• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DAWATI LA JINSIA NA WATOTO MANISPAA YA MOROGORO WAUNGANA NA KITUO CHA MSAADA WA KISHERIA MOROGORO KUSHEREKEA MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: November 26th, 2019

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na Dawati la ukaguzi wa Kijinsia Mkoa wa Polisi wa Morogororo pamoja na Kituo cha Msaada wa Sheria Morogoro wameungana kusherekea maadhimisho ya siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia.

Maadhimisho hayo yamefanyika  Novemba 25, 2019 kwenye Viwanja vya Kilakala Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Mkaguzi wa Polisi Mkuu wa  Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Polisi wa Morogoro, Sophia Ngoso, amesema maadhimisho hayo ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia hufanyika kila mwaka kuanzia Novemba 25 hadi Desemaba 12 yakiwa na lengo la kuzungumzia masuala mbali mbali yanayohusu ukatili katika Jamii.

Amesema kwa upande wa Morogoro, wameadhimisha maadhimisho hayo na kongamano ikiwamo kucheza mechi kati ya Waendesha Boda boda na Bajaji  kwani lengo la kuwakutanisha ni kutaka kupata ushirikiano baina ya Wanaume na Wanawake .

Aidha amesema siku zote wamekuwa wakiegemea kuwapatia elimu Wanawake na Watoto  huku wakiwasahau wanaume ambapo kwa upande wake amesema wanaume ndio kichochezi kikubwa cha ukatili wa Kijinsia katika Jamii.

"Tumeamua kuwakutanisha wanaume hapa kwani tunawasahau sana , ukiangalia katika takwimu yetu wanaume, Dereva wa Boda boda na Bajaji wanaongoza katika kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia, hivyo tumeitana ili tupeane mikakati thabiti na kuwafanya kuwa mabalozi wazuri na kuondoa ukatili huu ndani ya familia na nje ya jamii inayomzunguka " Amesema Bi. Ngoso.

Pia ameeleza kuwa anategemea baada ya maadhimisho hayo jamii itakuwa na uelewa mpana juu ya masuala ya ukatili wa kijinsia, na jamii itaishi huru bila ukatili wa kijinsia huku akisema hawatamvumilia mtu yeyote atakayefanya ukatili wa kijinsia.

Naye Nahodha wa Timu ya Bodaboda, John Luhembe, amesema mafunzo yaliyotolewa yatawasaidia sana hususani katika vikundi vidogo vidogo vya wananchi wataweza kuwa mabalozi wema wa kusimamia misingi ya sheria na kanuni pamoja na kuifuata katiba ya Jamhuri ya Muungano na kuacha tabia ya kufanya vitendo vya ukatili wa Kijinsia.

"Siyo boda boda wote wanajihusisha na ukatili wa kijinsia lakini wakati mwengine hali hii inatokana  na ugumu wa maisha, kwani unakuta mwanafunzi anatoka nyumbani mzazi hampi pesa ya kula hivyo akiwa anapakiwa na boda boda anaweza kumlaghai, lakini watakaa na boda boda kwa ajili ya kupeana elimu kwakuwa boda boda wanalalamikiwa sana katika ukatili wa kijinsia kwa Wananafunzi" Amesema Luhembe.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa