• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO AZINDUA KAMPENI YA FURAHA YANGU,PIMA,JITAMBUE ,ISHI

Posted on: November 12th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo amezindua rasmi kampeni ya Furaha yangu leo tarehe 10/11/2018 Manispaa ya morogoro.Kampeni hiyo yenye lengo la kuhamasisha wananchi kupima VVU na iwapo mtu akigundulika kuwa na maambukizi anaanzishiwa dawa mapema.

Akihutubia kwenye  uzinduzi wa kampeni hiyo, Mhe Chonjo amesema kuwa  hii inafuatia agizo la Waziri Mkuu Mhe Kasim Majaliwa aliyoizindua mkoani Dodoma mwezi Juni kwa lengo la kuhamasisha wananchi na hasa wanaume kujitokeza na kupima VVU.
Alisema kuwa dhamira ya serikali ni kuhakikisha ifikapo 2020 watu wote wawe wamepima VVU,watakaogundulika kuwa na maambukizi ya VVU wawe wameanza kutumia ARV na watakao kuwa wanatumia ARV wawe wamefubaza VVU.

"Kampeni ya Furaha yangu,Pima,Jitambue,Ishi inahamasisha mkakati mpya wa serikali wa upimaji wa VVU na kuanza kutumia ARV mapema.Kupitia Furaha yangu ujumbe wa Serikali ni kuwa kutambua hali yako ya VVU huleta amani,na kuanzishiwa dawa ARV kwa wale wenye maambukizi usaidia kuimarisha afya na kupunguza hatari ya kuambukiza VVU wenza wao",alisema Chonjo.

Kampeni hii inawalenga watanzania wote watambue hali zao za maambukizi ya VVU,hususani wanaume na makundi mengine ambayo ni wasichana walio katika umri wa balehe,wanawake vijana wenye umri wa miaka 15-24,akinamama wajawazito na wanaonyonyesha pamoja na watoto wao.

Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Halmashauri za mkoa wa Morogoro iliyoathirika na janga la UKIMWI na kwa mujibu wa taarifa za upimaji robo ya Julai-Septemba kiwango ch amaambukizi katika Manispaa kimepungua kutoka asilimia 3.7 na kufikia asimilia 3.5 kwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 49.

Naye mganga mkuu wa Manispaa  Baraka Jonas alisema takwimu zinaonyesha kiwango cha upimaji wa VVU Manispaa bado kipo chini kwa wanaume ikilinganishwa na wanawake,ambapo katika robo mbili zilizopita jumla ya waliopima VVU walikuwa 142,336 kati yao wanaume ni 57,272 saw na asilimia 40.2 na wanawake walikuwa 85,966 sawa na asilimia 59.8.

Hali hii ni hatari kwa afya ya watu hao na familia,kaya na taifa kwa ujumla kwani inadhoofisha mapambano dhidi ya UKIMWI nchini na kulifanya taifa letu letu kutofikia malengo ya kutokomeza ugonjwa,alisema Mganga mkuu Jonas.

Naye Mwenyekiti wa CCM wilaya Fikiri Juma akizungumza katika uzinduzi huo amesisitiza kampeni hiyo kutoishia ngazi ya Manispaa bali ishushwe ngazi ya kata,mitaa na badae mitaa ili kutoa hamasa kwa watu wengi zaidi kupima afya zao na kujitambua. Aidha amewatahadharisha wananchi kuachana na tabia hatarishi pamoja na unyanyapaa kwa watu wanaoishi na VVU.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa