• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KAMATI YA SIASA YA CCM YAIPONGEZA MANISPAA YA MOROGORO KWA UJENZI WA JENGO LA UDHIBITI UBORA WA SHULE.

Posted on: December 6th, 2019

KAMATI ya Siasa ya  Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Morogoro, imeipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kufuatia kujenga kwa ubora na kasi kubwa jengo la Ofisi ya Uthibiti Ubora wa Shule Manispaa ya Morogoro.

Hayo yamezungumza  na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro, Ndg. Fikiri Juma , wakati wa ziara ya kutembelea miradi yote ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa Habari , amesema kasi na ubora wa Ujenzi unaonesha dhahiri Manispaa imekimbizana na inastahili pongezi ya hali ya juu kwani licha ya ubora lakini imeonesha ni jinsi gani imezingatia  thamani ya pesa iliyotumika.

Aidha, amesema kuwa kama viwango hivyo , vilivyotumika katika mradi huo wa Ofisi ya Uthibiti Ubora wa Shule vikitumika katika miradi mingine Manispaa ya Morogoro itapiga hatua na kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Amesema kuwa Ujenzi huo umeonesha thamani ya pesa iliyotumika , hivyo ameiagiza Manispaa ya Morogoro kuhakikisha inasimamia vizuri na miradi mingine inayoendelea kutekelezwa na ile ambayo itatekelezwa.

Pia amemuomba Mthibiti wa Ubora wa Shule Manispaa ya Morogoro kuhakikisha katika majukumu yao wanawashirikisha Manispaa , Maafisa Elimu, Waalimu wakuu wa Shule, pamoja na Bodi za Shule ili kuangalia ni kwa namna gani wanaweza kufanya kazi pamoja na kuleta maendeleo chanya  katika suala zima la taaluma Shuleni.

" Nafahamu kwamba mpo chini ya Wizara ya elimu , shirikianeni na Manispaa , lakini niwaombe taaluma yoyote haiwezi kupanda kama Mtoto hajapata chakula vizuri , licha ya kufanya kazi za uthibiti ubora lakini suala la lishe kwa wanafunzi ni jambo la kulipa kipaumbele sana, niwaombe na kuwashauri katika vikao vyenu hakikisheni wajumbe wa bodi wanakwenda kushirikiana na Madiwani ambao wana ushawishi mkubwa wa kuongea na Wazazi ili waweze kuchangia chakula shuleni na watoto wafanye vizuri katika masomo yao" Amesema Fikiri

Amesema kuwa Shule nyingi hapa nchini zimetumia sana fedha katika ujenzi Mhe. Rais Dkt John Magufuli amejitahidi kuwekeza katika mpango wa Elimu bure bila malipo, hivyo ni wajibu wa kuhakikisha pamoja na ubora wa shule lakini matokeo yaonekane katika viwango vya ufaulu.

Hata hivyo, Mwenyekiti Fikiri amempongeza Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro, Eng. Juma Gwisu kwa kazi nzuri anazozifanya katika kusimamia ubora wa miradi.

Kwa upande wa Mthibiti wa Uthibiti Ubora wa Shule Manispaa ya Morogoro, Bi. Victoria Michael Bengesi, amesema kuwa  Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Halmashuri 100 nchini, zilizo  katika mpango wa Serikali wa kujengewa Ofisi za Uthibiti Ubora wa Shule Wilaya.

Bi Victoria amesema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa tarehe 1, Julai, 2019 kwa kipindi cha miezi mitatu ya utekelzaji hivyo kuchelewa kwake kumechangiwa na baadhi ya changamoto kama vile kutokuwepo kwa maji eneo la ujenzi, kuchelewa kwa vifaa kama vile Saruji na mabati kutoka kwa msambazaji hasa wa Viwanda kwa takribani wiki mbili na kuchelewa kupatikana kwa matofali yanayofaa kutoka kwa msambazaji aliyeteuliwa.

Aidha amesema mradi huo umegharimu jumla ya Shilingi Milioni 152 ambapo pesa hizo zimejumusiha gharama ya ujenzi pamoja na ununuzi wa samani na vifaa.

"Utekelezaji wa mradi huu umekamilika kwa asilimia 100, hivyo kwa sasa shughuli zinazoendelea ni pamoja na ufungaji wa milango, upigaji wa rangi awamu ya mwisho, uwekaji wa marumaru eneo la vyoo vya ndani pamoja na ufungaji wa mfumo wa umeme" Amesema Bi. Victoria

Katika hatua nyengine, amesema licha ya shughuli hizo kuendelea , zipo shughuli nyingine za ziada ambazo zimeongezeka kutokana na uhitaji na mazingira halisi ya ofisi ilipo.

Miongoni mwa shughuli hizo ni pamoja na Uwekaji wa uzio kwa ajili ya usalama wa Ofisi, Ujenzi wa kibanda cha mlinzi, Ujenzi wa Choo cha nje chenye matundu mawili na Ujenzi wa Karavati ili kuwezesha uingiaji na utokaji katika eneo la Ofisi kwa urahisi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa