• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

CMT YAJENGEWA UWEZO ZAIDI KUHUSU MRADI WA TACTIC MOROGORO

Posted on: February 2nd, 2024

Maafisa kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi Ndogo Inayoratibu Miradi Inayofadhiliwa na Benki Kuu ya Dunia na Wafadhili Wengine, leo tarehe 02.02.2024 wamefanya kikao na Kamati ya Wataalamu ya Halmashauri ya Manispaa Morogoro (CMT), kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu kipengele kingine cha Mradi wa Kuboresha Miji (TACTIC), kinachojumuisha kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri, mipangomiji, masuala ya majanga, kuzalisha ajira mpya kupitia rasilimali zilizomo ndani ya Manispaa, na udhibiti wa taka ngumu.


“Sisi leo tumekuja kukutana nanyi ili tuwafahamishe zaidi juu ya utekelezaji wa TACTIC ili mwe tayari na mjiandae kwa kuainisha mambo ambayo mnaona yakifanyika basi matokeo ya mradi huu yatakuwa mazuri sana kwa manufaa ya sasa na ya baadae, kwa wananchi, Manispaa na nchi kwa ujumla” alieleza mmoja wa maafisa hao, ambaye kwa cheo yeye ni Afisa Mipangomiji.


“Kipengele cha ujenzi wa miundombinu tayari kimeshaanza kutekelezwa na leo hii tumekuja kwa ajili ya kipengele cha usimamizi wa miji ambapo tunataka ninyi (menejimenti) mtuambie yale ambayo mnafikiri yakifanyika yataimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani, mipangomiji, yatazalisha ajira mpya na kudhibiti taka ngumu” alieleza Afisa mwingine.

Naye mwenyekiti wa Kamati ya Wataalamu ya Manispaa ya Morogoro, ambaye pia ndiye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, ndugu Ally Machela amewashukuru maafisa hao akisema kupitia kikao hicho yeye binafsi amebaini kwamba menejimenti inayo kazi kubwa ya kufanya `katika utekelezaji wa mradi wa TACTIC, pia anaamini kwamba uelewa wa timu yake kuhusu TACTIC sasa umeongezeka zaidi kutokana na maelezo waliyoyawasilisha leo maafisa hao.


“Kupitia kikao hiki ninaona kwamba menejimenti imeongezewa uwezo mkubwa katika ushiriki wake kwenye utekelezaji wa mradi huu hivyo itabidi baada ya kikao hiki tukae na kuainisha mambo yote muhimu ambayo tunataka yafanyike kwenye Manispaa yetu wakati wa utekelezaji wa mradi” alieleza Machela.


Mradi wa TACTIC unalenga kuboresha utoaji huduma kwenye miji, unatekelezwa kwenye miji 45 nchini ikiwemo Manispaa ya Morogoro, na utekelezaji wake upo katika vipengele vinne ambavyo ni kuimarisha usimamizi wa miji, kujenga miundombinu ya kimkakati, usimamizi wa mradi, na kipengele cha nne ni kuhusu wanufaika wa mradi, ambao ni wananchi.



MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa