• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA MOROGORO YAZINDUA MAFUNZO YA WAWEZESHAJI KWA KAYA ZINAZOSHIRIKI KWENYE MPANGO WA TASAF KIPINDI CHA PILI AWAMU YA TATU

Posted on: July 21st, 2020

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro, imezindua mafunzo ya wawezeshaji kuhusu utekelezaji wa kipindi cha pili awamu ya tatu na uhakiki wa Kaya zinazoshiriki kwenye mpango wa TASAF.

Mafunzo hayo yamezinduliwa leo Julai 20,2020 na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa ndani TASAF Makao Makuu, CPA-Christopher Sanga, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa.


Akizungumza na Waandishi wa habari, Sanga, amesema mafunzo hayo ni kujenga uwelewa wa pamoja na namna zoezi hili la uhakiki wa walengwa ambayo ni ya kwanza katika utekelezaji wa kipindi cha pili cha Awamu ya tatu ya TASAF ambacho kilizinduliwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Februali 2020.



Sanga , amesema tathimini ya kipindi cha kwanza cha Awamu ya Tatu TASAF inaonyesha kwamba mpango wa kunusuru Kaya zinazoshiriki kwenye mpango wa TASAF umechangia kwa kiasi kufikiwa azma ya Serikali ya kupunguza umasikini nchini.



Amesema utekelezaji wa kunusuru mpango wa Kaya Masikini pia umewezesha Kaya za Walengwa kujikita kwenye shughuli za kukuza kipato na kijiimarisha kiuchumi ikiwemo Ufugaji, uvuvi, kilimo, na biashara ndogondogo.



Aidha, amesema pamoja na mafanikio hayo Vijiji/Mitaa/ Shehia zilizofikiwa katika kipindi cha kwanza ni asilimia 70% ya Vijiji/Sheria/ Shehia vyote nchini hivyo bado kuna wananchi wanaoishi katika hali duni kwenye maeneo ambayo hayakufikiwa.



“Wakati wa uzinduzi wa kipindi hiki cha pili, Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli, aliagiza kwamba kabla ya shughuli zozote za kipindi cha pili kuanza, uhakiki wa walengwa ufanyike kote nchini ili kuondoa Kaya za walengwa ambazo zimepoteza sifa, mtakumbuka hapo nyuma kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu mpango kuwa na watu wasiostahili wakiwemo watu wasio kuwa masikini, Viongozi, orodha ya walengwa kuwa na watu waliohama au waliofariki ambao hao wote waliitwa walengwa hewa, ili kutekeleza agizo la Mhe. Rais na pia kuondoa dhana iliyojengeka kwa jamii ya kuwemo walengwa hewa, tutaanza uboreshaji kwa kusafisha daftari leo la walengwa”Amesema CPA Sanga.



Amesema kipindi cha pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF ,kitafikia Kaya Milioni moja na laki nne na nusu zenye jumla ya watu zaidi ya Milioni 7 Kote nchini hii ikiwa ni nyongeza ya Kaya laki tatu na nusu ambapo mkazo mkubwa utakuwa ni kuwezesha Kaya zitakazoandikishwa kwenye mpango kufanya kazi kufanya kazi ili kuongeza kipato.



‘”Tunataka kuwa na orodha Halisi ya Walengwa kwenye Masijala ya Kaya za Walengwa , Kaya ambayo haikufika kuchukua malipo yake mara mbili mfululizo Kaya hizo zote lazima ziondolewe” Ameongeza CPA Sanga.



Mjumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii- TASAF, (National Steering Committee ) Eng. Rogatus Mativila, amewataka Viongozi wafanye kazi kwa uadilifu ili wafikie malengo ya Serikali kupitia kipindi cha pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF ya kupunguza umasikini na kuchochea ukuaji wa uchumi ukiwemo ule wa Viwanda ambayo ni agenda muhimu ya Serikali.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, ameupongeza Uongozi wa TASAF Mkao Makuu kwa kuzindua mpango huo ambao unaongeza na kuboresha ili kutoa huduma za jamii na kuendeleza rasilimali Watoto hususani katika upatikanaji wa elimu na Afya.



Kwa upande wa Mratibu wa TASAF Manispaa ya Morogoro, Feliciana Katemana, amesema mpango huo wa kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu , utawezesha Kaya zote zinazoishi katika Mazingira duni zipate usaidizi wa Serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha kufanya kazi na kupambana na umasikini.



Katemana amesema mpango wa kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF Manispaa Morogoro umelenga kuwafikia jumla ya Walengwa 2793 katika Kata 29 ikiwamo Mitaa 164.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa