• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA KUJENGA SHULE YA MSINGI YA DHARULA LUKOBE

Posted on: January 31st, 2024


Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Manispaa Morogoro ikiongozwa Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, mheshimiwa Pascal Kihanga, wameridhia kujenga shule ya msingi ya dharula kwenye eneo la shule ya sekondari Tushikamane kwenye Kata ya Lukobe, ikiwa ni jitihada ya Manispaa ya kuhakikisha wanafunzi wa shule ya msingi Juhudi wanaendelea na masomo yao baada ya shule yao kufungwa hivi karibuni kwa ajili ya usalama wa wanafunzi na walimu dhidi ya mafuriko ambayo yametokea mara kadhaa shuleni hapo katika kipindi hiki cha mvua.

Ridhaa hiyo imekuja mara baada ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, ndugu Ally Machela kuwasilisha ombi la ujenzi huo, ambapo alisema Kamati yake ya Wataalamu (CMT) pia wamesharidhia na hivi sasa wanasubiri kibali kutoka Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Morogoro ndipo ujenzi uanze haraka ili ndani ya siku tano ujenzi uwe umekamilika na wanafunzi waanze kutumia madarasa hayo.

“Kiuhalisia, panahitajika madarasa zaidi ya 20 ili kukidhi uhitaji kwa sababu shule ya Juhudi ina wanafunzi zaidi ya 1600. Lakini kwa kuwa ni dharula, tutajenga madarasa kumi ya dharula na vyoo vya dharula kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tano, tutakamilisha maboma mawili kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la awali na Ofisi ya walimu.

Tunataka baada ya kupata ruhusa ya kuendelea na ujenzi kutoka Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, tupeleke timu kubwa pale chini ya wahandisi wetu ili ndani ya siku tano ujenzi uwe umekamilika na watoto wetu waweze kwenda kuendelea na masomo yao” ameeleza Machela.

Tarehe 25.01.2024, shule ya msingi Juhudi, iliyopo kwenye Kata ya Lukobe ilizingirwa na maji yaliyotokana na mvua kubwa iliyonyesha siku hiyo. Hali hii ilipelekea Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Morogoro, ambaye pia ndiye Mkuu wa Wilaya hiyo, mheshimiwa Rebecca Nsemwa kuifunga shule hiyo ikiwa ni tahadhari dhidi ya madhara yanayoweza kutokea tena kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa