• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MAJALIWA ATOA MAAGIZO KWA WATENDAJI WA HALMASHAURI NCHINI NA WAKALA WA VIPIMO.

Posted on: October 4th, 2018

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameziagiza halmashauri zote nchini kuendelea na kazi ya kupima ardhi za makazi na mashamba na kutoa hati ili wananchi wazitumie kupata mikopo na kuonya kuwa serikali haitasita kuchukua hatua kwa maafisa watakao hujumu ugawaji wa mashamba pori kwa wakulima kwa manufaa yao binafsi.

Pia ameuagiza Wakala wa Vipimo nchini kwa kushirikiana na halmashauri zote kuendesha msako wa vipimo maalumu ili kuwachukulia hatua wafanyabiashara wanaotumia vipimo vya lumbesa kununua mazao ya wakulima kwa vile ni unyonyaji na kuwataka MVIWATA kuisaidia serikali katika hilo.

Waziri Mkuu alitoa maagizo hayo katika hotuba yake ya kufungua maadhimisho ya miaka 25 ya Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania ( MVIWATA) jana kwenye uwanja wa Jamhuri wa mjini Morogoro.

Waziri Mkuu aliyekuwa mgeni rasmi katika ufunguzi alimwakilisha Rais Dk John Magufuli ambapo pia Waziri wa Kilimo, Dk Charles Tizeba alishiriki kwenye ufunguzi huo na kumkaribisha waziri mkuu.

“ Wakala wa vipimo endesheni oparesheni ya kukamata mfanyabiashara yoyote anayebeba lumbesa na shirikianeni na halmashauri , hatuwezi kuruhusu wizi wa rejareja …fanyeni kazi yenu na nitapita huko kujua kwanini lumbesa bado ipo “ alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Hata hivyo alisema, Serikali ya awamu ya tano inatambua umuhimu wa wakulima wadogo na mchango wao katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara , hivyo itaendelea kushirikiana nao kupitia Vikundi vyao ya ushirika ikiwemo MVIWATA.

Waziri mkuu lisema , mpango wa sasa ni kuona mazao yanalimwa kitaalamu kwa kufuata ushauri wa watalamu wa kilimo na ili kufanikisha jambo hilo , Serikali kupitia wizara ya kilimo itaendelea kusambaza pembejeo na mbolea kwa wakati kwa wakulima nchini .

Hata hivyo alisema , katika utekelezaji wa serikali kwenye sekta ya kilimo kiasi cha sh: bilioni 56.45 zimetolewa kwa ajili ya mikopo ya kilimo kupitia Benki ya Mendeleo ya Kilimo hasa katika zao la kahawa na mahindi kwa wanufaika 527,000 katika mikoa 13 nchini na upelekaji wa tani milioni 2.2 za mbolea na dawa maeneo ya wakulima vijijini.

Waziri mkuu pia alitioa agizo kwa Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwezeshaji , Charles Mwijage kufika kushiriki kwenye kongamano ya wakulima wa MVIWATA kusikiliza kero zao kwa lengo la kuzifanyia kazi kuagiza watendaji wa wizara husika za kilimo, ardhi na kutaka benki zote kushiriki kongamano litakalofanyika mjini Morogoro .

Alisema , lengo ni kushiriki kujadili masuala mbalimbali ya wakulima ili waweze kuishauri serikali namna ya kukabiliana na changamoto hizo wakiwemo na Wakurugenzi wa watendaji wa mabenki yanayohusika na utoaji wa mikopo.

Naye Mwenyekiti wa MVIWATA, Abdul Gea alimweleza Waziri mkuu juu ya changamoto ya bei ya mazao kuendelea kushuka chini tangu msimu wa mwaka 2017/2018 na bado mazao mengi yapo magharani hali inayochangia wakulima kuendelea kuwa maskini licha ya kuongeza kiwango cha uzalishaji wa mazao .

Hata hivyo alisema , wakulima wanayo imani ya serikali ya awamu ya tano kuweza kusaidia kupata masoko ya uhakika na wenye bei nzuri kwa ajili ya kuua mazo yao .

Mkurugenzi Mtendaji wa MVIWATA, Stephen Ruvuga alisema, kongamano la kitaifa la wakulima lenye mada inayohusu “ujenzi wa uchumi wa viwanda nini nafasi ya wakulima wadogo” limeshirikisha wanachama zaidi ya 2,400 kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa