• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JUKWAA LA UWEZESHAJI KIUCHUMI WANAWAKE MANISPAA YA MORO KUANZISHA KIWANDA CHA USHONAJI NGUO

Posted on: June 29th, 2018

MBUNGE wa Jimbo la Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood, ameliwezesha Jukwaa la Uwezeshaji wanawake Kiuchumi la Manispaa ya Morogoro ( JUWAKIMAMO) vyereheni 25 kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha ushonaji nguo ukiwa ni utekelezaji wa sera ya viwanda kukuza uchumi wa wananchi na taifa .

Mbali na Vyereheni hivyo pia alikabidhi seti moja ya kompyuta , printa , meza na viti kwa Uongozi wa Saccos ya Wanawake Manispaa ya Morogoro (SAWAMAMO) ambapo jumla ya vitu vyote hivyo vimegharimu zaidi ya Sh milioni 20.

Mbunge wa Jimbo alisema kuwa, vyereheni vilivyotolewa kwa Jukwaa hilo ni kwa ajili ya kufungua kiwanda cha ushonaji wa nguzo za aina mbalimbali zikiwemo za wanafunzi, akina mama na za wanaume .

Abood alisema , licha ya kiwanda hicho pia litafunguliwa darasa la kujifunza ufundi kwa watoto wakike waliomaliza elimu ya msingi na sekondari na kushindwa kuendelea ili baadaye waweze kujiajiri wao wenyewe kupitia ujuzi walioupata kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

“ Mradi huu utahusisha pia kuwekwa kwa mashine za kupukucha mahindi na kukamua alizeti … na hii ni kuonesha akina mama wa Manispaa ya Morogoro wanakuwa ni wa mfano Kimkoa kuweza kuwa na kiwanda kitakachowasaidia kujiari na kupata mapato” alisema Abood.

Hata hivyo alisema , mradi huo ni hatua ya utekelezaji wa Ilani ya CCM na pia kuunga mkono juhudi za Rais Dk John Magufuli alizohimiza kuhusu Sera ya Viwanda na akiwa Mbunge wa Jimbo hilo ni wajibu wake kuwa karibu na wananchi kuwasaidia kwa kutoa mchango wake .

“ Kiwanda hiki kitachangia kutoa mchango mkubwa wa kuinua uchumi wa akina mama wa Manispaa ya Morogoro na kutoa ajira kwa wengine “ alisema Abood.

Naye Mwenyekiti wa Jukwaa hilo ,Mary Kachale alimshukuru Mbunge huyo kwa kuwasaidia vyereheni kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha ushonaji nguo ambacho kitasaidia kuwakutanisha wanawake na vijana wakike kujifunza ujuzi wa ushonaji wa nguo ambao utawasaidia katika maisha yao ya kijamii na kiuchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Sawamamo Saccos , Beatrice Mogela ,licha ya kumshukuru Mbunge huyo alisema , seti ya Kompyta waliyopatiwa atawasaidia katika utunzaji wa kumbukumbu muhimu na kuondoa gharama za kuchapishaji wa nyaraka za masuala ya kiutawala .

Hata hivyo alisema , Saccos hiyo ina zaidi ya wanachama 900 waliopo kwenye vikundi 13 na ilianzishwa na mtaji wa Sh milioni tano na hadi sasa umefikia Sh milioni 11.8 ambapo utoaji wa mikipo kwa kikundi utaongezeka kutoka Sh milioni mbili hadi milioni 2.3 kuanzia Julai mwaka huu ( 2018).

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa