• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MORO ATAKA UAMINIFU NA WELEDI KWA WARATIBU ELIMU KATA UFUATILIAJI MPANGO WA KUKUZA KKK

Posted on: August 29th, 2018

Maofisa   elimu wa kata za Manispaa ya Morogoro wametakiwa kujituma na kuwa waadilifu katika kazi zao za ukaguzi wa shule za msingi na sekondari ili mapungufu yanayobainika yaweze kufanyiwa kazi kwa wakati kwa ajili ya kuboresha taaluma shuleni na ufaulu wa wanafunzi.

Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo alisema hayo Augost 29, 2018 kwenye viwanja vya jengo la Manipaa ya Morogoro wakati akikabidhi pikipiki 28 kwa Waratibu elimu kata wa Manispaa .

Piki piki hizo zenye gharama zaidi ya cha Sh milioni sita zimetolewa na Serikali kuu chini ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia wahisani wa mtandao wa “ Global Partnership for Education “ (GPE) kwa ajili ya mpango wa kukuza stadi za kusoma , kuandika na kuhesabu (KKK).

“ Mmepewa nyenzo za usafiri kuwawezesha kufika kwenye ukaguzi wa shule za msingi na sekondari kwa wakati , hivyo muwe waadilifu mnapokagua shule , msirubuniwe na taarifa zenu wasilisheni kwa Mkurugenzi ili changamoto zinazobainika zikiwa za wanafunzi kushindwa kujua kusoma , kuandika na kuhesabu zitatuliwe mapema” alisema Chonjo .

“ Kuanzia sasa hatutaki kusikia visingizio, wala kuona mwanafunzi anamaliza shule lakini hajui kusoma , kuandika na kuhesabu “ alisema Chonjo.

Hata hivyo aliwahimiza waratibu hao kuzitunza pikipiki hizo na kushauri baada ya saa za kazi ni vyema zihifadhiwe katika vituo vidogo vya Polisi Kata ili kuepuka kuibiwa kwani baadhi waratibu wanaishi kwenye nyumba za kupanga.

“ Wekeni kwanza usalama wenu ikiwa na kupata mafunzo ya udereva kwenye taasisi za umma kama Veta , kupata leseni , na kutunza chombo za kufanyia kazi ili kikutunze ” alisema Chonjo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , John Mgalula kabla ya kumkaribisha mkuu wa wilaya aliwataka waratibu hao kujituma kwa bidii kufanya kazi kwani kwa sasa hakuna visingizio vya kuchelewa usafiri kwani pamoja na kupewa usafiri huo watapatiwa na mafuta ya uendeshaji.

Naye Ofisa elimu Msingi wa Maniapaa hiyo, Abdul Buheti aliishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kutoa usafiri kwa waratibu elimu kata ambao ni moja ya kuzo kuu katika ufuatiliaji wa maendeleo ya shule za msingi na sekondari za serikali pamoja na shule za watu binafsi katika kuona ubora wa taaluma unakuwa wakiwango cha juu.

Nao baadhi ya waratibu wa elimu kata wa Manispaa hiyo akiwemo Thecla Mbiki kutoka kata ya Kilakala alisema ,kukabidhiwa kwa usafiri huo kutapunguza changamoto za kufuatilia shule za msingi na sekondari na kuwawezesha kufanya kazi kwa bidii zaidi .

Hivi karibuni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako alisema , wizara yake pamoja Tamisemi imewezesha Maofisa elimu kata kwa kuwapatia pikipiki zipatazo 2,864 katika wilaya 156 ili waweze kufanya ufuatiliaji wa ufundishaji na ujifunzaji katika shule zilizopo ndani ya maeneo yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa