• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO YAFURAHISHWA NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA DAMPO LA KUTUPIA TAKA NGUMU JIJI LA MBEYA

Posted on: June 25th, 2024

HALMASHAURI ya Manispaa ya  Morogoro imefurahishwa na usimamizi wa shughuli za dampo la kutupia taka ngumu katika Jiji la Mbeya.

Kauli hiyo imetolewa na  Meya wa Manispaa ya Morogoro Mh. Pascal Kihanga, katika ziara ya mafunzo ya kujifunza usimamizi wa miradi ya maendeleo na ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza mara baada ya ziara kukamilika, Mhe. Kihanga, amesema usimamizi wa dampo ambao unafanywa na Jiji la Mbeya umekuwa wa kisasa na wenye lengo la kuhakikisha kuwa Jiji linakuwa safi masaa 24.

“Kuna mambo makubwa tumejifunza kwa wenzetu wa Jiji la Mbeya, wenzetu kwenye usafi wametuacha mbali sana , kuanzia uzoaji wa taka, ukusanyaji wa mapato, wenzetu wamejikita sana kulinda dampo la taka na kulisimamia lakini kuhusu ukusanyaji wa taka wameviachia vikundi kazi na makampuni jambo ambalo kwetu sisi tumebakia kusimamia dampo na ukusanyaji wa taka , kuna cha kujifunza tutakaa na wataalamu wangu na madiwani tutaona na sisi namna ya kuboresha ili Mji wetu ambao ni Jiji tarajiwa liwe safi kama ilivyo kwa wenzetu wa Jiji la Mbeya” Amesema  Mhe. Kihanga.

Mhe. Kihanga,amesema Manispaa ya Morogoro imeshaanza ujenzi wa Dampo la kisasa ambapo amesema dampo hilo linakidhi matakwa yote ya kiafya na kimazingira, ”Sanitary Landfill’.

Kihanga,amesema Uendeshaji wa madampo kwa teknolojia ambayo Manispaa inakwenda kulitekeleza  hutumika sehemu nyingi duniani hususan katika nchi zinazoendelea.

Kwa upande wa Kaimu Afisa Mazingira Manispaa ya Morogoro, Alex Roman,amesema uchafuzi wa mazingira kwa maji machafu yanayotirikika ambayo husababishwa na kujichuja kwa taka hizo (Leachate) ni sehemu ya changamoto zinazoikabili Manispaa ya Morogoro katika eneo ambalo dampo lipo kwa sasa.

Roman, amesema ili kukabiliana na tatizo hilo, manispaa ya Morogoro imeamua kujenga Dampo la Kisasa lenye eneo maalumu la kutupa taka(Cell) na bwawa la kuhifadhi maji machafu yanayotokana na kujichuja kwa taka (Leachate pond).


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa