• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGOR0 YAINGIA MKATABA WA MIAKA 15 NA MWEKEZAJI AFRO OIL INVESTMENT LTD UJENZI WA KITUO CHA MAFUTA MSAMVU

Posted on: April 6th, 2022

MANISPAA ya Morogoro imeingia mkataba wa miaka 15 na Mwekezaji Afro Oil Investment Ltd kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha mafuta Stendi ya Msamvu utakao gharimu kiasi cha shilingi Milioni 750 katika utekelezaji wake.

Mkataba huo umesainiwa Aprili 5/2022 katika Ofisi ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro huku ukishuhudiwa na pande zote mbili wakiwamo Mstahiki Meya, Mkurugenzi wa Manispaa na upande wa Ofisi ya Manunuzi Manispaa ikiongozwa na Mkuu wa Idara Jafari Makulumla , pamoja na watu kutoka Ofisi ya Mipango.

Akizungumza mara baada ya kusainiana mkataba huo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal kihanga, amewataka wawekezaji kutoa taarifa na changamoto zote zinazojitokeza katika kipindi cha mchakato wa utekelezaji ili waweze kushirikiana ili kufanikisha ujenzi wa Kituo cha Mafuta unakamilika.

" Leo nimesaini Mkataba huu, muda wetu ni miezi 6 kama tulivyokubaliana , anzeni mapema ili mnufaike, matarajio yetu ni kuona ndani ya miezi 6 mkataba wetu unaanza kusoma na kituo kinafanya kazi na mnaanza kutulipa fedha zetu ili sasa kila upande uanze kunufaika maana shida yetu sio kupata fedha pekee bali tunataka kutoa huduma kwa wananchi " Amesema Mhe. Kihanga.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Ally Machela, amemtaka mwekezaji kulipa kodi kwa wakati ili Manispaa iweze kuendesha shughuli zake mbalimbali zinazotokana na mapato hayo na vyanzo vyengine.

Kwa upande wa Mwakilishi wa Afro Oil Investment Ltd, amesema watahakikisha wanatekeleza na kuheshimu makubaliano ya mkAtaba waliosaini kwani wana uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika uendeshaji wa soko la Mafuta.

Upande wa Afisa Manunuzi Manispaa ya Morogoro , Jafari Makulumla , amesema mkataba huo utainufaisha Manispaa kupitia tozo za huduma mbalimbali zitakazofanywa na Afro Ltd, tozo za leseni , tozo za ukusanyaji wa taka pamoja na kutoa ajira kwa wananchi wa Manispaa ya Morogoro.

Ikumbukwe kuwa katika mchakato huo ulioanza mwishoni mwa mwaka jana 2021 na kumalizika mwanzoni mwa mwaka huu 2022, ulishindanisha washindani wawili ambao ni Afro Oil Investment Ltd na Salimu Oil Ltd ambapo katika kinyang'anyiro hicho Afro Oil Investment Ltd aliibuka mshindi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa