• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MABILIONI YA FEDHA YATOLEWA NA SERIKALI KUZIWEZESHA HALMASHAURI KUJENGA MIRADI YA KIMKAKATI

Posted on: October 14th, 2018

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) Sulemani Jafo amewaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri nchini ambazo zinaendelea kujenga miradi ya kimkakati ya masoko na vituo vya mabasi kuhakikisha inajengwa kulenga mahitaji ya wafanyabiashara wote na kutoa kipaumbele cha kwanza kwa waliokuwepo awali kabla ya miradi hiyo.

Waziri Jafo alitoa agizo hilo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa soko jipya la kisasa la Manispaa ya Morogoro hivi karibuni mara baada ya Serikali kuu kutoa fedha Sh bilioni 17.6 .

Alisema ,kwa sasa Serikali ya awamu ya tano imetoa Sh bilioni 146 kwa miradi 22 ya aina hiyo katika halmashauri mbalimbali nchini ,lengo ni kuzifanya halmashauri zijitegemee kwa njia ya mapato na kujiimalisha kiuchumi .

Jafo alisema , baada ya kutolewa kwa fedha hizo , anao wajibu wa kufanya ziara ya kikazi ya kukagua na kujilidhisha utekelezaji wa miradi hiyo kuanzia mkoa wa Dar es Salaam pamoja na Morogoro ambapo ujenzi wa soko la kisasa unafanyika .

“ Rais wetu anayo malengo ya kuziwezesha halmashauri zetu zikuwe kiuchumi kupitia vitenga uchumi vyake ikiwemo ya kujengwa kwa masoko mapya ya kisasa likiwemo la la Manispaa ya Morogoro” alisema Jafo.

Hivyo alitumia fursa hiyo kutoa agizo kwa wakurugenzi wote wa halmashauri kuwa patia sehemu za kufanya biashara ‘vizimba ‘ wafanyabaishara wadogo ambao waliopisha maeneo ya masoko ya zamani kuwezesha ujenzi wa masoko mapya ya kisasa.

“ Hapa halmashauri ya Manispaa orodhesheni majina ya wafanyabiashara waliokuwepo zamani na kupisha ujenzi ili mara baada ya kukamilika wawe wa kwanza kupata maeneo na si kuwanufaisha wafanyabiashara wakubwa ama viongozi wa serikali wenye uwezo …hili nalitoa kama agizo kwa nchi nzima “ alisema Jafo.

‘ Si kwamba hatukatai hawa wafanyabiashara wakubwa wasifanye biashara ila kipaumbele kiwe ni wa wafanyabiashara wadogo na mama lishe wakitengewa maeneo yao” alisema Jafo.

Akizungumzia ujenzi wa soko hilo, Waziri huyo aliwasifu wakandarasi kwa kuonesha uwezo wao kwa maandalizi ya awali ya ujenzi na kuwaagiza kujenga soko hilo kwa kuzingatia viwango vya ubora kwa kuwa ni fedha nyingi zimetegwa kwa ajili hiyo.

Hata hivyo aliwahakikishia kuwa , Serikali itawalipa kwa wakati fedha zinapokuwa zinahitajika kwa ajili ya kuendelea na ujenzi hadi kufikia kukamilishwa kwake ifipako Augosti 2019.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Mgalula katika taarifa yake kwa Waziri Jafo alisema kuwa eneo la ujenzi wa soko lina ukubwa wa mita za mraba 23, 432 ambapo fedha hizo zimetolewa na Wizara ya Fedha kupitia hazina .

Alisema , soko hilo lenye ghorofa mbili litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua wafanyabiashara zaidi ya 2,000 na ujenzi wake unafanyiwa na Kampuni ya Uhandisi na ujenzi ya Nandhra ambao ilishinda zabuni na kuingia mkataba wa ujenzi .

Kwa upande wake ,Meneja wa mradi huo kutoka Kampuni ya Uhandisi na Ujenzi ya Nandhra , Rabinder Singh alimhakikishia waziri huyo kuwa watafanya kazi kadiri ya uwezo wao kwa kushirikiana na timu ya Manispaa pamoja na msimamizi na Mshauri wa mradi huo kukamilisha ujenzi huo kwa muda wa miezi 12 kama ulivyopangwa.

Soko jipya linalojengwa ni la kisasa na lenye ghorofa mbili kwa ajili ya matumizi ya wafanyabiashara wa aina mbalimbali na kujengwa huko ni baada ya soko la zamani iliyojengwa mwaka 1953 lilivunjwa miaka miwili iliyopita kutokana na uchakavu mkubwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa