• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DIWANI WA KATA YA CHAMWINO AKABIDHI MATOFALI 500 SHULE YA MSINGI KAMBARAGE KUASAIDIA UJENZI WA MADARASA

Posted on: November 18th, 2022

KATIKA kuhakikisha wanafunzi wanasoma kwenye mazingira rafiki na salama Kata ya Chamwino, Diwani wa Kata hiyo Mhe. Abdallah Meya, amekabidhi matofali 500 yenye gharama ya shilingi laki 600,000/= katka katika Shule ya Msingi Kambarage kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Matofali hayo ameyatoa leo Novemba 17/2022 akiambatana na Uongozi wa CCM Kata ya Chamwino, Uongozi wa Kata wa Serikali , viongozi wa matawi , pamoja na wadau wa maendeleo.

Akizungumza wakati wa kugawa matofali hayo, Mhe. Meya,amesema ameamua kuunga mkono Juhudi za Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan za ujenzi wa madarasa ili wanafunzi wasome katika mazingira rafiki.

Meya ,amesema , wazazi wamekuwa na mwitikio mkubwa wa kuwapeleka watoto wao shule hivyo kufanya idadi ya wanafunzi kuwa kubwa ukilinganisha na vyumba vya madarasa vilivyopo hivyo kupitia matofali hayo 500 aliyoyatoa yatasaidia kupunguza changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa.

"Nafarijika kuona wanafunzi wakisoma katika mazingira rafiki, niwaombe sana wananchi kuendelea na moyo wa kujitolea katika kufanya kazi za kimaendeleo hali itakayosaidia watoto kusoma katika mazingira mazuri na hatimae kutimiza ndoto zao" Amesema Meya.

Aidha, amewataka wananchi kuwa wazalendo kwa kusaidia shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kuchimba msingi, kusomba mawe ili kuweza kupunguza gharama zitakazosaidia katika kutekeleza shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu wa CCM Kata ya Chamwino, Mwajuma Kibwana, amemshukuru Mhe. Diwani kwa kujitoa kwake huku akiwataka wadau wengine pamoja na wananchi kuchangia maendeleo ya elimu na sio kuwaaachia viongozi na Serikali pekee.

Naye mwakilishi wa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage, Thecla Kamataita, amempongeza Mhe. Diwani kwa msaada wa matofali 500 ambapo amesema ujenzi wa Madarasa hayo yatakuwa suluhisho la kudumu na itasaidia wanafunzi kusoma vizuri.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa