• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KATA YA SABASABA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUWAKUMBUKA WATOTO WENYE UHITAJI.

Posted on: March 7th, 2023

KATIKA kilele cha maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani, Kata ya Sabasaba Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na Vikundi vya wanawake wameadhimisha siku hiyo kwa kuwakumbuka watoto wenye mahitaji maalum shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.

Maadhimisho hayo yamefanyika Machi 8/2023 yakiambatana na Maandamano.

Akizungumza katika Kongamano hilo, Diwani wa Kata ya Sabasaba ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Mohamed Lukwele, amesema wadau wamependekeza shule hiyo kwa kuwa ina watoto ambao hawana uwezo wa kusikia na baadhi ambao hawana uwezo wa kuona vizuri.

“Shule hii inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa mahitaji kama vile pempapasi ambapo wengine wamekuwa wakitokwa na haja , zipo changamoto nyingi nyingi sana kwa kutambua hilo ndugu zetu wanavikundi wameona watutembelee tunawashukuru sana kwani walichokitoa sisi kwetu ni kikubwa" Amesema Lukwele.

Upande wa Kaimu Mtendaji Kata ya Sabasaba , Abubakari Dikungule, ameshukuru wadau hao na kuomba kuendelea kujitoa kwa watoto wenye uhitaji.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Sabasaba, Asnaty Dibwe, amevishukuru vikundi vya Msimamo B Vikoba na Sabasaba Women kwa mahitaji ambayo wametoa kwa watoto hao na kuwafanya watoto kufarijika na kuwatoa katika upweke na wao kutambua wapo wanaowajali.

Mwakilishi wa Vikundi hivyo, Bi. Velda Msangi, amesema wameguswa na uhitaji wa watoto katika shule hiyo, hivyo watajipanga kuona namna ya kutoa zaidi ya hapo.

Aidha, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Dotto Kangeta , amevishukuru vikundi pamoja na Mhe. Diwani na Uongozi wa Kata kwa kuifanya shughuli hiyo katika shule yake na kutoa wito kwa wadau wengine kuwakumbuka watoto wenye uhitaji ili waweze kufarijika na mwisho kutimiza malengo yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa