• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA, AONGOZA MAMIA YA WANANCHI KATIKA KAMPENI YA KUPANDA MICHE YA MITI 15000 PEMBEZONI MWA BWAWA LA MINDU MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: December 9th, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro. Mhe. Bakari Msulwa, ameongoza mamia ya Wananchi wa Manispaa ya Morogoro ikiwamo Taasisi za Serikali na za watu binafsi kushiriki katika Kampeni ya Kupanda Miche ya Miti 150000 pembezoni mwa Bwawa la Mindu Manispaa ya Morogoro .

Zoezi hilo la Kampeni ya upandaji wa Miti pembezoni mwa Bwawa la Mindu Manispaa ya Morogoro limefanyika leo Desemba 09/2020 ikiwa ni Sherehe ya kutimiza miaka 59 ya Uhuru wa Tanzania.

Akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi walioshiriki katika zoezi hilo, DC Msulwa, amesema kuna umuhimu mkubwa na faida nyingi katika utunzaji wa mazingira hususani kupanda miti pembezoni mwa Mito na Mabwawa ambapo faida zake ni pamoja na kupata hewa safi, mvua za kutosha , kivuli, kutumika kama mipaka na kulinda vyanzo vya maji .

Aidha, amesema katika Siku ya leo , Wilaya yake ikiwamo Halmashauri zote mbili zimeandaa kampeni hiyo ya kupanda miti ili kulinda vyanzo vyake vya maji na kuendelea kutoa huduma bora ya Maji kwa Wananchi.

“Nimefurahishwa sana na Kampeni hii, kwani vyanzo vyetu vya maji hali tete watu wanafanya shghuli za kiuchumi katika vyanzo hivyo, wengine wanaziba vyanzo, sasa nimeambiwa Bwawa letu lina miaka 40, unafikiri kama tungeanza uharibifu nyuma tungekuwaje? Niwaombe tuache shughuli katika vyanzo vya maji, Bwawa lina jaa matope , tumeanza naomba wale wenye mashamba tuliyopanda miti watusaidie kusimamia miti hiyo ikue, ugomvi wetu utaanza hapa haiwezekani mazao yako yanakuwa na miti yetu inakufa wakati ipo katika shamba lake, nitoe wito tusiishie hapa kila mtu anawajibu wa kulinda vyanzo vya maji ili tuendelee kupata huduma hii” Amesema DC Msulwa.

“Pamoja na yote, nimefurahishwa sana na ujio wa wageni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka Jimbo la Mwanakwerekwe Zanzibar, hii imeonyesha ni jinsi gani Muungano wetu ulivyo na thamani kubwa ndani ya Taifa hili, tunaomba tuuenzi Muungano wetu kwani unafaida kubwa sana kwa Taifa letu na Maendeleo yetu “ Ameongeza DC Msulwa.

Katika hatua nyingine, DC Msulwa, ametoa wito kwa Wazazi kuhakikisha ifikapo mwakani kila mzazi anapomwandishikisha mtoto na wale wanaoanza kidato cha kwanza kufika shuleni hapo akiwa na mche mmoja wa mti ili kuweka mazingira yenye ukijani.

Kwa upande wa Brigedia Jenerali , Mkuu wa Kikosi cha Jeshi la Mazao Kikosi cha Mzinga, Seif Hamisi, amewaasa washiriki na wananchi kujali mazingira ya sehemu wanazofanyia kazi na kuahidi kuwa miti hiyo iliyopandwa itatunzwa na kulindwa ipasavyo kwa kushirikiana na Uongozi na Wananchi wa eneo la Bwawa la Mindu ambapo ndipo Kambi ya Mzinga ilipo.

"Tunataka Kampeni hii ya upandaji wa miti iwe endelevu ili kuhakikisha Mindu inapokea maji mengi kutoka katika vyanzo vya maji pamoja na kurudisha Mindu katika ukijani wake unaotakiwa kwani Mindu ya Kijani inawezekana" Amesema Brigedia Jenerali Seif.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Michael Waluse, amesema Manispaa ya Morogoro haipo nyuma ambapo wana wadau ambao wameingia nao mkataba wa kila mwaka kuwapatia miche kwa ajili ya kupanda.

Waluse, amesema Ofisi ya Manispaa ipo wazi inashirikiana na wadau wote wa Mazingira ikiwa na lengo la kuweka Mji safi lakini kutunza vyanzo vya maji visiweze kuharibiwa kutokana na shughuli za kiuchumi zinazofanywa na wananchi.

“ Kwa upande wetu Manispaa ya Morogoro, tunakusudia kupanda miti mingi kwani licha ya kuwa ni agizo la Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Mama Samia Suluhu pia ni faida kwa vizazi vijavyo” Amesema Waluse.

Naye, Mkurugenzi wa MORUWASA, Mhandisi Tamim Katakweba, amemshukuru Mkuu wa Wilaya Mhe. Bakari Msulwa pamoja na Bregedia Jenerali ,Seif Hamisi ambaye ni Mkuu wa Kikosi cha Jeshi Mazao Mzinga , kwa kukubali kuhudhuria uzinduzi huo wa Kampeni ya kupanda miti ambapo awamu ya kwanza imepandwa miche ya miti 15000 kati ya miche ya miti ya miche 500000 iliyopangwa kupandwa katika eneo hilo la pembezoni mwa Bwawa la Mindu.

“Leo tumeshuhudia Mkuu wetu wa Wilaya akiongoza Kampeni ya upandaji wa Miti, viongozi na wananchi wamepanda miti ikiwa ni uzinduzi wa Kampeni ya upandaji wa miti katika Vyanzo vya Maji Wilaya ya Morogoro inayosimamia na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Ofisi ya Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro , Ofisi ya Bonde la Mto Ruvu, Ofisi ya Idara ya Misitu pamoja na sisi watu wa MORUWASA, niendelee kuchukua nafasi hii kuwaomba wale wakazi wanaofanya shughuli mbalimbali katika ukanda huu wa pembezoni mwa Bwawa watusaidie kuhakikisha kwamba wanakuwa nje ya Mita 60 lakini wajitahidi kuitunza miti hii ambayo ipo katika mashamba yao” Amesema Eng. Tamim.

Katika hatua nyingine, Eng. Tamim, amesema MORUWASA imetenga kiasi cha fedha chenye thamani ya shilingi Bilioni 185 kwa ajili ya maboresho ya huduma za maji Manispaa ya Morogoro ikiwamo kupanua Bwawa la Mindu pamoja na kununua mtambo mpya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa