• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DKT. GWAJIMA AWATAKA RMO NA DMO KUANZISHA HUDUMA ZA VIPAUMBELE KATIKA VITUO VYA AFYA AMBAVYO HAVIJAKAMILIKA

Posted on: April 27th, 2021

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima amewataka waganga wakuu wa Mikoa (RMO) na wa Wilaya (DMO) zote hapa nchini kuanzisha huduma za kipaumbele katika vituo vya Afya ambavyo havijakamilisha ujenzi wa jengo la mama na mtoto zikiwemo huduma za chanjo, kupima akinamama wajawazito na matatizo madogo ya dharura wakati Serikali inajipanga kukamilisha majengo hayo.

Dkt. Gwajima ametoa agizo hilo leo April, 27 wakati wa uzinduziwa wiki ya chanjo Kitaifa iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Chamwino “B” katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

‘’Tutaanza kulia na jina la Gwajima kwasababu uwezekano wa kufanya vitu upo halafu hatufanyi, matatizo yetu ni mengi na rasilimali ni chache lakini tukijiongeza tutaweza kupunguza tatizo mojawapo hasa matatizo yanayogusa huduma za mama na mtoto’’ amesema Dkt. Gwajima.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amesema lengo la siku ya chanjo duniani, ni kuelimisha na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa Afya katika kujikinga na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo na kuepuka vifo vinavyoweza kuzuilika kwa njia ya chanjo.

Aidha, Loata Sanare amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Mkoani humo kuhakikisha wanasimamia zoezi la kuhamasisha wazazi kuwapeleka watoto katika vituo vya afya kwa ajili ya kupata chanjo na Elimu juu ya umuhimu wa chanjo.

Sambamba na hayo, Loata Sanare amebainisha kuwa kuongezeka kwa vituo vya kutolea huduma za Afya Mkoani humo, kumewanufaisha wananchi na kuhakikisha huduma zinawafikia popote walipo ikiwa ni sera ya Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. SamiaSuluhu Hassan.

Kwa upande wake Mwakilishi kutokaShirika la Afya Duniani – WHO Dkt. William Mwengee ameipongeza Tanzania kwa kutokomeza baadhi ya magonjwa kutokana na ufanisi wa chanjo ambayo imekuwa ikifanyika ikiwemo chanjo ya ugonjwa wa Fulio na Surua.

Dkt. Mwengee amesema WHO itaendelea kutoa ushirikiano na Tanzania katika kutoa huduma za Afya ili kufikia malengo endelevu ya kutoa huduma kwa wananchi ikiwepo huduma ya chanjo mbalimbali.

Mwakilishi kutoka Ofisiya Rais TAMISEMI Bi. Joseline Ishengoma, ametoa wito kwa wazazi kuwapeleka watoto katika vituo vya Afya kwa lengo la kupata chanjo na huduma nyingine kwa kuwa kwa sasa katika vituo vya kutolea huduma za Afya kuna vifaa na watumishi wakutosha wa kutoa huduma hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa