• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JAFO AIPA MANISPAA YA MORO FEDHA MILIONI 400 ZA KUENDELEZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA

Posted on: February 26th, 2019

Waziri  wa Nchi , Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Suleiman Jafo ameuagiza uongozi wa serikali ya mkoa wa Morogoro kuhamisha fedha kiasi c ha Sh milioni 400 kati ya sh bilioni 1.9 zilizoingizwa katika halmashauri ya wilaya ya Morogoro na kuzipeleka Manispaa ya Morogoro kwa ajili kuanza kuendelea kujenga hospitali ya wilaya ya Manispaa.

Waziri Jafo alitoa agizo hilo hivi karibuni mjini Morogoro kwa mkuu wa mkoa Dk Kebwe Stephen Kebwe , Katibu Tawala wa mkoa pamoja na Mganga mkuu wa mkoa wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa soko kuu la Morogoro.

Jafo alisema , kiasi cha Sh milioni 400 zilizoingizwa katika halmashauri ya wilaya ya Morogoro badala ya Manispaa ya Morogoro na kuifanya iwe na jumla ya Sh bilioni 1.9 baada ya awali kuingiziwa sh bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya.

Hata hivyo alisema , halmashauri hiyo bado haijafanya vizuri katika kusimamia mradi na bado ujenzi wa hospitali yake upo ngazi ya matayarisho na haijaonesha kuzitumia fedha hizo vizuri kwa lengo lililokusudiwa.

“ Nina aagiza Sh milioni 400 walioingiziwa zihamishwe na zielekezwe Manispaa ya Morogoro ambayo haijapewa fedha “ alisema Jafo.

Waziri Jafo alisema, ilifahamika kuwa fedha hizo zimepelekwa Manispaa ya Morogoro , lakini baadaye ikabainika ya kwamba hazikungizwa huko na badala kale zikapelekwa halmashauri ya wilaya ya Morogoro ambako tayari ilipatiwa Sh bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya.

Kutokana na kuwa na kiasi kikubwa cha fedha na ujenzi wake bado inasuasua alimwagiza mkuu wa mkoa Dk Kebwe , Katibu Tawala wa Mkoa na Mganga mkuu wa mkoa kuzihamisha fedha hizo na kuzipeleka Manispaa kwa ajili ya kujenga hospitali ya wilaya ya Manispaa ili kutoa huduma kwa wananchi.

“ Leo’ Februari 23, 2019 , naagiza hadi jumatano Februari 27 mwaka huu niwe nimepata taarifa ya utekelezaji wake , na nitaipima halmashauri ya wilaya ya Morogoro kwenye utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya kwa kiasi kilichobakia cha sh bilioni 1.5 sambamba na halmashauri nyingine “ alisema Jafo.

Pamoja na hayo alisema, atapanga kufanya ziara maalumu katika halmashauri hiyo kwa ajili ya kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo ya hospitali hiyo na endapo atakuta bado hawajaanza ama ujenzi wake unasuasua yuko radhi kuhamisha fedha hizo na kuzielekeza maeneo yaliyoonesha kasi kubwa ya ujenzi wa miradi ya kimkakati.

Kwa upande wake Meya Manispaa ya Morogoro , Pascal Kihanga, licha ya kutoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya tano kwa kutoa fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa vituo vya Afya alisema, Manispaa hiyo haijapewa fedha licha ya wananchi wamejitolea kujenga majengo ya vituo vya afya .

“ Wananachi wetu wamejitokeza kujenga zahanati na vituo vya afya , lakini kama halmashauri bado tumeshindwa kumalizia kwa ukosefu wa fedha za kutosha , tukipata Sh milioni 400 zitatuzaidia kukamilisha majengo haya na kutumiwa na wananchi” alisema Kihanga.

Hivyo alitumia fursa hiyo kumwomba Waziri kuipatia Manispaa hiyo fedha Sh milioni 400 kwa ajili ya kumalizia vituo vya afya ziliojengwa kwa nguvu ya wananchi ikiwemo na hospitali ya wilaya ambayo tayari jengo la utawala lilichajengwa miaka ya nyuma.

Mbali na hayo alimweleza juu changamoto ya jengo la standi Kuu ya mabasi ya Msamvu kuwa tangu agizo la Rais alilolitoa la kukabidhiwa stendi hiyo kwa Manispaa  hadi sasa bado hakuna utekelezaji wake na kuwomba waziri asaidie kulishungulikia.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa