• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA MOROGORO LAWAAGIZA WATAALAM KUWA WANATOA UFAFANUZI WA MAJENGO MAPEMA KABLA YA KUANZA KWA UJENZI WA MIRADI

Posted on: January 31st, 2020

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro limewataka Wataalam wa Manispaa kuhakikisha wanatoa maelekezo ya michoro yao mapema kabla hawajaanza utekelezaji wa miradi ili iwe na tija kwa wananchi.

Hayo yamezungumzwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, wakati wa Mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani ulilofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Morogoro  Januari 30,2020.

Akizungumza na Waandishi wa habari, amesema Baraza hilo halina shida ya kugombana na Timu ya Wataalamu wa Manispaa lakini kikubwa wangependa kupatiwa maelekezo ya kina kutoka kwa Wataalam  juu ya miradi wanayokwenda kuitekeleza ili kushauriana na kuangalia ni jinsi  gani miradi hiyo itakavyokuwa na tija kwa Wananchi.

Aidha, amewataka Wataalam kufanya kazi kwa pamoja na pale wanapokwama walishirikishe Baraza ili waone jinsi ya kuweza kukwamuana mahala ambapo panaonekana kuna tatizo au panahitaji maelekezo ya kina.

"Niwaombe Wataalam , msiwaone Madiwani wanalalamika na kupiga kelele, hii yote ni kutaka kujua miradi inavyoendelea na kuleta tija kwa wananchi maana hata hizo pesa zinazotumika ni kodi za Wananchi hivyo ni lazima wajue na kufuatilia ili wao wawe mabalozi wazuri wa kuizungumzia miradi hiyo katika vikao vyao na kama tutashirikiana kwa pamoja maendeleo ya Manispaa yetu yatazidi kuwa juu" Amesema Mhe. Kihanga.

Amesema maendeleo ya Manispaa ya Morogoro ni ya wote hivyo Manispaa wakifanya vizuri Mkurugenzi, Baraza la Madiwani , Watumishi, Wakuu wa idara na wananchi wote watasifiwa.

Katika hatua nyengine, akijibu swali la Diwani Viti Maalum Kata ya Kiwanja cha Ndege, Mhe. Doroth Mwamsiku lililouliza mikutano ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi ni endelevu au kwa muda mfupi, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema mikutano hiyo ya hadhara ni endelevu hivyo mpango uliopo ni kushuka Mtaa kwa Mtaa kufuatia agizo la Mhe. Rais la kutaka Manispaa na Wilaya kushuka chini kusikiliza wananchi.

Amesema lengo la ziara hiyo ni kusikiliza na kutatua kero za Wananchi ili kurahisisha huduma kwa jamii pamoja na kufahamu kuhusu miradi mbali mbali inayotekelezwa na kero zilizotatuliwa katika utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM chini ya Rais wa awamu ya tano, Mhe Dkt John Pombe Magufuli.

Katika kikao hicho pia kulikuwa na maswali ya papo kwa papo ambapo Diwani  wa kata ya Mji Mpya, Mhe. Wenslaus Kalogeries, amesema katika Soko la Mji mpya kuna mfereji mikubwa imechimbwa lakini haina mwendelezo mzuri pamoja na kuwepo kwa uharibifu wa barabara kipindi kilichonyesha mvua na kutaka kujua changamoto hizo zinatatuliwaje na mamlaka husika.

Kuhusu uendeshaji wa Soko, Sheilla, amesema suala hilo wamekuwa wakilijadili katika vikao lakini wanatarajia kulifikisha katika kwenye kikao cha fedha cha mwezi wa pili na Baraza la Madiwani kwani wao ndio wenye wananchi na kuona jinsi gani watapanga kwa ajili ya maslahi ya maendeleo ya Manispaa na wananchi kwa ujumla bila kuathiri mambo mengine na kufanya Soko hilo kuwa na tija.

Akijibu swali hilo, Meneja wa TARURA Manispaa ya Morogoro, Mhandisi James Mnene, ni kweli wakati wa mvua zinanyesha walikusanya taarifa ya barabara zote zilizoharibika na kuzipeleka TARURA Mkoa kwa ajili ya kuweza kupatiwa fedha za dharura ili kuanza matengenezo ya barabara hizo huku akisema suala la mtaro uliochimbwa kupisha barabara yenye urefu wa Mita 670, mtaro huo ulichimbwa kufuatia kukumbwa na changamoto ya maji (water table) lakini walimkata mkandarasi wa barabara hiyo jumla ya shilingi milioni 28  baada ya kuchelewa kushughulikia suala hilo la mitaro na taarifa  zilipelekwa TARURA  Makao makuu ili kupata fedha hizo lengo likiwa ni kujenga mtaro huo kwa mawe na kuleta ubora.

Katika hatua nyengine, Diwani Kata ya Kihonda, Mhe. Hamisi Kilongo, ameuliza swali la kujengwa kwa majengo mafupi katika Stendi mpya ya Daladala iliyopo Mafiga kufuatia mapendekezo ya kamati ya Fedha, huku Meneja wa TARURA , Eng. James Mnene amesema majengo hayo yalijengwa kwa kuzingatia dizaini na ushauri kutoka kwa Mshauri wa mradi huo na kusema yatakapokamilika hayatakuwa na shida.

Kwa upande wa Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro, Juma Gwisu, amesema Mapaa ya majengo yamezingatia vigezo vya eneo husika hivyo kama yatabadilishwa yatakuwa na athari zake.

Kuhusu Ujenzi Holela, Afisa Ardhi wa Manispaa ya Morogoro, Gisbert Msemwa, amesema katika mwaka wa fedha 2020/2021 wameweka maombi ya kupata Bodaboda 4 kwa ajili ya kusaidia kuzunguka katika maeneo yaliyopo katika Manispaa na kufanya ukaguzi wa ujenzi holela unaofanyika.

Amesema kwa sasa idara hiyo ina wataalam 11 na wanatakiwa wataalam 72 ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu lakini kikubwa ni ushirikianao kwa Madiwani, Wananchi ili kuweza kusaidia katika kukomesha ujenzi holela.

Pia amewataka Viongozi kuanzia ngazi za Mitaa na Kata wanapofanya mikutano na wananchi wawaite na kuiweka agenda ya  Ujenzi holela iwepo katika kila mikutano hiyo ili waweze kuendelea kutoa elimu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa