• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO YAFUNGA KWA KISHINDO MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: July 3rd, 2023


MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mheshimiwa Pascal Mwendishule Kihanga, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa fedha ambazo Serikali imekuwa ikizileta kwenye Manispaa hiyo na kufanikisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta za Afya, Elimu Msingi na Sekondari.

Mstahiki Meya Kihanga ametoa shukurani hizo wakati alipokuwa akihutubu katika Mkutano wa Kawaida wa Mwaka wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Morogoro ambapo ameeleza kwamba katika mwaka huu wa fedha 2022/2023, Manispaa imekusanya jumla ya shilingi 80,823,086,209.00 kutoka Serikali Kuu na katika mapato yake ya ndani kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa Halmashauri na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

“Mpaka hivi leo, kutoka Mapato ya Ndani, Manispaa imekusanya jumla ya shilingi 12,653,562,636.00 sawa na asilimia 100 ya makisio ya mwaka, huku shilingi 68,169,523,572.00 zikiwa zimepokelewa kutoka Serikali Kuu,” alifafanua Mstahiki Meya Kihanga.

Aidha, katika hotuba hiyo Mstahiki Meya Kihanga amebainisha mafanikio ya kisekta ambayo Manispaa imeyapata kutokana na makusanyo ya fedha hizo ikiwemo kuanza kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika kata ya Kihonda, ujenzi wa wodi ya wazazi katika Zahanati ya Konga, ujenzi wa Kituo cha Afya katika kata ya Tungi, ujenzi wa zahanati nne katika maeneo ya Uwanja wa Taifa, Mazinmbu,Mlapakolo na Kiegea.

Vilevile, Manispaa imefanikiwa kujenga majengo saba ya utawala katika shule za sekondari Mazimbu, Mbuyni Modern, Kola, Mkundi Mlimani, Mwembesongo, Mafiga na Tungi, ujenzi wa maabara za Sayansi, ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari, ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa katika shule za msingi na sekondari, ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule za msingi na ujenzi wa shule tano mpya za msingi zikiwemo shule za Jitegemee na Kihonda Maghorofani, na ujenzi wa jengo la machinga katika eneo la Fire.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Morogoro, Mheshimiwa Fikiri Juma amelipongeza Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana vyema na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo pamoja na Menejimenti yake katika kutekeleza shughuli za maendeleo zenye lengo la kutoa huduma bora kwa jamii kulingana na Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kwa kauzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma na Serikali kwa ujumla.

“Ombi langu ni kwamba muongeze juhudi katika kutekeleza mpango wa kuendeleza eneo la biashara katikati ya mji (CBD), ili kuwa na matumizi bora ya ardhi katika maeneo ya mjini kwa kuwa mpango huu unahamasisha ujenzi wa maghorofa badala ya ujenzi wa majengo ya chini.”

Mkutano wa Kawaida wa Mwaka wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Morogoro umefanyika tarehe 30.06.2023 katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa hiyo.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa