• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MOROGORO AWATAKA WAPIMA ARDHI KUJIEPUSHA KUWA VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI

Posted on: April 20th, 2018

Wapima Ardhi wameshauriwa kujiepusha kuwa ni sehemu ya chanzo cha kuzalisha migogoro ya ardhi kwa ajili ya tamaa  ya kujipatia fedha kutoka kwa makundi mbalimbali ya wananchi.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo kupitia hotuba ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa Umoja wa wapima ardhi waliosoma Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) uliofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa Chuo hicho mjini Morogoro.

Mkuu huyo wa wilaya aliwataka wapima ardhi hao kufanya kazi zao kwa uweledi na uadilifu mkubwa badala ya kuwa wao ni chanzo cha kuendeleza migogoro ya ardhi kutokana na tamaa ya kupata fedha.

“ Kada yenu ina umuhimu kubwa na kwa hiyo muachane na tamaa ya fedha , muwe wa kweli wakati wa kupima ardhi na pale mnapobaini eneo hilo tayari linaonekana limeshapimwa lina milikiwa na mtu mwingine , msichukue fedha , waambieni ukweli wahusika ili kuepusha kuendeleza mgogoro “ alisema Chonjo.

Alisema , kada ya wapima ardhi ina umuhimu wake kwa jamii na inahitajika kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuwapimia ardhi na mashamba yao ili kuipa thamani ya ardhi baada ya kupatiwa hati miliki zao.

Mkuu huyo wa wilaya alisema ,wananchi wa Tanzania wanategemea uchumi wao katika kilimo na viwanda , hivyo upimaji wa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa viwanda na wa mashamba ni muhimu kwa ajili ya kupata hati miliki ili kuongeza thamani ya ardhi .

Alisema kuwa, ardhi yote itakapopimwa itaondoa migogoro kwa vile kila mwenye eneo lake atakuwa ana hati miliki ambayo pia itamsaidia kuitumia kupata mikopo ya fedha kutoka kwenye mabenki kwa ajili ya maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi pamoja na sekta ya viwanda.

Hata hivyo alisema , kutokana na upimaji huo na kuwa na hati miliki, wananchi watakuwa na uwezo wa kuzitumia kwa ajili ya kuombea mikopo katika taasisi za fedha ili waweze kuanzisha na kuendeleza shughuli za uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara sambamba na miradi mingine ya kiuchumi.

Awali , risala ya Umoja wa wapima ardhi waliosoma Chuo cha Ardhi Morogoro, iliyosomwa na Katibu wa Arimo Group , Maliki Mang’indo alisema umoja huo umeiomba Serikali kupitia upya sheria ya usajili wa wapima na kampuni.

Alisema , Arimo inashauri sheria mpya iweze kuweka utaratibu unaruhusu kila mpima ardhi asajiliwe kwa ngazi ya elimu yake na wenye mitaji walioanzisha kampuni waweze kusajili kampuni zao katika bodi ya halmashauri ya wapima ili kuleta ushindani sawa katika soko.

Kwa mujibu wa katibu wa umoja huo kuwa , hadi sasa una wanachama 290 baada ya kuanzishwa mwaka 2013 na kusajiliwa mwaka 2016 kwa madhumuni ya kutatua changamoto za upimaji ardhi, kutoa ushauri juu ya upimaji bora wa ardhi , kubuni, kuratibu na kuaznisha miradi mbalimbali kwa manufaa ya wanachama na wananchi kwa ujumla .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa