• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JAFO ASHANGAA KUTOTEKELEZWA AGIZO LA RAIS LA KUIRUDISHIA MANISPAA YA MORO UENDESHAJI WA STENDI YA MABASI YA MSAMVU.

Posted on: October 16th, 2018

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) Selemani Jafo ameshangazwa na kusikitishwa na kitendo cha kutotekelezwa kwa agizo la Rais Dk John Magufuli kwa uliokuwa uongozi wa mfuko wa LAPF la kukabidhi uendeshaji wa mradi wa kituo cha mabasi Msamvu kwa Manispaa ya Morogoro.

Waziri Jafo alishangazwa na kauli hiyo baara ya kusikia taarifa kutoka kwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga , kuwa hadi sasa ni zaidi ya miezi minne stendi haijakabidhiwa s wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa soko jipya la kisasa la Manispaa hiyo hivi karibuni baada ya Serikali kuu kutoa fedha Sh bilioni 17.6 .

“ Nasikia kichefu chefu juu ya jambo hili , Rais aliagiza kuwa stendi ya mabasi ya Msamvu irudi Manispaa ya Morogoro , ni nani mwingine ambaye anayekwamisha utekelezaji huu , wakati akitoa agizo hili nami ( Jaffo) nilikuwepo jukwaani akiwahutubia wananchi wa Morogoro “ alisema Jafo .

Waziri Jafo alisema , Rais aliagiza Stendi ya Mabasi Msamvu irudi Manispaa ya Morogoro kwa kauli yake mbele ya wananchi  ( Mei 6, 2018) akiwa jukwaani , hivyo agizo la Rais halina mjadala kinachofuata ni hatua za utekelezaji .

Hata hivyo , Meya wa Manispaa ya Morogoro Kihanga kwa niaba ya uongozi wa halmashauri na serikali ya wilaya na mkoa alimshukuru Rais Dk Magufuli kwa kutoa fedha za ujenzi wa soko la kisasa.

Pia alimshukuru kwa agizo kwa iliyokuwa Menenimenti ya LAPF kukabidhi stendi ya mabasi ya Msamvu kwa Manispaa ili uendeshaji uwe ni wa asilimia 100 , licha ya agizo hilo kushindwa kutekelezwa kwa zaidi ya miezi minne tangu alipofanya ziara na kuzindua stendi hiyo.

Hata hivyo alisema , bado halmashauri ya Manispaa haijakabishiwa Stendi hiyo ingawa yamefanyika majadiliano baina ya pande mbili hizo na kumejitokeza kwa changamoto ya kiwango kikubwa cha fedha Sh bilioni 19 ambacho mfuko unataka ulipwe ili iweze kukabidhi uendeshaji kwa halmashauri wakati haina uwezo huo .

“ Tunakuomba Mheshimiwa Waziri utusaidie jambo hili kwa kuwa Mfuko huu upo chini ya Ofisi yako , tukabidhiwe ili tuweze kuanza kukusanya mapato kwa manufaa ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro” alisema Kihanga.

Mfuko wa LAPF kabla ya kuunganishwa mifuko iliyokuwa inahudumia watumishi wa Serikali na kuazishwa mfuko mpya wa PSSSF , iliingia kati yake na Manispaa ya Morogoro kwa kusaini makubaliono kujenga kituo hicho kinachopewa jina la Msamvu Properties Company (T) Limited ambapo umiliki wa hisa ulikuwa ni asilimia 60 kwa Mfuko huo , wakati Manispaa ikiwa na hisa ya asilimia 40.

Hata hivyo Mei 6, mwaka huu (2018) katika hotuba yake ya uzinduzi wa stendi hiyo , Rais Dk John Magufuli alisema kuwa , kutokana na mpango mzuri wa mradi huo na kwa vile serikali imekuwa inatoa fedha za ujenzi wa stendi kama hiyo kwenye halmashauri za wilaya nchini, serikali imeamua kulichukua deni lote lililokuwa ina daiwa na mfuko wa LAPF na kulipwa na serikali.

Katika hotuba hiyo alisema , baada ya kukabidhiwa stendi hiyo na LAPF ,Manispaa hiyo iweke utaratibu wa kuona kwamba kila mfanyabiashara mdogo anapata nafasi ya kufanya biashara katika kufuata utaratibu huo na si kuwabagua ikiwa ni pamoja na kuwa ni kitega uchumi cha kuiingizia mapato yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya uliokuwa uongozi wa wa mfuko huo mbele ya Rais wakati wa uzinduzi huo ilibainisha kuwa , awamu ya kwanza ya ujenzi wa kituo hicho ulikamilika Novemba 2016 kwa gharama ya sh bilioni 12 , pia kulikuwa na uendelevu wa ujenzi wa maduka madogo 80 ambao ulipangwa kuanza juni 2018 kwa gharama ya sh milioni 768.4.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa