• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA MOROGORO YATAKIWA KUJIBU HOJA ZA CAG KWA WAKATI .

Posted on: June 11th, 2018

MKUU wa mkoa wa Morogoro Dk Kebwe Stephen Kebwe ameiagiza halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuhakikisha hoja zote za Mdhitibi na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambazo hazijajibiwa kwa muda mrefu zinajibiwa.

Pia ameitaka halmashauri  kuhakikisha , inawasilisha hesabu zinazoishia Juni 30, 2018 kabla ya Septemba 30, mwaka huu ili ziweze kukaguliwa .

Mkuu wa mkoa ametoa agizo hilo baada ya Meya wa Manispaa hiyo, Pascal Kihanga kufungua kikao maalumu cha baraza la madiwani wa halmashauri  kupitia majibu ya hoja za ukaguzi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2016/2017.

Dk Kebwe aliitaka halmashauri  ihakikishe kuwa inadai madeni yake yote toka kwa wadaiwa ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wadaiwa sugu ili kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri ya Manispaa.

Pia alitaka kuhakikisha inapeleka fedha za miradi ya maendeleo kwa wakati ikiwa na pamoja na fedha a mfuko wa Jimbo zinazotolewa kwa wabunge.

“ Kutopeleka fedha za miradi ya maendeleo kwa wakati kunasababisha halmashauri kuonekana inashindwa kufanya matumizi ya fedha hizi na miradi kutokamilika kwa wakati , hivyo kupunguza imani ya wananchi kwa Serikali yao” alisema Dk Kebwe.

Mkuu wa mkoa pia alisisitiza kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kiwezeshwe ipasavyo ili fedha zote za miradi zikaguliwe kwa wakati na thamani ya fedha ionekane .

Dk Kebwe aliitaka halmashauri kulipa asilimia 10 ya fedha za wanawake , Vijana na watu wenye ulemavu kutoka katika mapato yake ya ndani kiasi cha Sh 318,164,055 sambamba na kulipa malimbikizo ya madeni ya nyuma.

Mkuu huyo wa mkoa alisema, taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 inaonesha kuwa , mkoa wa Morogoro umefanya vizuri kwa taasisi zake pamoja na halmashauri zote tisa za mkoa kwa kupata hati safi .

Naye Mkaguzi mkuu wa Nje Mkoa wa Morogoro, Mwabwanga Andindilile alisema, pamoja na kupata hati safi , bado madiwani wanalo jukumu la kuhakikisha wanasimamia vyema ukusanyaji wa mapato na kufuatilia matumizi yake ili kuona miradi ya maendeleo inakamilishwa kwa wakati .

kwa upande wake , Meya wa Manispaa hiyo, Pascal Kihanga alimhakikishia mkuu wa mkoa kuwa Baraza hilo kwa kushirikiana na wataalamu litazifanyia kazi hoja hizo ili ziweze kujibiwa na kuiwezesha halmashauri kuendelea kupata hati safi .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa