• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA AFUFUA MATUMAINI YA KUUNGANISHIWA UMEME MKAZI WA KATA KINGOLWIRA MANISPAA MOROGORO BAADA YA KUTESEKA KWA MUDA WA MIAKA 5

Posted on: July 18th, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, amefufua matumani ya Mkazi wa Mtaa wa Shule Kata ya Kingolwira Manispaa ya Morogoro, Bi. Joyce Macha , baada ya kuagiza Shirika la Umeme TANESCO kumunganishia Umeme mkazi huyo.


Hayo yamejiri leo Julai 18,2020, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kutatua kero za wananchi ambapo ameagiza Shirika la Umeme TANESCO Manispaa ya Morogoro kufikia kesho Julai 19,2020 kazi ya kuanza kuunganisha huduma ya umeme kwa mkazi huyo iwe imeshaanza.

Kauli hiyo ameitoa kufuatia mgogoro uliodumu kwa takribani miaka 5 tangia mwaka 2014 kati ya Bi. Joyce Macha na mmiliki wa Shule ya Sekondari Iyula Malaika iliyopo Kata ya Kingolwira ambaye aliendelea kushikiria msimamo wake wa kukataa mwananchi huyo kuwekewa huduma ya umeme kwa kile alichodai kwamba mkazi huyo alivamia katika eneo lake la Shule.

“Haiwezekani mtu akanyimwa huduma ya umeme, kila raia ana haki za kupata huduma bila kuvunja sheria za nchi, umeme uwekwe kwa mwananchi yeyote anaehitaji na mwenye uwezo wa kulipia gharama za kuunganisha hata kama nyumba yake ni ya udongo na kuezekwa kwa nyasi, lakini cha kusikitisha hata kama eneo hilo lingekuwa na kesi kubwa kiasi gani lazima mtu apate huduma kama haki yake ya msingi , kesi hii imeshamalizika , Kamishina ardhi alishatoa hukumu , na eneo hilo limebaki mali ya kimila na hakuna mwenye eneo hivyo mama huyu anatakiwa apate huduma haraka iwezekanvyo ili maisha yake yaende na maisha ya utoaji wa elimu yaende bila kuathiri shughuli za mtu yeyote” Amesema DC Msulwa.


Kwa upande wa Katibu Tawala Wilaya ya Morogoro, Bi. Ruth John, amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa kulivalia njuga swala hilo na hatimaye haki imepatikana.

“Huu ni mgogoro wa muda mrefu, umekuwa ukitusumbua sana , lakini Mkuu wetu wa Wilaya amefika hapa amejionea lakini tunampongeza sana kwa vile ametoa maelekezo mazuri kutokana na hukumu ya Kamishina wa ardhi alivyoitoa, kikubwa familia hizi ziishi vizuri kwani wao bado ni majirani wanatakiwa washirikiane badala ya kuleteana chuki” Amesema DAS Ruth.



Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , Sheilla Lukuba, amemuagiza Afisa ardhi wa Manispaa ya morogoro kuandaa michoro ya hapo ili wale wenye maeneo waweze kuyamiliki kihalali kufuatia maeneo hayo michoro yao kufutwa.



Afisa Ardhi Manispaa ya Morogoro, Gisbert Msemwa, amesema muda wowote wataanza utaratibu wa kuandaa michoro mipya ili maeneno hayo yaweze kupimwa na wenye maeneo waweze kuwa na hati miliki ya ardhi kwani mpaka sasa maeneo hayo ni ya kimila na hakuna mwenye umiliki wa ardhi.

“Hii kesi ya muda mrefu, lakini eleo imepatiwa ufumbuzi, sisi kazi yetu kuanda michoro na kama wenye maeneo watapenda tuendelee nao kupima tutayapima au wanaweza kuwapata watu wengine lakini kubwa zaidi hata eneno hili halikuwa limekusudiwa kuwa Shule bali eneo hili lilikuwa shamba hivyo hakuna taarifa ya kubadili matumizi ya eneo hili tuliyonayo, kwahiyo kuyapima na kuweka michoro kutampa fursa mmiliki wa Shule hii kubadilisha matumizi ya ardhi na kupata kibali rasmi cha ubadilishaji wa matumizi ya ardhi kutoka shamba kuja eneo a huduma ya shule””Amesema Msemwa.

Mkazi wa eneo hilo la Shule, Bi Joyce Macha, amemhukuru Mkuu wa Wilaya , Katibu Tawala, Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro pamoja na Idara ya ardhi kwa kulipambania suala lake na hatimaye kuipata haki yake aliyokuwa akiisubiria kwa muda mrefu.

Amesema sasa ameanza kupata matumaini mapya ya kupata hudma ya umeme kwa muda mraefu na ameahidi kuendelea kushirikiana na majirani zake waliopo katika eneno hilo la shule kwani bado maisha yanaendelea.



Katika hatua nyingine DC Msulwa, , ameuomba Uongozi wa Machinga Manispaa ya Morogoro kufanya kazi kwa uwaledi katika kuwaongoza wamachinga ili waweze kujipanga vizuri na kufanya biashara zao katika maeneo yaliyo salama.

"Nimesikia hapa kuna watu wanajiita wazawa na wandewa, wanawatoza watu pesa kuwakodishia maeneo , tabia hiyo ife mara moja, mtu akiwa na kitambulisho cha Wajasiriamali haruhusiwi kutozwa hela, sasa chukueni hizo hela za wandewa ipo siku mtachukua hela za wandewa wenzenu bila kujijua na mtaangukia mahala pabaya,ridhikeni na vipato vyenu pesa hizi mnazochukua za moto " Ameongeza DC Msulwa.

Pia ameagiza kuanzia mnada ujao wafanyabiashara wote wanaofanya baishara katika maeneo ya Shule ya Msingi Kikundi, Ofisi ya Kata ya Sultan Area pamoja na Kituo cha Polisi Kikundi kuondoka maeneo hayo na wafanye biashara eneo ambalo wamepangiwa na kamati yake ya kuandaa maeneo inayoongozwa na Afisa Tarafa Manispaa ya Morogoro, Wenyeviti wa Mitaa pamoja na Uongozi wa Wamachinga Manispaa ya Morogoro.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa