• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA MOROGORO YAIDHINISHA MATUMIZI YA BILIONI 101,091,069 MWAKA WA FEDHA 2024/2025.

Posted on: March 4th, 2024

BARAZA la Madiwani Manispaa ya Morogoro imeidhinisha kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 101,091,069 katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Kauli hiyo imetolewa Machi 01/2024 na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga katika Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani la kupitisha mpango na Bajeti ya Manispaa ya Mwaka 2024/2025  uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi Kuu ya Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza katika Baraza hilo, Mhe. Kihanga, amesema ,matumizi hayo yamepanda kwa asilimia 17.11 ya matumizi ya mwaka wa fedha 2024/2025ukilinganisha na bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ya shilingi Bilioni 83,792,226,268.00.

Mhe. Kihanga, amesema Bajeti hiyo itasaidia kuwaletea wananchi maendeleo ikiwa pamoja na kuongeza na kuboresha miundo mbinu ya huduma za kijamii kama vile huduma za Sekta ya Elimu,Huduma za Afya, Maendeleo ya jamii, miundombinu ya barabara na Mazingira.


Katika hatua nyingine, Mhe. Kihanga, ametakaWatumishi wazingatie maelekezo ya Waheshimiwa Madiwani katika kusimamia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo na kuzingatia vipaumbele vya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa lengo kuu la kuwaletea maendeleo Wananchi wa Manispaa ya Morogoro Pamoja na kutoa huduma bora.

“Baraza la Madiwani lina wajibu wa kusimamia mapato ya ndani kwa maslahi mapana ya Wananchi na kuhakikisha kuwa mstari wa mbele katika kuhoji matumizi ya mapato hayo ili kuepusha upotevu wa mapato kwa namna yeyote ile, hivyo hivyo Watendaji wa Kata mnatakiwa kusimamia na kutumia kikamilifu fedha za Miradi ya Maendeleo katika Kata zenu na kuwa na mpango kazi wa matumizi wa fedha hizo za miradi ya maendeleo jinsi mnavyosimamia “ Amesema Meya Kihanga.

Akiwasilisha rasimu ya Bajeti ya mwaka 2024/2025,Afisa Mipango wa Manispaa ya Morogoro kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa , Jeremiah Lubereje, amesema katika mwaka wa fedha 2023/2024 mapato ya ndani ya Manispaa yalikuwa ni shilingi Bilioni13,185,280,000.00.

Lubereje,amesema kwa mwaka ujao wa fedha 2024/2025  Manispaa ya Morogoro inategemea kukusanya jumla ya sh Bilioni 15,622,877,022.05 katika mapato ya ndani.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro , Ally Machela, amesema Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 utekelezaji wake utakuwa madhubuti katika ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na fedha zinazotoka Serikali kuu kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo kwa maslahi makubwa ya Wananchi.

Machela, amesema Bilioni 7,832,732,718.6 sawa na 60% zitatumika katika miradi ya Maendeleo, na Bilioni 5,221,821.40 zitaelekezwa kwa matumizi ya kawaida na milioni Tsh 59,388,000.00 zitatumika kwaajili ya mishahara ya watumishi wanaolipwa kupitia mapato ya ndani.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     

Kwa upande wa Mkuu wa wilaya ya Morogoro Mhe. Rebecca Nsemwa, ameupongeza uongozi wa Watumishi wa Manispaa ya Morogoro kwa kuandaa bajeti yenye kusimamia vigezo vyote vya mahitaji ya Wananchi kwa kusimamia IIani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwasisitiza kuisimamia vyema katika utekelezaji ili kumwakilisha vyema Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

DC Nsemwa, ameipongeza Menejimenti ya Manispaa ya Morogoro chini ya Mkurugenzi wa Manispaa, Ally Machela kwa kuandaa vizuri bajeti ambayo itakwenda kusaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto za wananchi.


“Wataalamu wetu mmeitendea haki sana hii bajeti hongereni sana lakini niwapongeze pia Madiwani wetu kwa usimamizi Madhubuti na imara wa miradi ya maendeleo , wananchi wana mategemeo makubwa na sisi, tuwatumikie kwa kusimamia vyema fedha za miradi ili kupata matokeo chanya, tunatarajia kuwa Jiji , hatuwezi kuwa Jiji kama tutashindwa kusimamia miradi ya maendeleo , tushirikiane kwa pamoja kuijenga Manispaa yetu na kutekeleza Ilani ya CCM na yale maagizo yote kutoka Serikali Kuu chini ya mama yetu kipenzi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan” Amesema DC Nsemwa.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Morogoro Mjini ,Fikiri Juma, amesema bajeti ya mwaka 2024/2025 inakwenda kuakisi utatuzi wa changamoto za wananchi.

Aidha ameleza kuwa ipo haja katika upade wa  Sekta ya Miundombinu, Uongozi wa Manispaaa ya Morogoro kuwa na kikao cha pamoja cha kujadili hali ya miundombinu ya barabara kwa Kata zote ambazo zina changamoto ya barabara ili kupata utatuzi wa pamoja.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa