• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JAFO AAGIZA UKAMILISHAJI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI MJI MPYA MANISPAA YA MOROGORO IFIKAPO AGOSTI 30, MWAKA HUU

Posted on: July 22nd, 2019

Waziri  wa Nchi , Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo ameuagiza Uongozi wa Manispaa ya Morogoro na mkandarasi wa ujenzi wa majengo ya Shule ya Sekondari ya Mji Mpya kukamilisha ujenzi ifikapo Agosti 30, mwaka huu ili wanafunzi waendelee kusoma kwenye madarasa yao.

Waziri Jafo alitoa agizo hilo mjini Morogoro alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa majengo mapya ya shule ya Sekondari Mji Mpya baada ya eneo yalipokuwa awali kupitiwa na njia ya Reli ya Mwendokasi (SGR) .

Alisema , Manispaa hiyo ilichelewa kuanza ujenzi huo tofauti na ilivyo kwa wenzao wa shule ya Sekondari Msoga iliyopo mkoani Pwani ambayo ilipitiwa na njia ya Reli ya SGR.

Waziri Jafo alisema , wenzao mara baada ya kulipwa fidia walianza ujenzi mara moja na tayari umekamilika na wanafunzi wapo shule tangu zilipofunguliwa mapema Julai mwaka huu tofauti na kwa Manispaa ya Morogoro.

 “Lakini kwa leo nimeona hapa kazi inaendelea vizuri na ninaagiza kuwa ifikapo Agosti 30, mwaka huu majengo haya yawe yamekamilika na wanafunzi wanakuwa madarasani na mimi nitarudi tena kuona utekelezaji wake “ alisema Jafo.

Waziri Jafo pia alimwagiza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuhakikisha anaweka mazingira mazuri ya shule hiyo kwa vile ina eneo kubwa tofauti na hapo awali .

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, John Mgalula alisema , walipokea cha fedha Sh bilioni 1.4 za ujenzi mpya wa shule hiyo zikiwa ni fidia baada ya shule iliyokuwa hapo awali kupitiwa na njia ya Reli ya Mwendokasi (SGR) kuvunjwa.

Mgalula alisema , ujenzi wa shule hiyo kwa sasa unaendelea kwa kasi na kwamba watakamilisha kulingana na maagizo yaliyotolewa na Waziri ili wanafunzi waweze kuendelea na masomo hayo .

Kwa upande wake Msimamizi wa Ujenzi wa Shule hiyo kutoka Vikosi vya Ujenzi mkoani Dodoma , Mhandisi Simeon Machibya alimhakikishia Waziri kuwa licha ya kuchelewa kuanza ujenzi huo wataukamilisha ufikapo Agosti 30 ,mwaka huu na kukabidhi kazi.

“ Vifaa vyote vya ujenzi vipo eneo la ujenzi na pia tuna nguvu kazi ya kutosha tumewapata wafanyakazi wa muda wa kusaidia mafundi na wengi ni wanawake ili tutimize lengo lililokusudiwa” alisema Mhandisi Machibya.

Pamoja na hayo alisema ,ujenzi huo ilianza wiki mbili zilizopita kwa kujenga vyumba vya madarasa 20 ,jengo la utawala ,maabara tatu ,nyumba nne za walimu na vyoo matundu 36 kwa matumizi ya wanafunzi na walimu na majengo mengineyo yaliyoanishwa kwenye michoro..

Katika hatua nyingine ,Waziri Jaffo alikagua maenendeleo ya ujenzi wa soko kuu la Morogoro na kuridhishwa na kasi yake na hivyo kuwapongeza wakandarasi wa ujenzi huo pamoja na uongozi wa Manispaa ya Morogoro na kuwataka wakandarasi wengine wazalendo kuiga mfano huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa