• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC NSEMWA AMETEMBELEA ZAHANATI YA SINA, DARAJA LA MAZIMBU NA MITAA YA SINA NA MAMBI MAFISA

Posted on: February 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro mheshimiwa Rebbeca Nsemwa ametoa pole kwa wananchi wa kata ya Mafisa kwa kupatwa na mafuriko na ugonjwa wa kipindupindu.

Mheshimiwa Nsemwa ameyasema hayo tarehe 14.02.2024 alipotembelea Zahanati ya Sina kujionea maendeleo ya ujenzi wake.

“Ni lazima tujikite kwanza katika suala la usafi. Tujitahidi kuhakikisha maji yote tunayotumia yawe yamechemshwa vizuri kwa sababu ugonjwa wa kipindupindu inasemekana unasababishwa na kula kinyesi, na baadhi ya vyanzo vyetu vya maji vimeathirika sana na mvua nyingi zilizokuwa zikinyesha kwenye maeneo mbalimbali hivi karibuni ” alieza Nsemwa.

Pia, mheshimiwa Nsemwa baada ya kukagua Zahanati hiyo na kujionea vifaa vya kisasa vya kupimia damu (Full Blood Picture), na uwezo wa ini kufanya kazi vikiwepo na havifanyi kazi kutokana na kutokuwepo kwa reagents na friji ya kutunzia reagents, amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha anapeleka friji ya kutunzia reagents, na kuhakikisha taratibu zinafanyika ili reagents husika zipatikane kwa ajili ya Zahanati hiyo.

Maeneo mengine aliyotembelea ni pamoja na daraja la Mazimbu ambapo ameagiza mto unaopitisha maji kwenye daraja hilo usafishwe ili kuzuia maji yake kuendelea kuchepuka na kuingia kwenye makazi ya wananchi, na mtaa wa Mambi na Sina ambako kuna dampo la maji taka na kuwataka TARURA wajenge barabara kwenyemaeneo hayo ili kupunguza adha ya ukosefu wa barabara zinazopitika wakati wote kwenye maeneo hayo.

Naye Diwani wa kata ya Mafisa mheshimiwa Joel Kisome, akamwomba Mkuu wa Wilaya asaidie kata yake iweze kujengewa mitaro ya kupitisha maji pindi mvua zinaponyesha kwani kukosekana kwa mitaro kunawaweka wananchi wake katika hatari kubwa ya kupata magonjwa ya mlipuko hasa nyakati za mvua.

“Sehemu tuliyopo sio rafiki. Hatuna mitaro, mvua zikinyesha maji kutoka pande zote yanakuja huku. Mto Morogoro nao umehamia huku. Tungepata mitaro tungeshukuru sana” alieleza mheshimiwa Kisome.  

Baada ya ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya, mheshimiwa Rebecca Nsemwa alifanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya Mafisa ambapo alisikiliza kero zao na kuzijibu kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Manispaa na watalamu kutoka TARURA na MORUWASA.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa