• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA AWAGEUKIA WAVAMIZI WA VIWANJA VYA MICHEZO

Posted on: September 26th, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro Mhe.Bakari Msulwa amewataka watu wanaovamia maeneo ya viwanja vya michezo kukomesha tabia hiyo kwani inawanyima fursa vijana kushiriki kwenye michezo.

Kauli hiyo ameitoa leo Septemba 26, 2020 kwenye Viwanja vya Michezo Gymkhana Manispaa ya Morogoro kwenye majadiliano ya kujadili changamoto za Sanaa na Michezo zinazo ikabili Wilaya ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Msulwa, amesema kuwa watu wanaovamia Viwanja vya michezo hawapaswi kuungwa mkono kwani wanawanyima ajira vijana pamoja na maeneo ya kufanyia mazoezi.

Msulwa,amesema kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakivamia maeneo ya michezo na kujenga jambo ambalo linakwenda kinyume na matumizi yaliyopangwa na serikali hivyo vijana kushindwa kuendeleza vipaji vyao.

“Watu wenye tabia hii inabidi waiache kwani inadumaza azma ya serikali kuendeleza michezo mbalimbali hapa Wilayani kwetu na nchini kwa ujumla, hasa ikizingatiwa licha ya michezo kuwa ni burudani lakini pia inatoa fursa ya ajira hasa kwa vijana,” Amesema DC msulwa.

Amesema kuwa serikali imekuwa na mipango mbalimbali ya kuendeleza michezo ikiwa ni pamoja na kuwa na viwanja ambavyo vitawawezesha vijana kushiriki michezo hivyo watu wanaovamia na kujenga ni dhahiri wanakwamisha juhudi hizo.

“Tunaomba wadau wa michezo wahamasishe ujengwaji wa viwanja vya michezo, lakini amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kutoa taarifa za Kata ambazo zina viwanja vya michezo ikiwamo maeneo yaliyovamiwa na watu kuanza makazi ili hatua ziweze kuchukuliwa, lakini niseme kitu kimoja hawa Vijana wanamategemeo makubwa na Serikali yao niwaombe sana Wakurugenzi na Watendaji lazima tujikite katika kuibua vipaji vyao katika nyanja mbalimbali, tukifanya hizi tutatoa ajira na kuwapa uhuru Vijana hawa kuwa na maeoeno ya wazi ya kufanyia mazoezi pamoja na kuendeleza jitihada za serikali kuendeleza michezo hapa nchini” Ameongeza Msulwa.

Katika hatua nyengine, amesema lengo la majadiliano hayo ni

kuwahamasisha vijana kushiriki michezo na sanaa jambo ambalo linatakiwa kupewa uzito wa hali ya juu kwa ajili ya kurudisha hadhi ya Mkoa wa Morogoro katika nyanja ya Michezo.

Mwisho amesema Jumamosoi ijayo ya tarehe 03 Oktoba 2020, watakutana tena na Wanamichezo ili kutoa mrejesho wa yale waliyoyazungumza na kuwekeana mikakati ili kuyafanikisha na kuifanya Morogoro kuwa ya Viwango.

Ikumbukwe kwamba Majadiliano hayo yaliafuatiwa na Mbio za Vijana wa Jogging zilizoanzia katika Viwanja vya Mashujaa majira ya saa 7 asubuhi hadi katika Viwanja vya Ghymkhana ambapo katika mbio za Jogging iliongozwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Bi. Rehema Bwasi , Watumishi wa Manispaa ya Morogoro, Jeshi la akiba na Migambo, Vijana wa Jogging mbalimbali, pamoja na Vijana wa Karate Komfuu ambao walishirikia katika majadiliano hayo.

Kwa upande wa mmoja wa wanamichezo, Sylivester Mokiwa, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya ubunifu wa kutaka kurudisha hadhi ya Mkoa wa Morogoro katika upande wa michezo.

'"Nichukue shukrani za dhati kumpongeza Mkuu wa Wilaya wetu, kwa kweli tulikuwa hatuna mategemeo kama tutakuja kuwa kitu kimoja lakini sauti zetu zimesikika na tunaona muelekeo mzuri wa Morogoro ya Viwango katika Michezo, niwaombe ndugu zangu tunapoitwa katika majadiliano kama haya tujitokeze kwa wingi, tumempata mtetezi wetu bila shaka sasa heshima ya Morogoro inarejea kwa kasi kubwa""Amesema Mokiwa.

KAULI MBIU : "MOROGORO YA VIWANGO KATIKA MICHEZO INAWEZEKANA"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa