• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MAFIGA WAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA KUZINDUA BARAZA LA WATOTO

Posted on: June 14th, 2023


KATA ya Mafiga Manispaa ya Morogoro imeadhimisha kilele cha Siku ya Mtoto wa Afrika Duniani pamoja na kuzindua Baraza la Watoto la Kata hiyo.

Maadhimisho hayo yamefanyika Juni 14/2023 Mtaa wa CCM ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku hiyo ambayo Manispaa ya Morogoro itaadhimisha katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwembesongo Juni 16/2023.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, mgeni rasmi Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Morogoro , Treiness Kadinda, amewataka wazazi kuwajali na kuwapenda watoto wao kwani waliwaleta duniani kwa mapenzi yao wenyewe yawapasa kuwalea na kuwakinga na ukatili wa kijinisia.

Kadinda , amesema kuwa, wazazi wanawajibika kikamilifu katika kuhakikisha watoto wao wanapata elimu, kuwalinda na ukatili wa kijinsia pamoja na kupinga ndoa za utotoni ambazo zinawakatisha masomo watoto hao.

"Hakuna mtoto aliyeomba kuja duniani bali ni sisi wazazi kwa starehe zetu tumewaleta hawa watoto na lazima tuwajali na kuwalinda, kuwapa elimu na pia kutowakatisha masomo yao na kupelekea ndoa za utotoni," Amesema Kadinda.

Aidha, Kadinda, amewataka Watoto kuripoti matukio yanayokiuka haki za watoto na kuzitolea haki za watoto kwa mlezi aliye karibu nawe na unayemwamini au kupiga simu namba 116 kupata msaada zaidi ili watoto waendelee kuwa katika mazingira huru na yenye furaha na amani kwa kupata haki za msingi.

kwa upande wa Diwani wa Kata ya Mafiga, Mhe. Thomas Butabile, amesema kuwa watoto ni tunu ya taifa yapaswa kulindwa kwani kauli mbiu ya mwaka huu katika siku ya mtoto wa Afrika kwa hapa nchini inayosema " ZINGATIA USALAMA WA MTOTO KATIKA ULIMWENGU WA KIDIJITALI" inalenga katika kuhamasisha ulinzi wa watoto kwani watoto wamekuwa wakijiingiza katika mitandao ya kijamii na kuiga tamaduni ambazo sio aili ya mwafrika.

Afisa Lishe Manispaa ya Morogoro, Jacqueline Mashurano,amewataka wazazi kuwapatia watoto matone ya vitamini A pamoja na dawa za minyoo.

Mashurano, amewataka wazazi kuzingatia lishe bora kwa watoto ili wawe na afya bora.

Aidha, ameshauri shuleni kuanzishwa klabu za lishe kwa ajili ya watoto kupewa elimu bora ya lishe katika kutokomeza hali ya udumavu kwa watoto.

Mtendaji Kata ya Mafiga , Amina Saidi, amewataka Wazazi na Walezi kuimarisha upendo na umoja kwani familia ndio msingi Mkuu wa malezi ya Mtoto kwenye jamii na kuwataka Watoto kuheshimiana,kupendana na kuthaminiana.

Katika hatua nyingine, Kata ya Mafiga iliweza kuzindua Baraza la Watoto ambapo mgeni rasmi wa maadhimisho hayo aliweza kuzindua Baraza hilo.

Maadhimisho haya yalienda sambamba utoaji wa elimu ya lishe na watoa huduma wa lishe ngazi ya Kata waliweza kugawa uji kwa watoto ambao umechanganywa na mchanganyiko wa lishe mbalimbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa