• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSANDO ATATUA MGOGORO ULIODUMU ZAIDI YA MIAKA 10 KATA YA LUKOBE, ATAKA HEKARI 385 ZIPIMWE ILI WANANCHI WAPE HATI ZA UMILIKI

Posted on: February 17th, 2022

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Albert Msando, ametatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 10 katika Mtaa wa Kambi 5 na Lukobe Juu Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro ili kuhakikisha Wananchi walio na maeneo hayo wanapata hati za umiliki kwa mujibu wa sheria.

DC Msando, ametatua mgogoro huo katika mkutano wa hadhara wa utatuzi wa migogoro ya ardhi uliofanyika Februari 17/2022 kwenye Mitaa ya Kambi Tano na Lukobe Juu .

Akizungumza na Wananchi wa Mitaa hiyo,amesema kuwa kutokana na Mgogoro huo kati ya Wananchi hao na Chuo cha  SUA ,ndio chanzo cha wananchi hao kukosa maendeleo kwa muda mrefu kutokana na kuwa na migogoro ya ardhi iliyodumu kwa muda mrefu.

Aidha, DC Msando, amesema kuwa wananchi wakitaka migogoro hiyo ya ardhi iishe, inaisha na pia wasipotaka migogoro iishe pia haiwezi kuisha.

“Leo tupo hapa kwa ajili ya utatuzi wa migogoro ya ardhi, hatuwezi kuwa na migogoro isiyoisha ambayo inachelewesha maendeleo najua wapo watu wachache ndio wanatuchelewesha katika mpango huu leo tungekuwa tunazungumzia maji, barabara, umeme, vituo vya afya lakini bado tupo katika migogoro haiwezekani, ni vyema kuchukua uamuzi wa kumaliza migogoro hiyo kwa wakati unaotakiwa ili kuweza kuleta maendeleo zaidi katika maeneo yetu, sitokuja tena hapa kwa ajili ya migogoro hii ndio mara yangu ya mwisho kinachofuata ni maamuzi tu" Amesema DC Msando.

"Nitoe rai, haya maeneo tunakwenda kuyapanga upya, sitosikia kuna biashara ya viwanja ikiendelea watakao fanya hivyo tutawachukulia hatua, tunataka kuupanga Mji huu, acheni kazi ifanyike, hakuna atakayebomolewa nyumba, wote mtapata haki zenu na kila mtu tutampa kiwanja hatutomuacha mtu nyuma, na hekari 43 za SUA tutawaachia wenyewe, na wale waliopo katika hekari hizo wanazohitaji SUA wataondoka huko ili tumalize mgogoro kabisa, na wenye hati kutoka Manispaa wasisumbuliwe, na wale waliosimamishwa ujenzi wakati wana hati waendelee, wavamizi wa maeneo ya wazi na barabara tutawachukulia hatua" Ameongeza DC Msando,.

Hata hivyo DC Msando, amesema kuwa mara baada ya Mkutano huo wa wananchi kuamua mpango wa kulipima upya eneo kuna hatua zitachukuliwa ikiwamo kupimwa kwa eneo lote la hekari 385 na kuwekewa bikoni, uhakiki wa watu wenye maeneo yao kwa wakulima na walionunua kila mtu atasimama katika eneo lake, Mipango Miji kuandaa mpango wa matumizi wa eneo hilo kwa kilichopo ardhini ili kupata maeneo ya huduma za kijamii na mpango huo kupelekwa Ofisi ya Kata , Kupimwa kwa Viwanja , mwisho hatua ya ugawaji wa hati za umiliki wa viwanja .

Amesema kuwa kila hatua zitakazofanyika watashirikisha wananchi ili waone kinachoendelea kuanzia hatua za mwanzo hadi za mwisho.

Naye, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Ally Machela, amesema kuwa zoezi la upimaji litaendeshwa katika eneo husika na kila mtu atatakiwa kuwa katika eneo lake wakati wa uhakiki wa maeneo utakapoanza.

“Tutahamishia ofisi hapa, Wataalam wetu watakuwepo hapa ili kukamilisha zoezi la uhakiki hatua kwa hatua mpaka pale zoezi litakapo kamilika, hatuna lengo la kumpora mtu ardhi, sisi lengo letu ni kulinda ardhi ya wananchi kutoka kwenye ardhi ya maneno maneno na kuwa mali halali ambayo inaitwa hati, hii ni ardhi salama kwa manufaa ya wananchi na vizazi vyao vijavyo”Amesema Machela.

Nae mkazi wa mtaa wa Kambi 5, John Aizaki,amempongeza Mkuu wa Wilaya pamoja Uongozi wa Manispaa ya Morogoro katika kutatua mgogoro huo uliodumu muda mrefu huku akisema kuwa baada ya mgogoro huo wanaweza kuendeleza maeneo yao na kujiletea maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa