• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DIWANI MSUYA ATOA UJUMBE KWA WANAFUNZI WANAOSOMEA TAALUMA YA MAENDELEO YA JAMII.

Posted on: May 21st, 2023

DIWANI wa Kata ya Mbuyuni, Mhe. Samwel Msuya ,amewataka wanafunzi wanaosomea Maendeleo ya Jamii wajifunze taaluma hiyo katika mtazamo mpana ambao utawasaidia kuwajenga katika nyanja yakutatua changamoto zinazozikabili jamii husika.

Kauli hiyo ameitoa Mei 19/2023 , wakati wa Ofisi yake ya Kata kwa kwa kushirikiana na Kikundi cha Maendeleo ya Jamii cha Community Development Association (C.D.A) kinachoundwa na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA wakitoa msaada wa vyakula kwenye Makao ya kulelea wazee Funga Funga ikiwa ni mpango wao wa kuona namna ya kusaidia jamii inayokabiliwa na changamoto mbalimbali.

"Leo tupo hapa fungafunga nadhani kuna kitu mmejifunza, hivyo kama wana taaluma ni wajibu kuona umuhimu wa kujali jamii hasa zile zinazoishi katika mazingira magumu. nimpongeze sana Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuona haja kubwa ya kuweka makao ya kulelea wazee na wazee wanapata malezi mazuri " Amesema Mhe. Msuya.

 Msuya, amesema wanafunzi hao wanajifunza masuala ya kuutumikia umma lakini lazima wajikite kuangalia uhalisia halisi katika jamii zinazo wazunguka kwani kufanya hivyo wanaweza kuzifikia malengo yakuzisaidia jamii zilizo katika maisha duni.

Kwa upande wa Mtendaji Kata ya Mbuyuni, Sada Mpina, ameishukuru Kikundi cha C.D.A kwa kujitoa kwao na kushirikiana na Ofisi yake huku akiwataka wasiishie hapo kwani bado jamii inahitaji msaada kupitia kwao aidha kwa vyakula au kutoa elimu juu ya maendeleo ya Jamii katika ustawi wa wananchi.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Mbuyuni,Alicia Mbaga, amewashukuru wanafunzi hao na kuwataka kujifunza kwa vitendo zaidi katika kusaidia jamii kama walivyofanya kupitia michango yao ya kujitolea vyakula.

Mwenyekiti wa C.D.A, Jamaica Magali, amesema Kikundi chao kitaendelea kutoa misaada kadri watakavyoweza kujaaliwa na kuhakikisha taaluma wanayoipata Chuoni wanaitumia kwa manufaa ya jamii inayowazunguka.

Mwakilishi wa Wazee Funga Funga, Mzee Hossea Daniel, ameushukuru Uongozi wa Kata pamoja na wanafunzi wa kikundi cha C.D.A huku akiwataka kuwa makini kwa kuzingatia masomo ili waweze kupata manufaa kwenye maisha yao .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa