• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

HALMSHAURI YA MANISPAA YA MPANDA YAIPONGEZA MANISPAA YA MOROGORO KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: December 18th, 2019

HALMSHAURI ya Manispaa ya Mpanda yaipongeza  Manispaa ya Morogoro kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo ikiwamo mradi wa Soko Kuu la Kisasa, pamoja na  Stendi ya mabasi Msamvu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Desemba 18, 2019,  Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda , ambaye ndiye kiongozi wa msafara, Mhe. William P. Mbogo, amesema kasi ya miradi ya maendeleo ya Manispaa ya Morogoro  imewafurahisha hivyo amelitaka Baraza la Madiwani Manispaa ya Mpanda kuhakikisha wanapo rudi nyumbani  waanze kufanya kazi kwa kile walichojifunza.

Amesema kuwa, Manispaa ya Morogoro inahitaji kupongezwa sana kwani wamepiga hatua kubwa huku wakionesha thamani  ya fedha katika miradi  na wamekuwa mfano wa kuigwa hususani katika miradi hiyo na kuifanya manispaa hiyo kuongeza miradi mingine katika pato lao la ndani.

Pia amefurahishwa zaidi jinsi Manispaa ya Morogoro ilivyoweka vipaumbele hususani katika kuwahamisha wafanyabiashara kwa maridhiano na kuwapa kipaumbele mara baada ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa soko kuu.

Aidha, amefurahishwa zaidi kuona Watu wenye uhitaji maalumu wametengewa maeneo yao maalumu, jambo ambalo linalenga kuleta usawa kwa wote na kuendeleza adhima ya Mhe. Rais  Dkt John Magufuli ya kuwaendeleza Walemavu , wakina Mama pamoja na Vijana.

"'Niwapongeze viongozi wa Manispaa kazi inaonekana  , kwakweli katika miradi yenu kuna vitu vingi tumejifunza, sisi kwetu tuna miradi mingi ikiwamo wa Stendi ya mabasi aidha tumejifunza jinsi ya kuendesha mradi wa soko na tutakwenda kukaa na wafanyabiashara kuona jinsi gani tutawasogeza kwa maridhiano ili kujenga soko manake kujenga soko nje ya mji haitakuwa biashara nzuri kwetu bora tujenge katikati ya mji ili tuweze kupata mapato, pia katika mradi wa stendi ya Msamvu tumeona wakaguzi wa Kimataifa wanavyofanya kazi yao kwakweli inaonesha ni jinsi gani Manispaa yenu mlivyo karibu na Serikali pamoja na Chama Tawala cha  CCM" Amesema Mhe. Mbogo.

"Ukiangalia Manispaa yetu ya Mpanda , tunataka kuibua miradi mikubwa lakini tunahitaji kukusanya kodi katika miradi hiyo, hivyo lengo letu kubwa kuja hapa ni kuona namna gani tutapata uzoefu  na kujua wenzetu wanatumia aina gani ya ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa miradi ili nasisi tuweze kufanya kama wanavyofanya wao " Aliongeza kusema Mhe. Mbogo.

Hata hivyo, amesema watamshauri Mkurugenzi pamoja na Baraza la Madiwani la Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda , kuhakikisha mara baada ya kukamilika kwa miradi ya maendeleo waweke uongozi mzuri ambao wataamua katika Baraza lao  na  utakaokuwa unauwezo wa kukusanya fedha ili Manispaa  iweze kuendesha miradi mingine.

Amesema siku zote katika kuhitaji maendeleo lazima ujifunze kwa mwenzako maana rasilimali pesa inakuwa ndogo kuliko idadi ya watu, hivyo wamejifunza jinsi ya kuendesha miradi  vizuri, isije tena ikawa wameibua miradi,harafu miradi hiyo ikaleta migogoro na kutokuwa na tija kitu ambacho hakitawasaidia katika kufikia malengo yao ya kukusanya kodi.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonio, ameipongeza Manispaa ya Mpanda kwa kujitolea kuja kujifunza namna ya kuendesha miradi na jinsi ya ukusanyaji wa mapato.

Aidha amesema kujifunza sio dhambi hivyo  wataendeleza ushirikiano huo pindi pale watakavyohitajika kufanya hivyo kwa Ustawi wa Maendeleo ya Tanzania na Wananchi kwa Ujumla.

Amesema kuwa kujifunza ni njia ya kupata maendeleo zaidi ,hivyo kwa kupitia mafunzo hayo Manispaa ya Mpanda watanufaika sana na wataimarisha mifumo ya kodi na kuiletea Manispaa yao Mendeleo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema kuwa ,  Manispaa ya Morogoro ipo chini kimapato ukilinganisha na Manispaa nyengine za Mjini kama kwenye Majiji makubwa  , lakini wanajitahidi sana kufuatilia vyanzo vya mapato  , amewahahakishia ushirikiano na kunufaika na lengo la  ziara yao yenye kulenga kuwajengea uzoefu  na kujua mbinu wanazotumia za ukusanyaji wa mapato.

" Kweli tumewapokea ndugu zetu wa Manispaa ya Mpanda kutoka mkoani Katavi kwa ajili ya kuja kujifunza hapa kwetu,  matumaini yangu ni kwamba  tangia walivyokuja ni tofauti na sasa baada ya kuondoka, lakini tunachowaambia mafanikio yetu ni kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha za miradi , hivyo tunakusanya fedha nyingi lakini hizi fedha tunazipeleka kwenye miradi ya wananchi na miradi hiyo inaonekana, lakini Manispaa ya Morogoro tumekuwa na miradi mikubwa matarajio yetu baada ya miradi hii kukamilika tutakusanya pesa na tutazielekeza katika kuibua miradi mengine ya maendeleo"Amesema Sheilla.

Aidha, amesema ili kufikia lengo katika ukusanyaji wa kodi ni lazima uheshimu misingi ya matumizi mazuri ya pesa pamoja na kuwekeza katika miradi ya wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa