakuja kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanyika katika haya maonesho,” Amesema Dk. Buriani.

Aidha, amesema kuwa maonesho hayo yana lengo la kutoa elimu kwa wananchi ili kuongeza mnyororo wa thamani kwa wakulima, wafugaji, wavuvi pamoja na wadau wengine sambamba na kuongeza tija na ufanisi katika shuguli wanazozifanya.

Amesema kuwa mikoa hiyo ya Kanda ya Mashariki inakila sababu ya kufanya vizuri katika sekta ya Kilimo kutokana na uwepo wa ardhi nzuri yenye rutuba, hali ya hewa nzuri pamoja na vyanzo vingi vya maji na kwamba wakulima kufanya hivyo kutaongeza usalama wa chakula pamoja na lishe.

Sambamba na hilo, Dk. Batilda ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wafugaji kufika katika maonesho hayo ili waweze kuona na kujifunza namna bora ya kupanda malisho na kuacha ufugaji wa kuhama hama ambao husababisha migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

“Na huu ufugaji tunaozungumzia hapa sio ule wa kuhama hama, katika maonesho yetu tunawaonyesha wafugaji aina za malisho kama majani ya aina tofauti yenye virutubisho vya aina mbalimbali ili wafugaji wetu waanze kufuga kisasa, tunataka tutokane na migogoro inayotokana na ufugaji holela,”ameeleza.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa