• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MABORESHO MAKUBWA KUFANYIKA KWA SHULE ZA MSINGI NCHINI

Posted on: January 10th, 2023

SERIKALI imetenga kiasi cha Sh trilioni 1.15 kwa ya matumizi ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya shule za msingi zilizochakavu kupitia Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST), katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka huu wa fedha.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) Angellah Kairuki, alisema hayo Januari 9, 2023 mjini Morogoro wakati akifungua kikao kazi cha mapitio ya tathimini ya utekelezaji wa shughuli za uboreshaji na usimamizi wa elimu kwa mwaka 2022 na mpango mwaka 2023.

Mpango wa ujenzi na ukaratabi wa miundombinu ya shule hizo unatarajia kuanza kutekelezwa Januari na Februari mwaka huu nchini kote.

Waziri alisema kuwa baadhi ya shule zitavunjwa na kujengwa upya ,nyingine zitafanyiwa ukarabati mkubwa pamoja na mdogo kwa lengo la kuzifanya ziwe na mazingira bora kulingana na hali ya sasa kwa walimu na wanafunzi.

Alisema Serikali inatambua shule nyingi ni za muda mrefu ambazo zilijengwa na Serikali, wadau na wazee na nyingine kwa njia ya kujitolea ambazo zimeweza kudumu kwa muda mrefu na imefika wakati sasa wa kuziboresha shule hizo.

Waziri alisema katika kuendelea kuimarisha elimu ya Sekondari kupitia mradi wa SEQUIP, ambapo Jumla ya sh trilioni 1.2 zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya 1,026 ( Za kata 1,000 na za bweni za wasichana za Mkoa 26) katika kipindi cha miaka mitano.

Waziri huyo alisema mwaka 2021 jumla ya shule mpya 232 za sekondari za Kata zimeshajengwa na 10 za bweni za wasichana za mikao zinaendelea kukamilisha ujenzi wake.

Alisema kwa mwaka 2022/23, Serikali inategemea kujenga shule mpya za Kata 184, moja kila Halmashauri na shule tano (5), za bweni za wasichana kwenye mikoa mitano.

Waziri pia alisema kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu Serikali itatoa sh milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa shule moja ya sekondari kwa kila Halmashauri nchini

“Nitumie fursa hii kumshukuru na kumpongeza Mhe. Dk Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa hizi anazoendelea kuzifanya katika kuimarisha na kuboresha sekta ya Elimu nchini” alisema Kairuki

Kwa upande uandikishwaji wa wanafunzi wa darasa la awali na msingi nchini aliagiza watendaji wa sekta ya elimu , wakurugenzi wa Halmashauri , wakuu wa wilaya na mikoa kuongeza kasi ya kusajili wanafunzi ili kufikia malengo ya yaliyokusudiwa ya asilimia 100 .

“Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa muendelee kuhamasisha uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali na msingi ili kuhakikisha mnafikia malengo ya uandikishaji mliyokuwa mmejiwekea” alisema Waziri Kairuki

Waziri Kairuki alisema “Kila kiongozi akahakikishe anaimarisha uwajibikaji wa watumishi wote katika ngazi zote ili kuongeza tija katika utendaji wa kazi” alisisitiza Waziri

Hivyo alisema natarajia kuanzia Januari 2023 kutakuwa na mabadiliko makubwa katika usimamizi wa elimu msingi na sekondari katika shule zetu.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Elimu Tamisemi, Vicent Kayombo alisema utekelezaji wa sera ya elimu bila ada imeongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa kujiunga elimu ya awali, msingi na sekondari nchini

Kayombo alisema bado zipo changamoto kadhaa ikiwemo kwa wanafunzi wanao maliza darasa la saba hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu huku kukiwa na wanafunzi asilimia 20 wanaoshindwa kufaulu mtihani wa elimu ya msingi na kushindwa kujiunga na kidato cha kwanza.

Pia alisema kumekuwepo na idadi ndogo kwa wanafunzi wanaofaulu mtihani wa kidato cha nne kwa daraja la kwanza hadi tatu likiwemo somo la Kiingereza .

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Fatma Mwassa,katika taarifa yake kwa Waziri alisema kuwa ,wanafunzi walioandikishwa darasa la awali na msingi hadi kufikia Januari 6, mwaka huu walifikia 74,578 kati ya hao wavulana 37,342 na wasichana 37578 sawa na asilimia 94.5 .

Mwassa alisema miongoni mwa wanafunzi hao ni wakiwemo wenye mahitaji maalum na kwamba hali ya uandikishaji bado inaendelea katika shule zote katika mkoa wa Morogoro.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) Angellah Kairuki, akizungumza na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya mkoa na Halmashauri  Januari 9, 2023 mjini Morogoro wakati akifungua kikao kazi cha mapitio ya tathimini ya utekelezaji wa shughuli za uboreshaji na usimamizi wa elimu kwa mwaka 2022 na mpango mwaka 2023.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa