• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JENISTA AWAPONGEZA WANUFAIKA WA TASAF MANISPAA MORO KWA KUANZISHA MIRADI YENYE TIJA KUJIPATIA KIPATO.

Posted on: August 8th, 2022

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Jenista Mhagama ameridhishwa na walengwa wa Mpango wa Kuzinusuru Kaya Maskini Manispaa ya Morogoro kwa kuendesha mradi wa funza chuma kwa ajili ya kuzalisha chakula cha mifugo kinachowaongezea kipato na kutatua changamoto ya upatikanaji wa chakula cha mifugo.

Jenista alisema hayo, baada ya kukagua mradi wa kuzalisha funza chuma, unaotekelezwa na walengwa wa TASAF wa kikundi cha Faraja kilichopo mtaa wa Mazimbu Darajani , Kata ya Mazimbu, Manispaa ya Morogoro.

Mpango huo wa Kuzinusuru Kaya Maskini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)

Alisema kumekuwa na shida ya upatikanaji wa chakula cha mifugo hivyo mradi huo unaotumia teknolojia rahisi kuzalisha funza chuma kwa ajili ya chakula cha mifugo utatatua changamoto ya upatikanaji wa chakula cha mifugo wakiwemo ng’ombe, kuku na Samaki.

“Mmesema hapa kupitia taarifa yenu kuwa, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimefanya utafiti na kubaini kuwa funza chuma ni chakula kizuri cha mifugo kuliko vyakula vingine ambavyo vimekuwa vikitumika kulisha mifugo na mradi huu ni mzuri na wa kimkakati ambao unapaswa kuendelezwa,”alisema Jenista

Alisema mradi huo utasaidia kuhifadhi mazingira na kutatua changamoto ya uchafu wa mazingira katika masoko kwani badala ya taka kutupwa hovyo ndani ya masoko, zitachukuliwa ili kuzalisha chakula cha mifugo na kuacha masoko yakiwa kwenye hali ya usafi.

“Huu mradi ni suluhisho kubwa la changamoto ya uchumi, uchafu wa mazingira na suala la ajira kwa makundi yote ya akina mama, vijana na wenye ulemavu na walengwa wa TASAF, kwani ni mradi fungamanishi wenye faida nyingi,”alifafanua Jenista

Naye Meya wa Manispaa ya Morogoro,Pascal Kihanga alisema mradi wa funza chuma una faida kubwa katika jamii, kwani utasaidia Manispaa kuwa na mazingira safi na kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwaongezea kipato.

“Kutokana na faida ya uwepo wa mradi huu, Manispaa ya Morogoro itawatumia Wahandisi waliopo kuwajengea walengwa wa TASAF na wananchi wengine vizimba vya kufuga funza chuma ili waweze kuzalisha kwa wingi chakula cha mifugo ambacho kitawaongezea kipato chao “ alisema Kihanga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa  Ally Machela alisema katika mwaka wa fedha wa Julai , 2021 hadi Juni , 2022 , Manispaa ilipokea jumla ya Sh milioni 904.2 .

Alisema fedha taslimu zilizolipwa kwa walengwa kwa njia ya mtandao na benki ni Sh milioni 390.9 ambazo zililipwa kwenye namba za simu na akaunti za benki za walengwa moja kwa moja.

“ Manispaa kupitia mpango huu inaendelea kutoa elimu kwa walengwa juu ya matumizi sahihi ya fedha na kuwahimiza kutoa taarifa , kuanzia viongozi wao wa Serikai za mitaa mara anapohama na kuripiwa katika Serikali ya mtaa wanapohamia “ alisema Machela.

Nao baadhi ya wanufaika na mpango huo kwa nyakati tofauti waliishukuru serikali kupitia TASAF kuwawezesha kifedha ambazo wamezitumia kusomesha watoto wao ,kuanzisha miradi midogo ya uzalishaji mali iliyowezesha kuwa na makazi bora .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa