• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KAZI YANGU YA KWANZA NI KUHAKIKISHA KUWA MOROGORO INAKUWA NA MISINGI YA AMANI - MHE. ADAM MALIMA, RC MORORORO

Posted on: May 26th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kazi yake ya kwanza kama Mkuu wa Mkoa huo ni kuhakikisha kuwa kuna Amani na Utulivu ndani ya Mkoa  kwa ajili ya wana morogoro pamoja na wawekezaji wanaotamani kuja kuwekeza ndani ya Mkoa huo.

Mhe. Kigoma Malima amesema hayo Mei 26, 2023 wakati wa kikao cha kujitambulisha kwa Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa huo kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ikiwa ni mara yake ya kwanza kufanya kikao na wajumbe hao tangu alipoteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wiki moja iliyopita kushika nafasi hiyo.

Amesema, jukumu lake la kwanza kama Mkuu wa Mkoa ni kulinda Amani na Utulivu viwepo hivyo wananchi kuendelea kufanya kazi zao za uzalishaji mali kwa Amani na utulivu lakini pia Amani hiyo itawezesha wawekezaji kuvutiwa kuja kuwekeza ndani ya Mkoa wa Morogoro

“Kwa hiyo, kazi yangu ya kwanza ni kuhakikisha kwamba Morogoro ina misingi ya AMANI na UTULIVU inayoongoza wananchi kufanya kazi zao ” amebainisha Mhe. Adam Malima.

Aidha, amesema jukumu lake la pili ni kusimamia maendeleo ya wananchi wa Morogoro na ya Serikali kwa ujumla kwa kuangalia na kushauri utekelezaji wa miradi hiyo ya Serikali inayotekelezwa ndani ya Mkoa huo.

Hata hivyo, amesema ili kutekeleza majukumu hayo makubwa ushirikiano unahitajika, kwa kuwa peke yake hawezi kukamilisha azma hizo za Mkoa na Serikali ya awamu ya sita, isipokuwa ni kwa kufanya kazi kama timu.

Akisisitiza suala la ushirikiano amesema kwenye suala la Amani, Wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama watatakiwa kumpa ushirikiano wa kutosha ili kuendelea kudumisha Amani ya Mkoa na kwa upande wa usimamiaji wa miradi ya maendeleo Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa wanatakiwa kuwajibika na kutoa ushirikiano huo kwake.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa huo kubadilika na kufanya kazi kulingana na wakati na mazingira yaliyopo badala ya kuendelea kufanya kazi kwa mazoea.

Aidha, amewataka Wajumbe hao kuwa na desturi ya kuwasiliana baina ya idara moja na idara nyingine katika utekelezaji wa majukumu yao jambo ambalo amesema bado ni changamoto katika taasisi hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa