• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO AWAFUATA WAJASIRIAMALI WADOGO WALIKO KUWAPA ELIMU YA MANUFAA YA KITAMBULISHO CHA MFANYABIASHARA MDOGO

Posted on: February 1st, 2019

Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo amelazimika kuwafuata wajasiriamali wadogo katika maeneo yao ya biashara ili kuwapatia elimu ya kutosha kuhusu faida ya kuwa na kitambulisho cha mfanyabiashara mdogo baada ya kubaini wengi wao hawajahamasishwa vya kutosha ya kutambua manufaa watakayopata.

Chonjo alisema hayo katika hotuba aliyoitoa kwenye kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Morogoro baada ya kualikwa kutoa salamu za serikali ya wilaya nakutumia fursa hiyo kuwahimiza madiwani kushiriki kutoa elimu kwa wajasiriamali wadogo katika kata zao waweze kununua vitambulisho hivyo kwa faida yao.

Mkuu wa wilaya alisema, baada ya kubaini elimu haijawafikia wajasiriamali wadogo kuchangamkia vitambulisho 5,000 alivyopokea tangu zoezi hilo lianze.Hivyo alisema , kuanzia Januari 26, mwaka huu aliamua kuchukua muda wa mchana kwenda mwenyewe maeneo mbalimbali kutoa elimu kwa wafanyabiashara wadogo na kuuza vitambulisho hivyo kwa wale waliokamilisha ujazaji wa fomu maalumu zilizotolewa.

Chonjo alitaja baadhi ya maeneo hayo ni Stendi ya mabasi Msamvu , eneo la Kingolwira, Mazimbu katika Manispaa ya Morogoro pamoja na halmashauri ya wilaya ya Morogoro eneo la Mkambarani na Mikese .

Alisema kuwa, kasi ilikuwa ni ndogo kwani hadi kufikia Januari 26, mwaka huu ni vitambulisho 581 pekee vilichukuliwa na walengwa kwa gharama ya Sh 20,000 kila kimoja.“ Elimu haijawafikia wajasiriamali wadogo , kwani tangu nimepokea vitambulisho 5,000 hadi Januari 26 mwaka huu vilivyonunuliwa vilikuwa ni 581 idadi hii ilikuwa ni ndogo “ alisema Chonjo.

Hivyo alisema , baada ya kuona mapungufu hayo kuanzia Jumatatu ya Januari 28, Mwaka huu majira ya saa nane mchana aliamua kwenda eneo la kibiashara la Msamvu na hadi kufikia saa 9: 30 alasiri alikuwa tayari ameuza vitambulisho 202.

Mkuu huyo wa wilaya alisema ,vijana wajariliamali zaidi ya 300 walijitokeza kuchukua fomu  kwa ajili ya kuzijaza ili wapate vitambulisho ambapo zoezi hilo lilifanyika pia katika eneo la kibiashara la Kingolwira kwa kutoa elimu na walengwa zaidi ya 180 walichukua fomu na kujaza.

Pamoja na hayo alisema ,alitaja hatua nyingine aliochukua ni kukutana na watendaji wa kata 29 za Manispaa na kila mmoja kupatiwa vitambulisho 100 na kutakiwa kuviuza hadi Februari 3, mwaka huu .

Hivyo alisema ,ili kufanikicha zoezi hilo Madiwani ni watu muhimu kwa vile ni wawakilishi wa wananchi wao katika Kata wanazotoka , hivyo ni vyema wakajitokeza kuhamasisha vijana , akina mama na watu wengine walengwa wa mpango huo ili wanufaika  kutobughudhiwa wanapokuwa kwenye biashara zao.

“ Nawaomba Madiwani mshiriki kutoa elimu kwa wananchi wenu kwa kushirikiana na watendaji ili walengwa wanunue vitambulisho hivyo , kwani fomu ni bure na kitambulisho ni Sh 20,000” alisema Chonjo.

Naye Meya wa Manispaa , Pascal Kihanga baada ya mkuu wa wilaya kutoa ujumbe huo alimhakikishia kuwa , Madiwani watashiriki kikamilifu kuhamasisha na kutoa elimu kwa walengwa ili waweze kuwa na vitambulisho hivyo kwa kuwa suala hilo litawasaidia kuwaondolea usumbufu wakati wa kufanya biashara zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa