• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO KUWA CHUO CHA MAFUNZO YA KUWAPANGA MACHINGA_ WAZIRI UMMY

Posted on: September 21st, 2021

WAZIRI wa TAMISEMI, Mhe. Ummy Mwalimu, amesema kwa sasa Manispaa ya Morogoro ndio Manispaa pekee ambayo itakuwa Chuo Cha kujifunza jinsi ya kuwapanga Machinga.

Kauli hiyo ameitoa Septemba 21/2021 wakati wa uzinduzi wa mabanda ya Machinga Soko Kuu la Chifu Kingalu Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Waziri Ummy, amesema moja ya kitu kilichomvutia ni jinsi walivyoweza kupanga vibanda na mfumo bora uliotumika katika kuwaondoa Machinga maeneo yasiyo rasmi na kuwaingiza Sokoni.

"Nimefurahishwa na spidi yenu na utaratibu wenu, nitamke rasmi sasa chuo cha mafunzo ya kuwapanga Machinga kwa Tanzania ni Manispaa ya Morogoro, nipongeze Uongozi wa Mkoa chini ya RC Shigela, Uongozi wa Wilaya chini ya DC Msando, Manispaa ya Morogoro ukiongozwa na Meya wetu Mhe. Kihanga, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe Abdulaziz Abood, Madiwani, wataalamu wa Manispaa pamoja na Machinga kwakweli agizo la Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan mmelitendea haki na mmelifanya kwa haraka na ustadi" Amesema Mhe. Ummy.

Aidha, amewataka Viongozi kuendelea kutatua changamoto nyingine kwani sio Machinga wote ambao wataenea katika Soko hilo.

" Hapa mmejipanga vizuri, angalieni na maeneo mengine ambayo mnaweza kuyapanga kama hivi, wapo Machinga wengi wanaibuka mtaani hivyo mkiwa Viongozi wajibu wenu kuona hao nao mnawajengea mazingira rafiki ya kufanya biashara zao" Ameongeza Waziri Ummy.

Waziri Ummy,amewataka Machinga kuendelea kuwasikiliza Viongozi wao kwani Serikali ipo bega kwa bega na wao kwa kutambua kundi hilo lina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Taifa.

Katika hatua nyingine, Waziri Ummy, amesema Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha mchakato wa kuwa na Idara pekee itakayoshughulikia biashara, Viwanda na uwekezaji pamoja na Dawati la kushughulikia changamoto za Machinga.

Kwa upande wa Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo, ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Morogoro kwa maamuzi sahihi ya kuwapanga Machinga katika maeneo rafiki.

Prof. Kitila, amesema Serikali kupitia Ilani ya CCM imeweka mpango wa kutoa ajira zaidi ya Milioni 800 hivyo kuwawezesha Machinga ni njia ambayo ajira zitazalishwa kwa wingi.

" Tukiwa na Machinga sehemu moja, tutakuwa na bodaboda, bajaji ambao watakuwa wanatoa huduma eneo hilo, kwa maana hiyo ajira zitaongezeka na ajira hizi sisemei ajira za vyeti nazungumzia ajira za mzunguko katika biashara " Amesema Prof. Kitila.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Martine Shigela, amesema chini ya uongozi wake atahakikisha Machinga wanaendelea kusimamiwa vyema kwani wao wanahaki kama ilivyo watu wengine.

" Serikali imewatambua Kama kundi muhimu, hivyo wajibu wetu Viongozi kuwasimamia na kutatua changamoto zao" Amesema RC Shigela.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe Albert Msando, amesema lengo lake ni kuona Machinga hawawi tena katika kundi la ziada kama ilivyozoeleka.

" Machinga wamekuwa wakichukuliwa Kama kundi la ziada lakini kwa Sasa tumewatambua na tumewahakikishia maisha marefu katika Soko hili ili waendelee kujitafutia riziki" Amesema DC Msando.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe Pascal Kihanga, amesema Manispaa ya Morogoro itaendelea kuwalinda Machinga na kuwatafutia maeneo rafiki ya kufanyia kazi.

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe Abdulaziz Abood, amesema watahakikisha wanatengeneza mifumo rafiki ya kuhakikisha Machinga hao wa Soko Kuu la Chifu Kingalu biashara zao zinafanyika na wanapata faida.

Vibanda hivyo vipo 780 kwa Mpango wa awali ambapo idadi kamili inatakiwa kuwa 1000 huku kila kibanda kikigharimu kiasi Cha Shilingi 230,000/=.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa