• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA MORO YAWEKA MAZINGIRA BORA YA UTOAJI HUDUMA KWA WAZEE.

Posted on: June 18th, 2019

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imetenga kiasi cha Sh milioni 10 kwa ajili ya matumizi ya upatikanaji wa vitambulisho vya wazee vitakavyowawezesha kupatiwa huduma mbalimbali zikiwemo za matibabu bure .

Pia halmashauri imeandaa vitambulisho vya wazee 4,002 kati ya hivyo wanaume 1,521 na wanawake 2,481 sambamba na kuwalipia wazee 3,378 bima ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF iliyoboreshwa) wakiwemo wanaume 1,462 na wanawake ni 1,416 .

Kaimu Mganga wa Manispaa ya Morogoro , Vulfrida Kyara, alibainisha hayo kwenye kongamano la siku ya kuelimishana kupinga ukatili dhidi ya wazee Duniani ambapo kauli mbiu yake ni “ Tuungane Kupaza Sauti ya Wazee 2019”.

Kongamano hilo ngazi ya Manispaa ya Morogoro ambalo liliandaliwa na Shirika la kusaidia Wazee mkoa wa Morogoro (MOREPEO), kwa kushirikiana na Shirika la kimataifa la HelpAge.

Hata hivyo Kaimu Mganga mkuu wa Manispaa alisema , licha ya vitambulisho hivyo kudumu kwa muda wa mwaka mmoja , wazee wamekuwa wakipewa kipaumbele cha kwanza wanapofika kupata matibabu kwenye zahanati na vituo vya afya.

Katika hatua nyingine , Kyara aliungana na wazee wa Manispaa juu ya changamoto ya walioko kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,(NHIF), kwa kushindwa kupata dawa katika vituo vya afya licha ya sasa vina madaktari wenye uzoefu.

“ Kwa sasa kuna maboresho makubwa ya huduma za afya zinazotolewa na Serikali na Vituo vya Afya vimeboreshwa na vina madaktari wa magonjwa tofauti ambao wanauwezo wa kutoa dawa ,lakini mgongwa mwenye NHIF hawezi kupata dawa alizoandikiwa hata kama kituo kina daktari mbobezi” alisema Kyara.

Nao wazee hao waliiomba Serikali kupitia upya Sera ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuzingatia namna orodha ya magonjwa na dawa zinapaswa kutolewa kuanzia ngazi ya zahanati, kituo cha afya na hospityali na hasa ngazi ya vituo vya afya kwa vile sasa vina madaktari wengi tofauti na huko nyuma.

Katibu mkuu wa Baraza la Wazee wilaya ya Morogoro, Dk Bakil Anga licha ya kuipongeza Serikali kwa juhudi kubwa inazoendelea kufanya ili kuhakikisha maisha ya wazee wote nchini yanakuwa bora na salama zaidi alitaka mkakati endelevu wa uundwaji wa mabaraza ya wazee yawe jumuishi na TAMISEMI.

Naye Mkurugenzi wa MOREPEO, Samson Msemembo alisema ,wazee wanakabiliwa na changamoto nyingi hasa katika huduma za afya hivyo ameziomba mamlaka husika kuwasaidia kwa karibu zaidi.

Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro ,Pascal Kihanga pamoja na Afisa maendeleo ya Jamii na vijana Manispaa  Enedy Mwanakatwe kwa nyakati tofauti wamesema, serikali inaendelea kuweka mifumo mizuri ili kuhakikisha wazee wote wanaendelea kupata huduma bora.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa