• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JUMLA YA WATOTO 32,093 SAWA NA 72.5% CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO MANISPAA YA MOROGORO WAPATA USAJILI WA VYETI VYA KUZALIWA.

Posted on: March 12th, 2020

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, imetoa taarifa ya ujumla ya watoto 32,093 sawa na 72.5% chini ya umri wa miaka mitano wapata usajili wa vyeti vya kuzaliwa uku Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro akisisitiza wazazi na walezi kuwaandikisha watoto wote ambao hawajaandikishwa kabla ya Machi 15 2020

Taarifa hiyo imetolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga katika Ofisi yake Manispaa ya Morogoro leo Machi 12, 2020.


Akizungumza na Waandishi wa habari, Meya Kihanga, amesema Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inajumla ya watu 315,866, ambapo Kati ya hao watoto chini ya miaka mitano  ni 44,472.


Amesema kuwa, awali zoezi la usajili wa vyeti vya kuzaliwa lilikuwa likitekelezwa na Ofisi za RITA ambao kwa sasa wanaendelea kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kuanzia umri wa miaka mitano na kuendelea.


Amesema kuwa tangu mpango wa kusajili vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ulipoanza, jumla ya watoto 32,093 (sawa na asilimia 72.5) wamesajiliwa hadi kufikia tarehe 20 Februari, 2020.


Aidha amesema kuwa , kuanzia tarehe 6/12/2019 na kuendelea zoezi la usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka 5 linatekelezwa na Halmashauri kupitia Ofisi za kata na vituo vya kutolea huduma za afya vinavyotoa huduma ya baba, mama na mtoto (Kliniki) ambapo vyeti hivyo vinatolewa bila malipo.

Meya Kihanga, amesema vyeti hivyo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano vina faida kwakuwa ni utambulisho wa awali kisheria utakaomwezesha mtoto kupata haki nyingine kama kuzuia ajira ya watoto na kuwalinda na watu wanaokinzana na sheria, kummsaidia mtoto kuandikishwa shule za Msingi na Sekondari,ni kitambulisho cha msingi ili kupata kitambulisho cha Taifa, Kuwawezesha wanafunzi kujiunga na vyuo na elimu ya juu na kupata mikopo ya elimu ya juu pamoja na kumsaidia kupata hati ya kusafiria ( Passport).

Amesema miongoni mwa vitu muhimu vya kwenda navyo wazazi /walezi katika kituo cha Usajili ni pamoja na nakala ya kadi ya kliniki au tangazo, barua ya mwenyekiti wa Mtaa, Cheti cha ubatizo ambapo aliwataka

Wazazi /Walezi kuhakikisha kwamba ifikapo tarehe 15/03/2020 watoto wote chini ya umri wa miaka mitano wanaoishi Halmashauri ya Manispaa Morogoro kilamtoto awe ameshasajiliwa na kupata cheti cha kuzaliwa.

"Niwaombe wazazi/ walezi wapelekeni watoto wenu wakapate haki yao ya vyeti vya kuzaliwa, kwani zoezi hili la utoaji wa vyeti vinatolewa  katika ofisi zote za kata na vituo vyote vinavyotoa huduma ya baba, mama namtoto ( Kliniki), lakini pia cheti hiki cha kuzaliwa kinapatikana bila malipo huku ikibebwa na kauli mbiu ya “ Mtoto anastahili cheti cha kuzaliwa , Mpe haki yake”Amesema Meya Kihanga .

Pia ametoa wito kwa Madiwani pamoja Wenyeviti wa Mitaa wapite katika maeneo yao na endapo kuna watoto hawaja sajiliwa waandikishwe.

Katika hatua nyingine, amezitaja Kata ambazo zimefanya vizuri na zile ambazo hazikufanya vizuri huku akitaja sababu kubwa ya kufanya vibaya kwa baadhi ya Kata ni pamoja na uelewa mdogo wa wananchi, utamaduni wa kusema wenye dhamana wahamasishe zaidi.

Kata ambazo zimefanya vizuri zaidi ya asilimia 100 katika usajili wa watoto chini ya umri wa miaka mitano katika vyeti vya kuzaliwa ni pamoja na Kata ya Kihonda, Mkundi , huku kata zilizofanya vibaya chini ya asilimia 40 ni Kata ya Mbuyuni, Kata ya Magadu, Kata ya Mji Mkuu pamoja na Kata ya Kauzeni.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa